MWACHE CHAIRMAN AFANYE VITU VYAKE....ee bwana ee!..hivi unamjua king of kings?Hisoria ni kwamba huyo jamaa alikuwa jambazi mkubwa sana.Kawapa sana tabu manjagu hapa bongo miaka ya sabini na early eighties,alikuwa anakaa tandika,siku alivopigwa shaba watu tulipumua saana!! jamaa alikua nuksi.
Anywayz,I just wanted to share those memories with you bro!...cause your name reminded me of him!
Tatizo la Lowasa sio kura za watanzania kwa sasa. Tatizo lake ni namna gani atajijenga ndani ya chama ili ateuliwe. Lowassa haishi leo, anaishi June/July 2015 wakati wa kura za maoni CCM. Akipenya hapo nani atamzuia tena bwana? Na humo CCM sio kwamba wanambania kwa sababu ati hawampendi. Sababu hasa ni kwamba wapo wengi wenye malengo ya 2015 na wapo wanaomtukuza EL mchana lakini usiku wanamloga ili nao malengo yao yapate kutimia. So kazi ipo kichama zaidi. Mambo mengine endelea kufuatilia habari hizi, thanks to mugumu.
MWACHE CHAIRMAN AFANYE VITU VYAKE....ee bwana ee!..hivi unamjua king of kings?Hisoria ni kwamba huyo jamaa alikuwa jambazi mkubwa sana.Kawapa sana tabu manjagu hapa bongo miaka ya sabini na early eighties,alikuwa anakaa tandika,siku alivopigwa shaba watu tulipumua saana!! jamaa alikua nuksi.
Anywayz,I just wanted to share those memories with you bro!...cause your name reminded me of him!
HUYO M/KITI WAKO ALIANZA UFISADI ZAMANI SOMA HAPO CHINI
Kikwete, kura na watuhumiwa ufisadi
Na Ndimara Tegambwage - Imechapwa 22 September 2010
Uchambuzi
JAKAYA Mrisho Kikwete, yule mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ameonyesha yuko tayari kumfukua rafiki yake wa siku nyingi, Edward Lowassa kutoka kwenye kifusi.
Vyombo vya habari vimemnukuu Kikwete akisema kuwa hajawahi kuona mchapakazi kama Lowassa na kwamba ndiyo maana anamwombea kura.
Angalau magazeti matatu ya kila siku yameandika kuwa Kikwete alisema, Yaliyopita si ndwere, tugange yajayo; kwa maana kwamba yaliyomsibu rafikiye Lowassa sasa yawekwe kando.
Katika mazingira ya uandishi wa kushawishi na kushawishiwa, yawezekana Kikwete hakusema yaliyochapishwa; lakini usalama wa mchambuzi ni kwamba si Kikwete wala maofisa wake, wamekanusha taarifa hizo kwa wiki nzima sasa.
Kikwete alikuwa akihutubia mikutano ya kampeni za urais, ubunge na udiwani huko Monduli na Mto wa Mbu, mkoani Arusha.
Kikwete alishika mkono wa Lowassa, akauinua juu kwa staili ya makomredi, akionyesha kuwa yaliyokuwa yamemsibu Lowassa yameisha na kwamba sasa wamchague kuwa mbunge wao.
Yote haya yana ujumbe maalum; kwamba Kikwete alikuwa anamuibua rafiki yake Lowassa kutoka kwenye kifusi cha lawama, shutuma na tuhuma zilizomwelemea, hasa kuhusiana na kashfa ya mkataba wa kufua umeme kati ya serikali na kampuni ya Richmond.
Kauli za Kikwete juu ya Lowassa na hasa kibwagizo kuwa ni mchapakazi hodari, vimethibitisha uvumi uliokuwepo kwamba kabla ya mchakato wa kuwania urais ndani ya CCM, ililazimu Kikwete akutane na Lowassa ili kusafisha njia yake.
Uvumi uliokuwepo ni kwamba Kikwete alimwita Lowassa na kumuuliza iwapo atagombea urais. Jibu lililopatikana ni kwamba Lowassa alisema hajafanya uamuzi.
Ni wakati huo baadhi ya viongozi ndani ya CCM walikuwa wakisutana na wengine kusikika wakijiapiza kusimamisha mgombea wao wa urais Lowassa akitajwa mara nyingi.
Mmoja wa watu wa karibu na Lowassa alinukuliwa akisema kuwa kauli yake kwamba hajaamua iwapo atagombea, ilimlazimu Kikwete atafute suluhu na mwenzake kwa maana ya nikune hapa, nitakukuna pale.
Taarifa zinasema ilikubaliwa kuwa hata kama Lowassa hataki au hawezi kugombea, basi akae kimya na asijaribu kumharibia mwenzake. Mkataba. Hakika Lowassa hajavunja mkataba huo.
Yaliyotokea Monduli ndiyo yalitokea Rombo, mkoani Kilimanjaro. Kikwete alimwinua Basil Mramba na kumwombea kura kwa maelezo kuwa ni panga la zamani ambalo lingali na makali.
Bila shaka Kikwete amefanya au atafanya hivyo kwa wengine zaidi ya Lowassa na Mramba.
Kikwete alikarabati magereza ya Dar es Salaam na kuyapa hadhi ya makazi hata kama ni kwa kutengwa na ndugu zako. Akawakamata aliochekecha na kuona ni watuhumiwa wa ufisadi. Akawaweka ndani na kuwafungulia mafaili mahakamani.
Bila shaka kuna tofauti kati ya kufungulia mtu faili mahakamani na kufungulia mtu mashitaka. Hilo litajieleza kadri tunavyofuatilia kinachoendelea mahakamani.
Wakati Lowassa alijiuzulu uwaziri mkuu, tena katikati ya tuhuma ambazo bado zingali mbichi kabisa, Mramba anakabiliwa na mashitaka ya kutumia ofisi yake vibaya na kusababisha hasara kwa serikali.
Kwa mujibu wa alichofanya Kikwete, tuhuma ambazo hazijaisha nje au ndani ya mahakama hazina uzito. Anawapigia kampeni wahusika waingie bungeni kama walivyo.
Bila shaka atafanya hivyo kwa watuhumiwa wengine; kwa mfano Andrew Chenge ambaye, pamoja na tuhuma, anaendelea kuwa katika kamati ya nidhamu ya CCM.
Tukirudi kwa Lowassa, wachunguzi wamekuwa wakieleza, waziwazi na kimyakimya, kuwa mwanasiasa huyo ana ndoto za kuwania urais, kama ambavyo matendo kadhaa yameelekeza huko.
Hata Kikwete anajua vema, kwamba Lowassa ana wakuu wake wa wilaya na mikoa; kwamba ana maofisa utawala na wakurugenzi wa serikali za mitaa. Kwamba ana wafuasi miongoni mwa wabunge. Analenga mbali.
Hii ndiyo inafanya wachunguzi watwambie kuwa Lowassa ana chama na serikali, ndani ya chama na serikali anayoongoza Kikwete.
Kwa hiyo, kunyamza kwa Lowassa ili Kikwete amalizie ngwe yake ndiko kunatajwa kuwa sehemu ya mkakati wa Kikwete wa kulegeza wabunge waliokuwa wameshupalia Lowassa kuhusiana na kashfa ya Richmond.
Kilichoitwa muwafaka wa kamati ya Nishati na Madini, kwa upande mmoja, na serikali kwa upande mwingine, ndicho kilizimua ukali wa wabunge waliojitambulisha kuwa wapambanaji dhidi ya ufisadi, na hasa juu ya Richmond na Lowassa.
Kupondeka kwa wabunge, kwa shabaha ya kununua upendeleo ndani ya CCM ili wasitemwe katika mchakato wa kutafuta wagombea, ndiko kulitoa ushindi wa kwanza wa Lowassa dhidi ya maadui wake.
Hatua hii ndiyo inaitwa usaliti wa wabunge wa CCM kwa wananchi na hasa wanaharakati, waliosimama imara na kamati ya bunge kuweka watuhumiwa wote matumbo moto.
Hoja ya ufisadi wa Richmond iliwaunganisha wananchi na kundi la wabunge, hata kama baadaye iligundulika kuwa kundi hilo lilitaka kutafuta upenyo tu wa kisiasa na ndiyo maana likajisalilisha.
Ni rahisi kwa CCM kuvunja kila kitu, lakini je, ni rahisi kwao na hususan kwa mwenyekiti wao kusikiliza kile Watanzania wanataka na kutenda katika hicho badala ya kutenda katika matakwa ya marafiki? Maana twaweza furahia kuvunjwa kwa kila kitu, lakini wanapokuwa nje ya mfumo wa utawala wa CCM wakawa bado wanawaendesha walioko ndani ya mfumo kwa mtindo wa remote control.....binafsi sidhani kama hatua hii ni ya kushadadia sana.
ohh mimi nimelewa na kukuzwa na protocol....maraa ohhh....kobello kaa kimya post zako na ubishi usio na maana hatuuhitaj hasa katika jukwaa hili na katika thread hii...kama vipi kakojoe then ulale
Hapo kwenye red hapo....akakojowe wapi? maana sehemu za kukojolea ziko nyingi....tafadhali malizia sentensi yako ili Kobello akuelewe! tehe tehe...teheeee....
Usijali mpendwa huo ndiyo ushuhuda wenyewe asipo sema hivyo haitakuwa fulfilled bora amesema ili litimie kwa kasi na kwa haraka anadhani kila mara anaongea na watu wa kawaida; hajui kuwa some of us are Kings and our words are decree. As I said so shall it be ninasema nakurudia tena hakuna fisadi atakaye pona nyakati hizi never the mission is completed imebaki utekelezaji!
You watch and see confusion wanayoiendea hawa watesi wa nchi yetu; and some of us will be just some where laughing na kugonga glass za ushindi.
pole sana wanaCCm maana hapa mtu wa kutoa kafara ni makamba
UVCCM walianza propaganda za kuwa makamba ndo anayumbisha chama lakini hizi ni mbinu za mafisadi kuwatuma wamshamulia makamba ili aonekane ndo kakiaribu chama na wenyewe weendelee kupeta
HII mbinu ni mbaya maana chama bado hakijasafishika MAFISADI KAMA RA BEN EL CHENGE WANADUNDA MTAANI
Usijidanganye. Ikitokea Lowassa akatumia njia yoyote ile kuteuliwa kuwa mgombea wa CCM, lazima atashinda uchaguzi mkuu. Sio kwa sababu namkubali, bali namfahamu. Kwa hili ninaweza ku-bet hata nyumba yangu, maana najua akiteuliwa atapita na mimi nitakuwa na nyumba mbili.
Kwa vile ulikuwa raised na viongozi wezi unafikiri kila mtu ni mwizi.
kwa mawazo yako unafikiri Tanzania haitakuja pata viongozi wazalendo kamwe, kuna nchi zilikuwa masikini wa kutupwa kwa sababu ya viongozi wake kudhani ni wao tu waliozaliwa kuongoza lakini zilipopata viongozi wazalendo mambo yalibadilika, think of China, Hong kong, Kenya, SA etc.
Unawazimu wewe....huyo Lowasa wako atakuwa Rais kwa wizi wa kura na kwa nguvu ya dola....lakini kamwe hatakuwa Rais kwa mapenzi ya mungu na watanzania walio wengi. Tafakari....
Huyo consultant atakuwa alipewa hadidu ya rejea moja.
Ukweli ni kuwa ushindi kiduchu wa JK ni kwa sababu ya uwezo wake mdogo. Huo uwezo mdogo unafanya ashindwe kushughulikia mambo mengi ikiwemo ufisadi. Na wananchi wanamwona kama msanii fulani tu. Hivi ulishawahi kusikia nchi ina ambulance za bajaji, zimamoto za bajaji na matrekta ya power tillers sijui huku viongozi wakitesa na magari yenye thamani ya shs milioni 200 kila moja ikaendelea? Unategemea kiongozi wa namna hiyo atapendwa na wananchi wake?
Nakubaliana na wewe kuwa uwezo wa JK ni mdogo sana ndio maana hata sasa anatapatapa, bila kujua waTZ wanahitaji nini. mfano mafisadi alitakiwa kuwafuuza tangu 2007/2008 sasa leo kumeshakucha yeye ndio anatafuta shuka ajifunike huyu rais wetu kweli ni kilaza.
Kuhusu matokeo ya uchaguzi sio ushindi mwembamba bali alishindwa kwa kupata chini ya asilimia 30, sasa ndio wanatafuta mchawi leo.
JK is very weak, na ana njama za kumtengenezea membe njia ya urais, mwambieni yatamtokea puani maana si wananchi wako nyuma yake wala mafisadi ila wapo mbayuwayu kama kina makamba, mkuchika, Ridhiwani, Lukuvi angalia CV zao kama mimi nawadanganya.
pole sana wanaCCm maana hapa mtu wa kutoa kafara ni makamba
UVCCM walianza propaganda za kuwa makamba ndo anayumbisha chama lakini hizi ni mbinu za mafisadi kuwatuma wamshamulia makamba ili aonekane ndo kakiaribu chama na wenyewe weendelee kupeta
HII mbinu ni mbaya maana chama bado hakijasafishika MAFISADI KAMA RA BEN EL CHENGE WANADUNDA MTAANI
Namsikitikia kuliko maelezo maana is the one who is going to fall a victim yeye huyo huyo hana la kufanya sasa acha ajimalize kwanza then tukae chini kuona tunaelekea upande upi! What I am sure of is the future of Tanzania is now brighter than ever!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.