Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Wachambuzi kesho kazi wanayo kwenye kusifiasifia 😂 wachambue watakavyochambua ila sisi mashabiki wa Chelsea hatutaki kelele za kutaka ubingwa.
 
Shida ya utd ni kule mbele, tuna wachezaji wa hovyo wasio wapambanaji yaani unakuta mchezaji leo yuko vizuri kesho hamna kitu, allikuwepo Martial, Lindgad na Rashford wakaondoka wawili akabaki mmjoja, sasa kaibuka Garnacho . Kwa timu yenye kutaka matokeo hawa wawili hawapaswi kuanza ni bora wauzwe au waanzie sub. Leo Kocha kanifurahisha sana kuwatema naona kachoshwa nao.
 
KUANZIA LEO.

Marufuku jezi ya Man United kufuliwa kwa maji ya chumvi au sabuni ya magadi.

Marufuku shabiki yeyote wa Man United kusimama kwenye daladala, kama siti zimeishia akalie hata siti ya dereva.

Marufuku kwa shabiki yeyote wa Man United kuongozana na mtu alievaa jezi ya Arsenyau, kufanya hivyo ni kuidhalilisha jezi nyekundu na nembo ya club.

Jua likishazama ni marufuku shabiki wa Utd kutembea peke yake, sogea kituo cha polisi cha karibu utapatiwa ulinzi mpaka sehemu unayoenda, kuna watu wana husda sana.
 
Huyu Pep aongeze mkataba mrefu wa kutosha pale City, naona wapinzani wake EPL wameanza kumjulia namna ya kucheza naye.
 
Ila mashabiki wa Man Utd tuna shida sana, yaani allypipi leo katembea tokea Manzese mpaka Kariakoo na paja la mbuzi mkononi
1734360788995.jpg
1734360737594.jpg
 
Jana tulikuwa na moment kadhaa za intensity za kuutaka mpira Kwa nguvu na Kwa haraka sana, hii ni ishara nzuri. Kwa jinsi system ilivyo Inahitaji kujitoa sana, kama umezoea kucheza nusu uwanja basi pole sana, Kwa jinsi back three zinavvyofanya kazi lazima timu nzima muwe tayari kukimbizana. Tunatakiwa misimu miwili mbele timu iwe na intensity ya Hali ya juu Kwa maeneo yote.

Lazima tuongeze kiungo ya kazi kweli kweli wa kusaidiana na Ugarte, huyu punda (ugarte) anakimbia na fiziki yake ipo vizuri, asije akaumia kipindi hichi tutakuwa exposed sana kwani Bado hatujajipata.

Mount anafaa kabisa Kwa system ya jamaa, kitakachomuua ni majeruhi tu daah. Tunahitaji kiungo mkali wa kusaidia pale kati. Muda huu ni wa kuwakimbiza wachezaji na kuhakikisha wanasuffer kweli kweli Ili tuondoe wachovu na wavivu wote watakao kuwa exposed na hii system.

Kwa system ya jamaa ni rahisi kujua wachovu ni akina nani maana unawaona kirahisi in training na kwenye game, tukiingia sokoni unajua kabisa huyu Kwa system yetu hatufai. Hatutaki wachezaji makobe na wavivu.
 
Manjesta bhana waliingia kwenye box la Arsenal mara 6 tu ndani ya dk 94

Hii ni record toka mwaka 2017 ambapo manjesta waliingia mara chache kwenye box la mpinzani,ilikuwa dhidi ya Arsenal

Yaani kila baada ya dk 15 ndio manjesta wanafika mara moja kwenye box la Arsenal

Ni timu ambayo Kwenye usajili imetumia zaidi ya €200m
Wazee wa kukalia tawi, Chelsea washakuacha huko
 
Jana tulikuwa na moment kadhaa za intensity za kuutaka mpira Kwa nguvu na Kwa haraka sana, hii ni ishara nzuri. Kwa jinsi system ilivyo Inahitaji kujitoa sana, kama umezoea kucheza nusu uwanja basi pole sana, Kwa jinsi back three zinavvyofanya kazi lazima timu nzima muwe tayari kukimbizana. Tunatakiwa misimu miwili mbele timu iwe na intensity ya Hali ya juu Kwa maeneo yote.

Lazima tuongeze kiungo ya kazi kweli kweli wa kusaidiana na Ugarte, huyu punda (ugarte) anakimbia na fiziki yake ipo vizuri, asije akaumia kipindi hichi tutakuwa exposed sana kwani Bado hatujajipata.

Mount anafaa kabisa Kwa system ya jamaa, kitakachomuua ni majeruhi tu daah. Tunahitaji kiungo mkali wa kusaidia pale kati. Muda huu ni wa kuwakimbiza wachezaji na kuhakikisha wanasuffer kweli kweli Ili tuondoe wachovu na wavivu wote watakao kuwa exposed na hii system.

Kwa system ya jamaa ni rahisi kujua wachovu ni akina nani maana unawaona kirahisi in training na kwenye game, tukiingia sokoni unajua kabisa huyu Kwa system yetu hatufai. Hatutaki wachezaji makobe na wavivu.
Dalot,kobie gernacho rasshford washaanza kutema bungo🤣🤣
 
Wewe manjesta unagombea kushuka daraja🤣🤣🤣

Pumbaff kabisa ,

Chelsea anajua kabisa hana pumzi
Nyambafu gape langu na wazee wa tawi ni points 8 tu, soon nakukuta jiandae 😂
 
Back
Top Bottom