Mamlaka za maji za Tanzania zina dharau kubwa sana kwa wananchi, hakuna usimamizi wa watendaji

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
877
4,106
Mamlaka za maji nchini zina kiburi sana, hakuna nidhamu ya watendaji. Miradi ya maji wanapiga, kuunganisha watu maji awataki, wanabambikia wenye maji bili, ukienda ofisini kwao hakuna anayekuchukulia kama mteja kila mtu yupo busy na masuala yake, wengi wana elimu ndogo ya uchumi na hivyo wanaamini wao niwadhibiti huduma kuliko kutoa huduma.

Matokeo yake ni nini! Kwa sasa wametengeneza madeni mengi yasiyolipika kutokana na kujipangia bili wanazoona wao zinafaa. Mapato ya mamlaka hizi yanakwenda kushuka na watu wameanza kujiunganisha maji kinyemela mtaani.

Kwenye mamlaka nyingi kwa mujibu wa CAG kuna madeni mengi, maji yanapotea pale mabomba yanapopasuka na response kwenye huduma aidha kupokea simu au kutunza kumbukumbu za malalamiko hazipo.

Ukifuatilia zaidi unabaini ndani ya mamlaka mfano DAWASCO ya huko jijini kwa wafanya biashara wametengeneza vishoka ambao ni watumishi wanaobambikia watu bili then wanapokea rushwa na kuchepusha maji. Kuthibitisha hayo niwatonye DAWASCO wakague idadi ya watu waliokatiwa maji kwa miezi sasa na wametulia, means waliokata maji walifanya mchongo maji yapatikane kwa mgongo mwingine.

DAWASCO wapitie malalamiko ya wateja watabaini kwamba idadi ya wateja wanaojenga mahusiano na watendaji wao inaongezeka kwa kasi means kuna biashara inafanyika. Wapitie response za watendaji wao watabaini kila mtendaji anatumia namba binafsi kutongoza mteja na wanaotonhozeka wanapewa huduma aidha kwa mgongo wa nyuma au mfumo halali.

Kwa msingi huu, endapo waziri utaendelea kuwaacha watu wa DAWASCO na mamlaka nyingine za maji wajiamulie cha kufanya; endapo wateja wataendelea kukatiwa maji mkatulia bila kufuatilia chanzo; na endapo watendaji wataendelea kukalia kimya malalamiko ya wateja nakuhakikishia utaondoka. Mtu mmoja anawezaje kuchepusha mradi mzima wa mabomba ya maji kutoka mtaa A na kupeleka mtaa B bila mamlaka kujua?

Mhe. Waziri, ulichoambiwa na Chongolo Dodoma kikufundishe jambo, tengua teuzi za hawa watu wanaotia doa nchi, la sivyo ukiendelea kukaa ofisini utapoteza V nane unayotembelea.
 
Ni sahihi asilimia kubwa ya watendaji hasa hawa wasoma mita wengi wao si waaminifu japo wapo wanaofanya kazi kwa uaminifu.Japo changamoto ni TAMAA tu maana wengi wao kwenye mshahara wasisingizie kabisa,msoma mita tu ambae hajaajiliwa tu analipwa zaid ya laki tano.
 
Waziri mwenye dhamana na hii wizara tunakupa taarifa za kushtua za kuongezeka kwa gharama mara dufu za Ankara za maji.Ni mshtuko Arusha nzima.Hii sio huduma tena bali ni anasa.

Wananchi tunashangaa kuna nini nyuma ya pazia katika hili? Yani kutoka kulipa 3000,5000,4000 mpaka kwenye 70,000,900000 mpaka laki naa!

Hata kama ni mpango wa kukusanya mapato ,au kupanda kwa gharama za uendeshaji sio katika namna hii kwakweli.Huu ni ukandamizaji wa wazi kwa wananchi na wengi wataachana na maji yenu kwa kutafuta Alternative zingine za kupata maji.

Pia mamlaka imekuwa ni wabambikizaji wa madeni yasiyoeleweka yametoka wapi?

Moja ya hotuba yako uliwahi sema "Ni marufuku kukata maji kwa wateja kwa sababu maji ni huduma" Sasa nakwambia watanzania wanabambikiwa madeni ya uongo na wanakatiwa maji.Na hii inatokana na kuwa mamlaka ina utaratibu wa kulipa mishahara pamoja na posho kutokana na makusanyo yaliyopatikana.

Mwisho:
Mfumo huu wa huduma ya maji si rafiki kabisa kwa watanzania na Rais Samia Suluhu aliangalie hili litaleta chuki kwa gharama kuwa kubwa hivi.

Pre paid meter zifungwe haraka sana sana ili iwe kama umeme.
 
Ni sahihi asilimia kubwa ya watendaji hasa hawa wasoma mita wengi wao si waaminifu japo wapo wanaofanya kazi kwa uaminifu.Japo changamoto ni TAMAA tu maana wengi wao kwenye mshahara wasisingizie kabisa,msoma mita tu ambae hajaajiliwa tu analipwa zaid ya laki tano.
Kumbe wasoma mita nao awajaajiriwa wanapiga pat time? Ndo maana dili zimekuwa nyingi sana...........kata kata za maji zimekuwa nyingi na uchepushaji unakua kwa kasi.

Natabiri pamoja na uwekezaji uliowekwa kwenye mamlaka kama DAWASCO soon itaanguka kwa kukosa wasimamizi.........wamekuwa sana mabosi.

Mhe. Waziri akiomba idadi ya miradi iliyochepushwa, akiomba trend za ukataji maji kwa wateja, akiomba idadi ya malalamiko mitandaoni na kwenye ofisi za mamlaka za maji atabaini kwamba tumekwama.

Mh.Rais anakwamishwa makusudi na wasimamizi wa huduma na miradi......akiwekeza kwenye tumbua tumbua akawarudisha majumbani wanaoshindwa kuperfom nadhani tatizo la ajira litapungua nchini kwa sababu watu sahihi watapata ajira na wachumia tumbo watarudi nyumbani kujitaftia
 
Waziri mwenye dhamana na hii wizara tunakupa taarifa za kushtua za kuongezeka kwa gharama mara dufu za Ankara za maji.Ni mshtuko Arusha nzima.Hii sio huduma tena bali ni anasa.

Wananchi tunashangaa kuna nini nyuma ya pazia katika hili? Yani kutoka kulipa 3000,5000,4000 mpaka kwenye 70,000,900000 mpaka laki naa!

Hata kama ni mpango wa kukusanya mapato ,au kupanda kwa gharama za uendeshaji sio katika namna hii kwakweli.Huu ni ukandamizaji wa wazi kwa wananchi na wengi wataachana na maji yenu kwa kutafuta Alternative zingine za kupata maji.

Pia mamlaka imekuwa ni wabambikizaji wa madeni yasiyoeleweka yametoka wapi?

Moja ya hotuba yako uliwahi sema "Ni marufuku kukata maji kwa wateja kwa sababu maji ni huduma" Sasa nakwambia watanzania wanabambikiwa madeni ya uongo na wanakatiwa maji.Na hii inatokana na kuwa mamlaka ina utaratibu wa kulipa mishahara pamoja na posho kutokana na makusanyo yaliyopatikana.

Mwisho:
Mfumo huu wa huduma ya maji si rafiki kabisa kwa watanzania na Rais Samia Suluhu aliangalie hili litaleta chuki kwa gharama kuwa kubwa hivi.

Pre paid meter zifungwe haraka sana sana ili iwe kama umeme.
Kwa hiyo huu ubambikiaji wa bili kumbe unatumika kwa lengo la kuongeza mapato ili watu walipane posho?
Sehemu yoyote inayoruhusu vibarua kwa mgongo wa posho lazima rushwa itatawala. Usishangae watoto wa viongozi wa mamlaka za maji wakawaajiri watoto wao kama vibarua na kuwalipa posho kwa kuumiza wananchi.

Posho ya laki tano wakati kima cha chini cha mshahara kimetangazwa ni 370000? Means bora uwe kibarua kuliko kupata ajira rasmi si ndiyo.............rushwa rushwa rushwa rushwa rushwa
 
Back
Top Bottom