Oltung'anyi
JF-Expert Member
- Nov 23, 2010
- 284
- 197
Naam. Muweza wa yote mwenye contradictions ambazo ukijipa muda wa kumtafakari unakuta ni hadithi za kusadikika. Mungu muweza wa yote ambaye ni "function" ya watu, vitu na hali. Yani, watu, vitu na hali ndivyo vinavyom-define Mungu. Halafu tuseme ndiye muweza wa vyote.Mjadala wa Mungu (mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote) unaisha pale ninapoomba contradiction ya kuwepo kwa Mungu huyu ya "problem of evil" inapokosa majibu.
Kama hi contradiction haijaweza kujibiwa, Mungu huyu atakuwa ni hadithi tu.
Ni sawa na mtu akwambie kwamba katika Euclidean geometry kuna pembetatu ambayo hapo hapo ni duara.
Halafu umuulize mtu huyo, sasa pembetatu ina nyuzi 180, na duara lina nyuzi 360, hilo pembetatu duara lina nyuzi ngapi? 180? 360? au ngapi?
Pembetatu ikiwa pembetatu mbona tayari haiwezikuwa duara?
Duara likishakuwa duara mbona tayari haliwezi kuwa pembetatu?
Halafu mtu anashindwa kukujibu.
Anakwambia pembetatu duara lipo tu.
Halipimiki, halionekani, halichoreki, lipo tu.
Halafu anataka ukubali lipo.
Yani ni kama hakuna watu, hali na vitu, kumwelezea Mungu inakuwa kazi ngumu kama kuelezea f ( ) ina maana gani haswa. Anayefahamu relations/ functions lazima akuulize hapa variables ni zipi. Vinginevyo, ni vigumu sana kuelewa f( ) inamaanisha nini. Same applies to God.