Malecela and Dr. Salim - Into Oblivion?

Malecela and Dr. Salim - Into Oblivion?

Salim atakumbukwa kwa kuleta mitumba TZ!!!

Hapana,

Atakumbukwa kama mwanasiasa ambaye alikataa kuingia katika utamaduni wa siasa chafu wakati zilipokua zinaota mizizi, atakumbukwa kwa kuwa mmoja wa wanasiasa aliyeonyesha kutokuwa na tamaa ya kukimbilia urais hata kwa gharama yoyote,atakumbukwa kama mmoja wa watu wawili ambao waliaminiwa na baba wa taifa Mwalimu Nyerere kuliongoza taifa letu (mwengine ni marehemu Moringe Sokoine) atakumbukwa kama mmoja wa wanasiasa wachache ambao wametumia nafasi zao kipeperusha vema bendera ya tanzania yet na pia atakumbukwa kama mtu aliyetuamsha watanzania kutambua tatizo la ubaguzi miongoni mwetu katika wakati ambao wengi tulikuwa tunajidanganya kuwa hilo ni tatizo la majirani zetu tu.

Na kuhus mitumba na wanajeshi wetu atakumbukwa kama kiongozi aliyeonyesha kuthamini utu wa watanzania na kutekeleza kwa vitendo.


Tanzanianjema
 
Mzee Tz,

Ninaomba niseme kitu kimoja tukiwa tunaendelea na huu mjadala, kwamba ni muhimu kujua chanzo cha uanasiasa wa wanasiasa wetu, Originally, wanasiasa wetu walikuwa ni makundi mawili, yaani la Kambona na la Mwalimu,

Kambona aliwaingiza kwenye siasa kwa kutumia ubavu wake binafsi, viongozi kama Balozi Lusinde, Dr. Malecela, Dr. Marsha, Kamaliza, Chifu Fundikira, General Nyirenda, Sitta, General Sarakikya, Bibi Titi, Dr. Babu, Balozi Magombe, Kihampa, Kisumo na wengineo..!

Mwalimu aliwaingiza, Kahama, Bomani, Mark Bomani, Jamal, Bryson, Kawawa, Sokoine, Dr. Salim, Tandau, Mwakawago, Msekwa, Warioba, Apiyo, Mama Mongella, Mhaville, Siyovelwa, General musuguri, General Twalipo, General Natepe, Nassoro Moyo, Elinawinga, Dr. Kleruu, Kisokky, Maswanya, Mkapa, na wengineo...!

Sasa swali la msingi hapa ni kwamba je kulikuwa na maelewano mazuri kisiasa, kiitikadi, na kiuongozi kikazi kati ya haya makundi mawili? Je nini matokeo ya kuondoka kwa Kambona kwa wale aliowaingiza, yaani lile kundi lake?
 
Bila kupingana na asili ya uanasiasa wa wanasiasa wetu,as wale wa Kambona na wa Mwalimu,kinachonitatiza ni kwanini Mwalimu "alimvumili"Malecela kwa miaka yote hiyo na wakaja kutibuana baada ya Mwalimu kuondoka madarakani.Je Mwalimu aliogopa kuwatimua wafuasi wa Kambona lkn akapata nguvu ya kuwapinga baada ya kutoka madarakani (referring to his criticism to Malecela)?

Wapo wambeya wanaosema kuwa mtu aliye-cross path na Mwalimu basi huyo angefutika kabisa katika upeo wa siasa...na wale aliowapenda aliwalea hadi anastaafu (na hapo ndipo baadhi ya watu wanamwona kuwa pengine pasipo kukusudia alikuwa akikwaza maendeleo ya nchi kwa kung'ang'ania watu walewale kila kukicha).
 
Mzee Tz,
Ninaomba niseme kitu kimoja tukiwa tunaendelea na huu mjadala, kwamba ni muhimu kujua chanzo cha uanasiasa wa wanasiasa wetu, Originally, wanasiasa wetu walikuwa ni makundi mawili, yaani la Kambona na la Mwalimu,

Kambona aliwaingiza kwenye siasa kwa kutumia ubavu wake binafsi, viongozi kama Balozi Lusinde, Dr. Malecela, Dr. Marsha, Kamaliza, Chifu Fundikira, General Nyirenda, Sitta, General Sarakikya, Bibi Titi, Dr. Babu, Balozi Magombe, Kihampa, Kisumo na wengineo..!


Inaendana na hii,

Tanzania: Mkapa's Brush With Bad Karma
East African (Nairobi)
26 June 2007
Philip Ochieng


During his term in office, the former Tanzanian president led a campaign to 'de-Tanzanianise' publisher Jenerali Ulimwengu, who it was claimed was Malawian. Now there are allegations that Mkapa is in fact a Mozambican. PHILIP OCHIENG', recalling the days when he, Mkapa and Ulimwengu all worked together at the Daily News, draws the moral lessons from this tale

THE ANCIENT TEACHERS HAD A FITTING moral rule for Benjamin Mkapa: Do unto others as you would have them do unto you; or, the other way round: Never do to anybody anything you would not want him to do to you. Both the Buddha and the Christ are reported to have admonished: Never condemn or punish anybody for a "sin" that you yourself commit. It is difficult to see what his detractors hope to achieve - so late in the former president's life - by charging that he is not a "Tanzanian." According to reports reaching me from Dar es Salaam, the charge is getting thicker by the day that he is a "Mozambican."

A surprising number of Tanzanians have fallen into this ethnic Eldama Ravine. When I worked in Dar, in the early 1970s, Tanzania looked like the only African country completely free of tribalism - the virus that has eaten so destructively into Kenya's body politic.But if Ben now finds himself a target of it, it does unfortunately look like a fitting comeuppance. For, not so long ago - during his years at Ikulu (State House) - he reportedly led the way by spearheading a determined campaign to "de-Tanzanianise" a mutual friend, saying that our friend's parents had come from the other side of Lake Tanganyika.

Even at the personal level, I found it most painful, because I once worked very closely with Jenerali Ulimwengu and Benjamin Mkapa under the direction of what is probably the broadest mind I have ever known among the world's practising politicians. I mean Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Ben was our managing editor when I wrote a highly critical column called "The Way I See It" for a government-owned newspaper originally known as The Tanganyika Standard. This Dar es Salaam Standard had been part of a huge East African newspaper conglomerate owned by Roland "Tiny" Rowland's Lonrho.Nairobi's own East African Standard - which had for a long time been a mouthpiece of Kenya's diehard British colonial settlers - was its flagship. Its satellites included The Argus of Kampala, The Times of Zambia, The Mombasa Times and a Nairobi-based Kiswahili periodical called Baraza.

IN 1970, WHEN MWALIMU NATIONALISED The Tanganyika Standard, he renamed it The Standard Tanzania. But, in 1972, it was merged with The Nationalist, which had been the organ of the ruling party Tanu since nationalist times, to give birth to the present Daily News.
Benjamin Mkapa, one of the keenest minds I have ever worked with, was always central to these changes - indeed, to Tanzania's entire information system. He was always to Nyerere's right, to be sure, and never indulged in the "revolutionary" phrase-mongering that went on in Tanzania at that time.

But one thing I must say. Ben's manner was always polished, his mind always remarkably cosmopolitan. His capacity for tolerance was shown by the fact that he allowed all nuances of political thought - from "sixth-lane right-wing" reaction to Trotskyite leftism - to be expressed fully through the newspapers that he edited.
AND, ALTHOUGH BEN WAS firm in the implementation of the editorial policies that Mwalimu had laid down for The Standard when he took it over, I never detected any arrogance of power, and not a single whiff of ethnic or national narrowness, in Ben's leadership.

His amiable personality, and Nyerere's, probably contributed to the disproof of a deeply held Western prejudice - that a newspaper can serve society fully, objectively and with impartiality only if it is independent of all government influences. Clearly, it depends also on what kind of government is in place.
But the upshot is that, thanks to the policy guidelines that Mwalimu issued, The Standard Tanzania for which I worked (successively under Frene Ginwala, Sammy Mdee, Ben Mkapa and Ferdinand Ruhinda) was probably the freest newspaper that I have ever known. Probably Ben's moral and intellectual attributes were inborn. But he must owe much to his formal intellectual upbringing. It is hard to imagine he didn't go to Tabora Boys Government Secondary School, Tanganyika's equivalent of Kenya's Alliance High School and Uganda's King's College, Budo. Most of Tanzania's prominent leaders at that time - including Mwalimu - were Tabora products.

Instead, he went to Ndanda Secondary School and St. Francis College, Pugu. Ben then took a degree in English from Kampala's Makerere - that era's tertiary concentration of East Africa's intellectual elite - where he was a classmate of such potent minds from Kenya as the novelist Ngugi wa Thiong'o, the poet Jonathan Kariara and the literature don Grant Kamenju. On returning from New York City's Columbia University with a master's in English, Ben started life as a speech writer for Oscar Kambona, the party's secretary-general who, at Independence, became the foreign minister, probably the most brilliant of the stars rising in the Haven of Peace.

However, following Azimio - the Arusha Declaration of 1967 - Kambona rebelled against Nyerere over the document's Ujamaa policy, especially the imposition of a stringent code of conduct barring a certain echelon of party and government leaders from private business.

Kambona dashed into exile in London, from where, in the beginning, he gave Nyerere quite a run for his money in terms of propaganda, but where he gradually wasted away into national oblivion. By the time he returned home, in the 1980s, he had lost all steam and died soon afterwards.
BUT, BACK IN THE MID-60S, it was Kambona who arranged for Ben Mkapa to be appointed the editor of The Nationalist, assisted by such able journalists and dedicated wazalendo (patriots) as Costa Kumalija and Ferdinand Ruhinda. It would never at that time have occurred to any Tanzanian to mention the link.
But Kambona and Ben had something in common that may shed light on what is happening to Ben today. If the question of one's tribe had been as paramount in Tanzania's national mind as it remains in Kenya's today, Kambona would have been accused of tribalism.
For both he and Mkapa were said to belong to the Ngoni community. Rashidi Kawawa, the redoubtable colonial-era trade unionist who was later to become even more powerful as prime minister, was also said to be a Ngoni. The thing about that ethnic community is its omnipresence in the southern half of the continent.
In his book A History of the African People, Robert W. July, an American historian, traces the Ngoni all the way to the Zulu of Natal and reports that, today, they are to be found in Botswana, Lesotho, Malawi, Mozambique, Swaziland, Tanganyika (mainland Tanzania), Zambia and Zimbabwe.
Kambona's roots were claimed to be either in Malawi or Mozambique. So were those of Austin Shaba and Michael Kamaliza. The latter was a powerful trade unionist (with close links with Kenya's Tom Mboya). Both were close allies of Kambona in Nyerere's first Cabinet, and both petered out with him.

But that is where the question arises. What does it matter if Ben Mkapa has this South African link? What does it matter that - like the denizens of Mombasa's Kisauni - Kambona's people came from Malawi? What does it matter if Jenerali's great grandparents were Rwandese or Congolese?
In the first place, every last one of Africa's international boundaries is completely artificial. All were drawn up totally arbitrarily by European powers following the partition conference in Berlin in 1885. The Maasai, for instance, were divided into two, half going to Kenya and half to Tanganyika.
THAT IS WHY TWO BROTHERS called Awori may one day become presidents simultaneously, Moody in Kenya and Aggrey in Uganda. Jenerali's family may have been sundered in a similar manner, some going to Belgian Congo, some to Belgian Rwanda, and some to German Tanganyika.

Every African country has that problem and it is the cause of all our secessionist movements, which, if allowed, would - as Kwame Nkrumah pointed during the formation of the Organisation of African Unity in Addis Ababa in 1963 - logically culminate in puny little tribal states.
But, secondly, even before Europe's advent, tribes and races - like human beings all over the world - were moving into and out of Africa, back and forth, all over. That is why the "Hottentots" of South Africa and the Malagasy of Madagascar have such prominent Mongoloid (Indonesian) features.
Indians, Arabs and Shirazis (Iranians) were settling along the East African littoral a millennium and half before my Luo people arrived in Nyanza from the Sudan or the Kikuyu in the Mount Kenya region from Mozambique.
In his remarkable book The Kalenjin People's Egypt Origin Legend Revisited: Was Isis Assis? - sub-titled A Study in Comparative Religion - Kipkoech arap Sambu shows that the Kalenjin arrived in East Africa from Nilotic North Africa. Indeed, we can say that their cousins, the Maasai, are Kenya's only true autochthons.

So neither Mwai Kibaki nor Raila Odinga nor Musalia Mudavadi nor Musikari Kombo nor Uhuru Kenyatta nor William Ruto nor Kalonzo Musyoka nor Ali Mwakwere nor Joe Khamisi can claim that he is "more Kenyan" than Davinder Lamba, Ali Mazrui, Najib Balala and Pheroze Nowrojee or, for that matter, Richard Leakey and even the hapless scion of Lord Delamere.
That is the point. If you pose the question: Who is a Tanganyikan? - the answer has to be: every tribe and race which was covered by the Berlin treaty that created Tanganyika, and everybody else whom the vicissitudes of history brought into that country who satisfies all other legal citizenship requirements.
That is why neither Jakaya Kikwete nor Kingunge Ngombale-Mwiru nor Chief Abdalla Fundikira nor Pius Msekwa nor Mark Bomani nor Bhoke Munanka nor Anna Tibaijuka can claim that he or she is "more Tanzanian" than Salim Ahmed Salim, Zakia Meghji, Timothy Apiyo and Joseph Mungai.

That is why Ben Mkapa should have left Twaha - Jenerali Ulimwengu's given name - well alone. But that is also why Tanzanians should leave Ben Mkapa himself alone. Not only are both fully Tanzanian but also both have served the people of that country in very senior capacities.

Jenerali, who now publishes his own newspaper, was the one to whom I bequeathed my Daily News column when I left Tanzania in 1973. Afterwards, he served Tanu - later rechristened Chama cha Mapinduzi - in various senior capacities, including for many years as its envoy to a continental youth organisation based in Algiers.
When The Nationalist was merged with The Standard Tanzania to create the Daily News, Ben replaced Mdee as its editor. He then served for a number of years as Tanzania's diplomatic envoy first in Ottawa and then in Washington, before being named foreign minister. Benjamin William Mkapa was on his way to Ikulu.
I had occasion to criticise some other aspects of his government, especially corruption and, more recently, Tanzania's un-Nyerere-like surrender to the predatory global power structure. Official Dar es Salaam's reaction to my criticism was remarkable for its cowardice.Instead of replying through the newspaper in which I had written it, Dar simply organised a few Kiswahili rags in Dar to pour uneducated insults on my name. It was not behaviour that Julius Nyerere would have applauded. It was a far cry from Mwalimu's 1967 injunction to us: "Argue, don't shout!"
What had happened to the open and firm but positive, friendly and good-mannered freedom of opinion and criticism which I had enjoyed successively under Frene, Sammy, Ferdinand and, above all, Ben Mkapa himself? What unalloyed fun it was!
COULD IT BE THAT SUCH SENIOR Dar colleagues of mine as Tony Barros, Immanuel Bulugu, Felix Kaiza, Kusai Kamisa, Fili Karashani, Naijuka Kasihwaki, Scholastica Kimaryo, Hadji Konde, Guido Magome, Joseph Mapunda, Khassim Mpenda, Nsubisi Mwakipunda, Ulli Mwambulukutu, Adarsh Nayar, Abdalla Ngororo, Robert Rweyemamu and Pascal Shija were the ones now pouring such bilge water on me?

I don't know. But one thing is certain. When Ben Mkapa was editing an authoritative newspaper, Tanzania was the African nation most conscious of its objective interests and, at the same time, most committed to mankind's liberation, especially Africa's.
When Benjamin William Mkapa was the chief policy custodian of the Indian Ocean city, Tanzania seemed to lose that international leadership role which once made Dar es Salaam the moral and intellectual capital of the world. What happened?




Mjumbe hauwawi!!!!

Tanzanianjema
 
Thanks Ziro,

Mimi sikujuwa kwamba ni bora kuvaa gunia kuliko mtumba!
 
Saidi Maulidi alipovuliwa uraia (alipotangazwa kuwa si raia) alienda mahakamani na haki ikapatikana. Kwa hiyo kama una uhakika wa uraia wako na unaweza kuthibitisha hivyo bila ya walakini wowote, acha watangaze kukuvua uraia nawe utarudishiwa na historia itajiandika once and for all. Kwa maana hata aje nani sidhani kama kuna kizazi cha Saidi Maulidi kitakuwa na matatizo ya uraia. Vinginevyo option inayokuwa imebaki ni kuomba tu uraia huo, kitu ambacho akina Twaha Khalfan (Ulimwengu) walifanya.

Hata kama Mkapa au wewe unayesoma hapa utagundulika siyo raia wa nchi hii, haijalishi umeshika nyadhifa zipi, ni kwamba ulikiuka sheria ukijua kwamba siyo raia wa nchi hii kwa hiyo ni lazima uvuliwe na ukipenda uombe uraia kwa kufuata taratibu. Peru walishawahi kuwa na rais ambaye ni raia wa Japan, lakini hilo halikuzuia yeye kutimuliwa hata baada ya kuwa ameacha urais.
 
Mzee Mlalahoi,

Baada ya Kambona kuondoka, victim wa kwanza walikuwa Dr. Marsha (Baba wa waziri Marsha), Kamaliza, Nyirenda, na Bibi titi, baadaye General Sarakikya.
 
Mbona wanasiasa wengi waliotajwa kwamba walikuwa ni wafwasi au marafiki wa Kambona (Malecela, Lusinde, Mkapa, na wengineo) hawakuhusika na coup attempt iliyoongozwa na Kambona? Except Bibi Titi na Michael Kamaliza.

Na ni kwanini Kambona alitaka kupindua serikali ya Mwalimu na kutegemea kwamba wananchi wengi wangekubaliana naye - knowing full well how popular Mwalimu was, hasa miaka ile?

Nimemaliza kusoma kitabu kuhusu Mwalimu, "Nyerere and Africa: End of an Era," kilichoandikwa na mzalendo mmoja, Godfrey Mwakikagile, na sijaona sababu yoyote - ya kisiasa - katika kitabu hicho kwanini Kambona alitaka kumpindua Mwalimu.

Kitabu hiki kimeeleza vizuri sana siasa nchini Tanzania, na uongozi wa Mwalimu. Ni kiongozi aliyekuwa mtetezi wa wanyonge. Pia alikuwa hana upendeleo. Kuna chapter nzima katika kitabu hicho kuhusu coup attempt ya Kambona na comments za Andrew Nyerere anayefahamiana na mwandishi wa kitabu hicho. One reviewer, amazon.com, amesema kwamba labda Mwakikagile ni rafiki ya kina Nyerere, na ndiyo maana aliandika kitabu hicho kinachompendelea Mwalimu. Bado sijaona na sijasikia evidence yoyote kuonyesha kwamba ni kweli mwandishi huyo alikuwa na uhusiano wowote na Mwalimu na watoto wake - except Andrew, schoolmate wake miaka mingi iliyopita.

Nilipomaliza kusoma kitabu hicho, I had a full understanding of Nyerere's policies, domestically and internationally, na bado sijui kwanini kulikuwa na Watanzania waliotaka kumpindua kiongozi huyo na kutegemea kwamba wananchi would have sided with them - against Mwalimu!

What was Kambona thinking?

Labda mnaweza kunisaidia nielewe zaidi kuhusu jambo hilo.

Na mwandishi huyo, Mwakikagile, yuko wapi? Anafundisha katika nchi za nje? Sijasikia kwamba yuko nyumbani Tanzania.
 
Cheche,
Kuna kitu kinaitwa tamaa ya madaraka. Kambona naye alijiona kuwa presidential material. Mwakikagile nadhani bado yuko US. Nitakutafutia contacts zake.
 
Kama Mobutu aliweza kumeliminate Lumumba then I do not see any problem kwa Nyerere. Although this does not mean that Kambona was capable of doing that. After all nasikia Kambona ndiyo alikuwa mstari wa mbele kuwatuliza wanajeshi walipotaka kuasi. Nyerere mwenyewe aliingia mitini!!!
 
Cheche,Mzee ES,TanzaniaNjema,
Historia ya Tanzania[Tanganyika & Zanzibar] inapotea kwasababu Watanzania hatuna tabia ya kuandika vitabu. Ukiangalia nchi za wenzetu, haswa mataifa yaliyoendelea, karibu kila kiongozi aliyeshiriki ktk jambo lolote la "kihistoria," basi anahakikisha ameliweka ktk maandishi.

Kwanini Mwinyi,Kawawa,Malecela,Warioba,Salim Salim,Msuya,Mtei,Fundikira,Bomani,Kahama,Msekwa,Musuguri,Kiwelu,Kiaro,Ngwilizi....hawaandiki vitabu?

Tatizo lingine tayari kuna "Official storyline" ya mambo yaliyotokea na wapo waandishi wanaojaribu kuirudirudia. Huwezi kupata ukweli kuhusu historia ya siasa za Tanzania kwa kupitia vitabu vilivyoko sasa hivi.

Sote tunafahamu kwamba nchi iliporomoka kiuchumi wakati wa Mwalimu Nyerere. Kitu cha ajabu hakuna anayejitokeza kuelezea makosa yalifanyika wapi na kwasababu gani. Vilevile hakuna anayejitokeza kutueleza kama kulikuwepo viongozi waliopinga maamuzi yaliyofanyika, na kwanini hawakusikilizwa.

Kila kitu ni SIRI,SIRI,SIRI.....majuzi Museveni kapasua jipu kwamba Kaburu alitushambulia Dar, na makaburu wameweka kumbukumbu hiyo ktk Kitabu "the silent war."
 
Mzee ES,
Mbona Sarakikya alijiunga na jeshi kabla hata ya Uhuru? Ila uvumi ulioenea ni kwamba na yeye alitaka kumpindua Mwalimu. Inasemekana kwamba hiyo ndiyo sababu akaondolewa Jeshini.

Vilevile kuna kipindi askari wasomi waliotokea mikoa ya kaskazini waliondolewa jeshini na kupachikwa kazi uraiani. inasemekana serikali ilikuwa haina imani nao.

Mr.Zero,
Madai yako ni ya kweli. Kambona ndiye aliyekuwa akiwatuliza wale Askari na kujaribu kusikiliza matatizo yao. Habari iko well documented kwenye kitabu cha Maasi ya 1964.
 
Kambona na Mwalimu, ninaamini walianza kutokubaliana kuhusu muelekeo wa nchi yetu kisiasa na kiuchumi, na pia Mwalimu alianza kumtumia Kawawa kwa ajili ya kumtia nyongo Kambona, hatimaye Kambona akaamua kutimua,

(1). Baada ya Kambona kuondoka, victim wa kwanza alikuwa Dr. Marsha, aliyekuwa katibu mwenenzi wa kwanza wa TANU, alifukuzwa TANU na kupigwa marufuku kuajiriwa na muajiri yoyote bongo, mpaka kibali kitoke kwa Butiku, kila alipojaribu kibali hakikutoka, akapeleka kesi yake UN, wakamchukua na kumsomesha zaidi na kumpa kazi kama Director wa Information kwa angalau 30 years, hadi sasa ni mbunge wa EAC!

(2). Next on line alikuwa General Nyirenda, aliyedaiwa kuhusika na coup, alihamia in exile Zambia, mara ya mwisho nilimuona Lusaka mwaka 1980 kwenye uwanja mmoja wa tenis pale Katima Muliro Road, kwenye viwanja vya bunge la nchi hiyo, nilipoomuuliza kulikoni, alisema kuwa Mwalimu hamtaki bongo, kwa hiyo alimuombea aishi huko!

(3). Bibi Titi na Kamaliza, walihusika na njama za mapinduzi, Mwalimu aliwasamehe kwenda jela, lakini ikawa ndio mwisho wao katika siasa!

(4). Sarakikya, became too powerful na popular huko jeshini, alihamishiwa wizara ya utamaduni, baadaye ubalozi Lagos, Adis, na Nairobi, kwenye uchaguzi uliopita alimwabia Muuungwana in his face kuwa haitakuja kutokea yeye kuwa rais wetu! Sasa hivi ni majority share wa Azania Bank!, siasa kaputi!

(5). Lusinde, alihamishiwa China, baadaye Nairobi, mchezo ukaisha!

(6). Malecela, alifichwa kwenye EAC, baadaye akapewa second chance ya kuwa foreign minister, akajaribu kuwa independent minister kwa kufanya maamuzi mengi on his own, kwa mfano aliposuluhisha vita kati ya Somalia na Idd Amin, hakufuata kabisa maagizo ya Mwalimu, na pia kwenye suluhisho la kwanza la amani kati yetu na Uganda, pia alienda huko na kuamua maamuzi yake mwenyewe, ingawa yalikuwa ni kwa manufaa ya taifa, lakini hayakuwa maagizo ya Mwalimu, na kwa mara ya kwanza Mwalimu akagundua kuwa alianza kuwa na ambitions za urais, akatupwa kilimo, mawasialiano, na Madini, kabla ya kukoseshwa ubunge kabisaa wakati Mwalimu akiwa ana-retire, the plan ilikuwa asirudi tena kwenye siasa,

Mwinyi, akamrudisha as an-act of rebellious against Mwalimu, tena kwa kumtoa Warioba, baada ya hapo Mkapa, Warioba, Apiyo, Butiku na the likes, wakaanza kupishana kwa zamu kwenda Butiama, kumlalamikia Mwalimu, kuhusu Malecela, Mwinyi, na Diria.

......Itaendelea.....
 
Cheche,Mzee ES,TanzaniaNjema,
Historia ya Tanzania[Tanganyika & Zanzibar] inapotea kwasababu

Kwanini Mwinyi,Kawawa,Malecela,Warioba,Salim Salim,Msuya,Mtei,Fundikira,Bomani,Kahama,Msekwa,Musuguri,Kiwelu,Kiaro,Ngwilizi....hawaandiki vitabu?

kati ya hawa uliowataja wapo wanaoandika na wapo ambao ilikuwa waanze kuandika lakini hivi sasa majukumu yamewazidi. Hata hivyo ni kweli hili ni tatizo kubwa mno. wengi wanadai watawaharibia wenzao lakini nadhani ukweli ni kuwa hatuna utamaduni wa aina hii. hata hivyo nadhani ni jukumu la vijana haswa wale wasomi kuwapush hawa wazee wakubali na wao kuwasaidia. Mzee Jumbe ameeandika vitabu na anasubiri mungu amchukue vitoke. Kazi hii aliifanya akisaidwa na mwanawe mmoja. Sasa kwa kuwa na hapa tuna watoto wa wenye historia ya nchi ni changamoto kwao pia kuwabana washua waandike wakati kina sisi ambao majina yetu ya mwisho hayana uzito katika historia tujitahidi kuwabana hawa wazee hata kuwa wasaidizi wao katika kukusanya data. Changamoto hii ni kwetu sote.

Naamini wakitokea wasomi vijana wakatengeneza project ya kuandika vitabu vya hawa wazee wetu angalao kitabu kimoja kila mwaka tutaweza hata kupata funds za kufanikisha hili.

Mimi binafsi tayari nimewatega wangu wa kuwang'ang'ania. Ni masuala ya kuweka sawa mipango. Hatuwezi tukaacha hawa wazee wetu waondoke na historia ya nchi yetu na kutuacha sisi tukitegemea longolongo la mitaani kushape nchi yetu.

kuna kijana mmoja wa kimarekani tayari ameshandika historia ya Seif Sharif,Sultan Issa na wengine. Natumai soon watapublish. Wapo wengine wanawork on getting Mzee Kawawa. I hope mambo yataenda vizuri..

Tanzanianjema
 
Mzee TZnjema,

Maneno yako ni mazito sana, binafsi I am working na at least viongozi kama sita ambao bado wako hai, na niliwahi kufanya hiyo shughuli na viongozi kama watano ambao hawapo tena duniani, when the time is right kutokana na conditions walizizozitoa na wanazozitoa, vitabu vitapatikana,

Lakini vyema wananchi wakafuata mawaidha yako, itakuwa ni plus kwa vizazi vijavyo na hasa watoto wetu!
 
tatizo watz hatuna akili za upeo tumekuwa kama watoto wadogo leo ni miaka mingapi imepita hakuna maendeleo yoyote eti mtu akiacha madaraka ndio tunajitia kusema hakufanya jambo lolote la maendelea lakini akiwa bado yopo tunasema ndio mzee kama si wewe hutunge[pata maendeleo kila siku watu ndio walewale hawataki kuondoka utadhani tz ni mali yao
 
Mzee tonga,

Kama maneno yako ni kweli, basi tusingekuwa na hii forum, hebu ninakuomba upitie thread zote za hii forum, halafu uionyeshe topic inayosema "ndio mzee kama si wewe tusingepata maendeleo", angalau nitolee one topic inayofanana na maneno yako ya kututukana wa-Tanzania wote, na hasa wa hii forum!


Quote[I].."Kila siku watu ni wale wale hawataki kuondoka utadhania TZ ni mali yao...",[/I]


ebo sasa Tanzania ni mali ya nani kama sio wananchi wa-Tanzania? Kati ya viongozi wetu wa CCM na upinzani kuna mnyasa au banyamulenge? Hebu mtaje kiongozi mmoja wa siasa bongo ambaye hakuchaguliwa na wananchi kwa njia ya ki-demokrasia, yaani kwa kupigiwa kura anayenga'ng'ania madaraka?

Mzee hakuna m-Tanzania anayekatazwa kugombea uongozi, awe kijana au mzee, hatuna sheria inayo-limit wananchi kutogombea wakifikia umri fulani, je unaweza kuwaita wa-Israeli waliomchagua rais mpya Bwana Peres majuzi mwenye umri wa miaka 83, kuwa rais for the next 7 years, kuwa ni wajinga kisiasa kuliko sisi bongo?

Quote: [I]"tatizo wa-TZ hatuna akili za upeo tumekuwa kama watoto wadogo" [/I]

Hapana labda wewe peke yako katika hii forum, ndio una-fit hiyo conclusion, ya kutokuwa na akili za upeo, maana forum hot kama hii ambayo sasa inasomwa na karibu viongozi wote Tanzania, na mpaka Waziri mkuu kuona umuhimu wa kuja hapa na kujibu hoja ya mwana-forum, Mzee MMJ, wewe unasema eti hapa watu hawana akili za upeo, what a life loser are you bro? Kama huna akili za upeo ni wewe peke yako bro, hizo lugha za choooni hazina nafasi hapa mkuu, next time ongelea jinsi wewe binafsi ulivyo na upeo mdogo wa mpaka kuweza kuandika hiyo post yako hapo juu, badala ya kuwazungumzia wana-forum hapa, kwa sababu hii sio forum ya watz wasiokuwa na akili za upeo kama zako peke yako!

Kama huzitaki mbichi hizi kaaa pembeni, upewe elimu ya bure hapa! Tanzania ni mali yetu wote, ila kila mtu na ubavu wake, na hakuna nchi yoyote duniani ambayo wananchi wake walikuwa hawataki maendeleo lakini wakaletewa maendeleo hayo na viongozi wao anyways?

Pia nenda usome vitabu ili ujifunze kuwa maendeleo ya nchi huletwa na wananchi sio viongozi, ili next time usituletee this kind of pumba hapa forum bro, hizi tulishazipita long time ago kule BCS!!
 
Mzee ES,
Mimi nina matatizo na huyu Mzee wetu John Malecela, na haswa alipokuwa Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Raisi.

Mimi nadhani Malecela alishindwa kumrudisha Mwinyi katika mstari. Mwinyi alikuwa kama vile yuko pale kutetea maslahi ya Wazanzibari at the expense ya Watanzania Bara.

Kwa upande wangu nadhani Makamu wa Raisi John Malecela angekuwa strong basi Mwinyi asingekuwa na ujasiri wa kufanya alivyokuwa akitaka.

Naamini hoja ya wabunge 55 kuhusu kuanzishwa kwa Tanganyika, ilitokana na hasira ya wabunge kuhusu mwenendo wa serikali ya Mwinyi, ambayo Malecela alikuwa Makamu wa Raisi.

Kuna mambo mengine kama kutokukusanya kodi. Yaani mwaka 1995 walikuwa wanakusanya bill 25, mwaka 2005 walifikia karibu bill 250. Hiyo mimi nadhani ilikuwa hujuma ya waziwazi. Sasa Malecela alikuwa wapi, na akifanya nini.

Kulizagaa uvumi kwamba serikali ya Mwinyi ilikuwa "ikiwayeyusha" JWTZ kuhusu madai yao ya nyongeza ya mafao. Uvumi ulienea kwamba wanajeshi walikuwa wanakosa subira na wako tayari kufanya "kitu mbaya." Sasa huo si ulikuwa uzembe wa hali ya juu. Kiranja Mkuu wa Mawaziri na Msimamizi wa shughuli za serikali, John Malecela alikuwa akifanya nini haswa?

Nia yangu hapa si kumchafua Mzee Malecela ila nahitaji kumfahamu vizuri. Nimeongea na watu wanaomjua Mzee Malecela nje ya kazi na wanamsema vizuri kuwa ni mtu mkarimu sana. Hata alipoondolewa Uwaziri Mkuu nasikia wako wabunge waliotokwa na machozi!!

Kwa kweli kama itatokea kikaandikwa kitabu kuhusu Cygwiyemwisi John Samuel Malecela basi ni lazima kifafanue maswala niliyouliza.
 
"Mzee ES,
Mimi nina matatizo na huyu Mzee wetu John Malecela, na haswa alipokuwa Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Raisi.

Mimi nadhani Malecela alishindwa kumrudisha Mwinyi katika mstari. Mwinyi alikuwa kama vile yuko pale kutetea maslahi ya Wazanzibari at the expense ya Watanzania Bara.

Kwa upande wangu nadhani Makamu wa Raisi John Malecela angekuwa strong basi Mwinyi asingekuwa na ujasiri wa kufanya alivyokuwa akitaka."


Mzee wangu Joka Kuu, katika siasa za kisasa huwa tunahukumu charges za kisiasa against wanasiasa, kwa kutumia mifano iliyofanyka kabla hawajaingia madarakani,

Je wakati wa utawala wa awamu ya kwanza iliyodumu kwa miaka 24, je kati ta Mwaziri wakuu wa awamu hiyo wafuatao Kawawa, Marehemu Sokoine, DR. Salim, Msuya, na makamu wa rais kama Kawawa, Jumbe, Mwinyi, na Idrisa, ni nani kati yao aliyewahi kumuweka Mwalimu katika mstari unaotakiwa?

Je Muungwana sasa hivi yupo pale kutetea masilahi ya wa-Bara tu? Sasa wa-Zanzibari wafanye nini ili kubalance na kauli yako hiyo kuwa Mwinyi aliyewekwa na Mwalimu, alikuwa pale kwa manufaaa ya wa-Zanzibari?

Ni makamu gani unayemfahamu toka tupate uhuru, kuanzia na Kawawa, Jumbe, Idrisa, Mwinyi, na Warioba, ambaye alikuwa "strong" as of your definition, ambaye alipaswa kuwa mfano wa kuigwa na Malecela?
 
Back
Top Bottom