Mambo 10 muhimu ya kuzungumza kabla ya ndoa ili kuepuka maumivu baadae

Mambo 10 muhimu ya kuzungumza kabla ya ndoa ili kuepuka maumivu baadae

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Kabla ya Ndoa, haya ni mambo muhimu sana mnayopaswa kuyazungumza ili kuepuka maumivu na kuvunjika moyo baadaye:

1. Fedha - Tutazisimamiaje? Pamoja au kila mmoja kivyake?
Nani ataweka akiba, nani atatumia, na tufanye nini mambo yakibana?

2. Watoto - Je, tunataka watoto?
Wangapi? Na ni maadili gani tunataka kuwalea nayo?

3. Familia - Wazazi na ndugu watakuwa na nafasi gani katika maisha yetu?
Tutawekaje mipaka bila kuleta chuki au kinyongo?

4. Majukumu ya Nyumbani - Nani atafanya nini nyumbani?
Je, majukumu yote atambebeshwa mwanamke, au tutabeba maisha pamoja?

5. Uaminifu - Kukosa uaminifu kunamaanisha nini kwako?
Ni kimwili, kihisia, au hata mawasiliano ya siri (DMs) ambayo wengine hudai "hayana maana"?

6. Migogoro - Matatizo yanapotokea, tunapiga kelele, tunanyamaza, au tunakaa chini na kuyazungumza kwa hekima?

7. Mipango ya Maisha - Tutaishi wapi?
Ni ndoto zipi tunazozipigania pamoja, na je, tunakua katika mwelekeo mmoja?

8. Ukaribu (Intimacy) - Kama watoto hawatapatikana, itakuwaje?
Ukaribu ukibadilika, tutabaki waaminifu au tutaanza kutengana taratibu?

9. Ukuaji na Mabadiliko - Watu hubadilika.
Mmoja wetu akiacha tabia, imani au malengo ya zamani, tutakua pamoja au tutatengana?

10. Usalama wa Kihisia - Je, tunaweza kuwa wazi bila hofu?
Mmoja wetu akiwa dhaifu, amechoka au ameshindwa, je, hii ni mahali salama pa kupumzika?
 
Kabla ya Ndoa, haya ni mambo muhimu sana mnayopaswa kuyazungumza ili kuepuka maumivu na kuvunjika moyo baadaye:

1. Fedha - Tutazisimamiaje? Pamoja au kila mmoja kivyake?
Nani ataweka akiba, nani atatumia, na tufanye nini mambo yakibana?

2. Watoto - Je, tunataka watoto?
Wangapi? Na ni maadili gani tunataka kuwalea nayo?

3. Familia - Wazazi na ndugu watakuwa na nafasi gani katika maisha yetu?
Tutawekaje mipaka bila kuleta chuki au kinyongo?

4. Majukumu ya Nyumbani - Nani atafanya nini nyumbani?
Je, majukumu yote atambebeshwa mwanamke, au tutabeba maisha pamoja?

5. Uaminifu - Kukosa uaminifu kunamaanisha nini kwako?
Ni kimwili, kihisia, au hata mawasiliano ya siri (DMs) ambayo wengine hudai "hayana maana"?

6. Migogoro - Matatizo yanapotokea, tunapiga kelele, tunanyamaza, au tunakaa chini na kuyazungumza kwa hekima?

7. Mipango ya Maisha - Tutaishi wapi?
Ni ndoto zipi tunazozipigania pamoja, na je, tunakua katika mwelekeo mmoja?

8. Ukaribu (Intimacy) - Kama watoto hawatapatikana, itakuwaje?
Ukaribu ukibadilika, tutabaki waaminifu au tutaanza kutengana taratibu?

9. Ukuaji na Mabadiliko - Watu hubadilika.
Mmoja wetu akiacha tabia, imani au malengo ya zamani, tutakua pamoja au tutatengana?

10. Usalama wa Kihisia - Je, tunaweza kuwa wazi bila hofu?
Mmoja wetu akiwa dhaifu, amechoka au ameshindwa, je, hii ni mahali salama pa kupumzika?
Jitahidi kupata mwanamke ambae yuko tayari kuwa submissive na kufuata dira yako. Mwanaume ndiye mbeba maono na mke ni mshauri/msaidizi.

Tofauti na hivyo utajuta sana na kuchukia ndoa
 
Mwanzo mahaba mnayopeana kila mmoja anamuona mwenzie malaika… gari likianza kuchanja mbuga ndio mnagundua hata matairi ni vipara 😹😹😹
😂😂😂😂😂😂
 
Jitahidi kupata mwanamke ambae yuko tayari kuwa submissive na kufuata dira yako. Mwanaume ndiye mbeba maono na mke ni mshauri/msaidizi.

Tofauti na hivyo utajuta sana na kuchukia ndoa
Hata maono yasiyofaa au ya kiwakii??
😂😂😂😂
 
Uliyaongea yanaweza kufanya kazi zaidi kwa wazungu, kwa sababu wapo honest. Sio hawa dada zetu ambao wanaficha past na character zao wakiwa wanataka ndoa.

Bed to bed midfielder akiwa kwenye mawindo ya ndoa unafikiri anaweza kukwambia idadi ya abortions alizofanya?

Kibongo bongo ukiwa hapo kwenye kipindi cha courtship usijadiliane na mwanamke kuhusu hayo masuala wewe nenda nae tu huku ukiwa unamfanyia udadisi kimya kimya kama anatiki kwenye vigezo vyako vya muhimu.

Na hili kufanikisha kujua zaidi kuhusu past yake, mitazamo yake, fantasy zake n.k jifanye bad boy hata kama sio. Women are more open and honest to bad boys than intentional men.
 
Kinachofanya mkutane, mkulane mpaka kufikia kuoana ni hisia zaidi.

Na hata hayo mkiulizana tegemea mmoja kujibu ndivyo sivyo baadae mje kulikoroga tena.
 
Back
Top Bottom