Malecela and Dr. Salim - Into Oblivion?

Malecela and Dr. Salim - Into Oblivion?

Fala sio tusi. Kama unabisha tafuta kamusi ya kiswahili toleo lolote lile uangalie maana yake.
 
Acha kubandika uchafu wako hapa. Hivi una mtindio wa ubongo ama...?


Je kui-categorize hoja ya mwanabodi mwingine kama uchafu na kumkebehi kwa kumuuliza kama ana mtindio wa ubongo ni uungwana ? Hivi kwa nini tunashindwa kupingana kwa hoja mpaka tukimbilie kwenye kuchafuana majina ?
 
Busara inasema kama kungekuwa na nia njema tungewajadili mawaziri wakuu wote; vinginevyo ni chuki na umafia.

Anayetaka kujuwa Salim atakumbukwa kwa lipi akawaulize watu wa mtwara aliowapelekea nguo wakati wakivaa magunia enzi za utawala wa mwalimu!

Ukweli wa mambo ni kwamba kuna genge la watu ambao wanataka kutupangia na kutuamulia nani anafaa na nani hafai.

JM (na Salim) ana matatizo yake kama kiongozi wa juu wa CCM na serikili. Kubwa linalotajwa kuhusu JM ni kuharibu chaguzi ndogo lakini wapo waliofanya mazito kuliko yeye katika chaguzi na hatutaki kabisa kuwazungumzia kwa uwazi stahiki hapa JF.

Hebu mnaowauliza hao wazee tuambieni ni nani aliyebadilisha matokeo ya uchaguzi mkuu kule Zanzibar mwaka 1995 na (mwengine) aliyeharibu uchaguzi mwaka 2000 na 2005. JM yumo katika hao?

Mtu ambaye akiwa Rais wa nchi wameuawa raia wake zaidi ya 20 na akadiriki kutamka "only nineteen" as if raia 19 sio kitu chochote, wakafukiwa watanzania ili kuwapisha wageni wapore madini yetu. Kiongozi kama huyu ndio mabingwa wa takwimu walio jaa JF wanataka tumkumbuke kama hero!

Watanzania tunajuwa mengi na chanzo cha chuki kwa JM. JM hakuwa chaguo la Mwalimu na kuteuliwa kwake kuwa PM na kuondolewa Warioba lilikuwa pigo la pili kwa Mwalimu baada ya kuwa alishaondolewa Timoth Apio (katibu mkuu ofisi ya Rais) kwani ilikata kabisa mawasiliano kati ya Ikulu na Mwalimu.

Sijui kama tunakumbuka matusi ya Mwalimu kwa utawala wa Mwinyi yalianza lini. Na kumbukumbu zangu zinanionyesha kuwa matusi kwa JM yalianzia kwake.

Mtanisamehe kama nitakuwa nimegusa wasio paswa kuguswa hapa JF lakini kama tuna ujasiri wa kuwajadili hao wazee wawili basi tusihofu pia yakitajwa majina mengine.
 
Nyani,

Ninaheshimu michango yangu mingi kwani inajaa nguvu ya hoja lakini contribution yako hapo naona kama ni hoja ya manguvu.

Mwache Mzee ES aandike anachotaka na tuchambue hoja zake.

Mimi naamini jambo moja, kama nina interest au chuki ya aina fulani kwenye jambo, basi ninajizuia sana ili nisichangie. Hoja
ambayo inaendana na jazba au conflict of interest haiwezi kusimama imara hata ikisimikwa kwa zege.

Ni vizuri tukiendelea kuheshimiana maana sisi ni binadamu na tutaendelea kupigana vikumbo sehemu mbalimbali tukihangaikia maisha.
 
Nyie mbona mnakuwa wageni na Nyani!!! Hamkumbuki enzi za BT alivyopambana na gabachori mpaka forum ikawa hacked!! Mnapoteza nguvu zenu. USHAURI WA BURE!!!
 
Nyani Ngabu, Mzee wa Mwanza, mzee wa inueni moyo....

Unataka tuanze malumbano kama BCS au unajaribu kuongeza posts zako humu?!!! OK mimi sijasomea popote kutazama shilingi pande zote, ila ninawasikiliza watu mbali mbali kabla ya kufanya maamuzi. Hata "mafala" pia ninawasoma na kuwasikiliza, na hata "WAJANJA" kama wewe pia ninawasikiliza na kuwajibu hata kama wameandika "VIZURI" sana kama unavyoandika wewe.

FD
 
Guys punguzeni munkari.. changieni hoja bila kutukanana!
 
FIKIRADUNI,
Sasa kwa nini unakuwa subliminal...kwa nini ume-capitalize "WAJANJA" na "VIZURI"? Unanifanya mi mjinga nisiyeweza kung'amua subliminals?

Kwanza mimi sitokei Mwanza kwa hiyo usianze jujifanya unanijua.
 
Ahahahaaa, sikufahamu. No problem. najua u mwerevu.

Msg delivered....

FD
 
Well.. Malecela atakumbukwa kama Mzee ES anavyosema? Na je Salim historia itamkumbuka kwa aliyoyafanya katika Umoja wa Mataifa?
 
MMKJJ,

Kuhusu Salim, angalia post No 127 Ukurasa wa 13 paragraph ya pili.
 
Back
Top Bottom