Hayo yote ndugu yangu, uliyoyaeleza yanathibitisha Mungu yupo, kujua au kutokujua chanzo cha ulimwengu SI picha itakayo kanusha uwepo wa Mungu bili itazidi kuimarisha dhana ya uwepo wake kwa sababu ni YeYe Mungu aliyetuzawadia nyenzo ya kutufikisha hapo, nyenzo yenyewe ni AKILI.
Umezungumzia juu ya maendeleo ya tiba, hapo napo inabidi tuzidi kumshukuru Mungu kwa kutujaalia AKILI iliyotuwezesha kufika hapo pia kuna tafiti zinafanyika kwa ajili ya kutumia viungo vya nguruwe kama macho,moyo,ini nk kama viungo mbadala vya binadamu, shukrani kwa Mungu aliyetuzawadia AKILI.
Umezungumzia juu binadamu kupambana na magonjwa anayo yaleta Mungu kuondoa uhai wetu, ungalijua falsafa ya kwa nini "SISI TUPO HAPA DUNIANI' wala usinge uliza kwanini tufe!!, wewe ulitaka uishi milele hapa duniani??! hapa duniani tupo njiani tu na makazi yetu ya milele ni akhera kwa hiyo lazima tufe na kabla yetu walishakufa watu wengi na sisi tutafuata, ila namna gani mtu anakufa ndiyo suala la kujadili:- kuna vfo kutokana na uzembe na ujinga wa binadamu, kuna vifo vya kawaida "natural death" na kuna vifo kama adhabu na mitihani kutoka kwa Mungu.
Unasema "nifikirie hali sasa sipo, nafikiri ni kipi hasa kipo katika hali ya kutokuwepo hakuna kilichopo"

Hapo ni "total illogical statement", kwa sababu unataka kusema wakati wewe hujazaliwa (hujakuwepo) hakukuwa na chochote??!!


, hata wazazi wako, babu, mabibi, wajomba, baba na mama yako na dunia haikuwepo??!!


.
Unasema eti "hakutakuwepo na kitu hadi siku utakapokuwepo",

Nakuomba kaa tena kitako na utafakari hiyo statement yako.




.