Tz mbongo
JF-Expert Member
- Mar 12, 2015
- 15,096
- 8,902
Hebu tutumie akili kidogo kupima huo mtazamo wako.hakuna uongo hapo! hakuna ulicho kitunga vyote vimeandikwa kwenye vitabu vya dini.
watu wanahofu kutokana na jinsi dini zao zinavyowaaminisha.Lakini kiuharisia haya mambo ya dini probability kama ni ya kweli ni ndogo sana.
bado siwalaumu waanzisha dini waliona mbali sana walijua hiyo ndio njia ya kuleta amani na ustaarabu ktk jamii .
Mimi na wewe tunajukumu la kusupport dini kuendelea ili jamii isiwe na maovu.Binafsi najiita na dini fulani hata wanangu nitawaambia hivyo ingawaje akilini mwangu najua mimi ni mpagani nafanya yote hyo ili kutaka kujenga maadili mema kwa familia na jamii,ila mambo ya moto,pepo,shetani nk ni hamasa na vitisho ili watu wakae kwenye mstari, binadamu wengine hawana kabisa selfdispline hawawezi kujiongoza wenyewe.
Kuna dini ambazo zina adhabu zake kwa makosa mbalimbali kama vile kuuwa,kuiba,kuzini na mengine mengi tu. Hayo yote yanafanyika hapa hapa na si kwamba ukiiba unaachiwa kwa kutishwa kwa kuwa kuna moto kwa Mungu,sasa wewe unaposema watu wametunga tu hayo mambo ya moto ili kuwatisha watu kufanya maovu,labda ungeeleza ni maovu yapi hayo?