Akijaribu yatamkuta yaliyomkuta Kihiyo.Kwa nini mkuu?
Huyo hawezi kugombea ubunge, labda kama hana akili kabisa ndiyo anaweza kufanya hivyo. Kuna mtu dizaini ya bashite miaka ya nyuma akiitwa Kihiyo aligombea Temeke, waulize waliokuwepo kilichompata.
Hoja za kuokotaokota Kama hizi itachukuwa miaka kujikomboa kifikira .Hata alipofika madhabahuni alishindwa kui acknowledge itifaki na kumsalimia Waziri Mkuu
Hivi tunawezaje kuviacha vichwa vyenye akili kama Membe, Lissu, Zitto, January na wengineo na kumruhusu Bashite kuwa mtukufu?
Unamaana Magufuli na Bashite akili zao ni sawa?mbona waliachwa wakina malecela kuwa rais waliachwa wakina mwandosya na wengine mashuhuri akawa rais makufuli
Le mutuz anaingiaje hapa? au unataka wewe ndio ungekuwa le mutuz?
Mbeleko hii labda ipotee na mwenye mbeleko bila hivyo mtasubiri sana. Bashite ni untouchable .
Huyu ataendelea kuwa RC wa Dar na ninasikia ana mpango wa kugombea jimbo la Kawe. Akiwa mbunge anaweza kuwa waziri wa mambo ya ndani.



Huyu ataendelea kuwa RC wa Dar na ninasikia ana mpango wa kugombea jimbo la Kawe. Akiwa mbunge anaweza kuwa waziri wa mambo ya ndani.
Wanazuga wote HawaKwa mwenendo wa Makonda pale Kanisani hata Musiba ameshindwa kumtetea.
Mtakumbuka Makonda alikataa kuwaomba radhi Clouds kwa kitendo chake cha kuwavamia.
Hata pale Kanisani ukisikiliza kwa makini utaona kwamba Makonda aligoma hakuomba radhi kwa kauli za kibaguzi alizotoa.
Musiba ameshangazwa na jinsi Makonda alivyokosa unyenyekevu akiwa madhabahudi, huku akishuhudiwa na Waziri Mkuu, Katibu Mkuu wa chama, na viongozi wengine wa kidini na kijamii.
Ndiye anayetumia jina lisilo lake. Ndiye anayetumia cheti cha masomo kisicho chake.Huyu kijana mwenzetu kabebewa mbeleko la aina yake. Makosa anayoyafanya hadharani bila kukemewa, kuonywa na kuadabishwa Kama wanavyofanyiwa viongozi wengine kwake ni ndoto kwenye awamu hii hii inayosifiwa kwa kutenda haki. Makonda amefanya mengi ya kuudhi na kuvunja sheria.
Ni Makonda aliyevamia clouds, ni Makonda aliyetukana bunge, ni Makonda aliyetuhumu watu hadharani kwa dawa za kulevya na kuharibia watu haiba zao, ni Makonda anayebaguwa wachaga.
Hata hivyo ni muda mrefu watu wamesema hakuna hatua yoyote anayochukuliwa zaidi ya kupongezwa na kukingiwa kifua. Makonda huyu habadiliki na anarudia makosa Yale Yale.
Sasa anasemwa hadharani na katibu mkuu wake wa chama, na makanisani. Anasemwa na Kila kundi la jamii. Si wapinzani, si chama tawala, si maaskofu, si wanahabari, si wanajamii peke yao lkn anasemwa na Kila kundi.
Hilo taulo la kumbeba Makonda limechoka, limetoboka. Sasa ni wakati kumbadilishia mbeleko. Wakati ni Sasa kabla hajaendelea kulitia hasara taifa.
Hilo ni sahihi kabisa na ndiyo maana ' hatumbuliwi ' hapo kwa sasa kwani kama ' akitumbuliwa ' basi itaweza ' Kuathiri ' sana harakati zake za Kisiasa na akaukosa. Hata hivyo wana CCM wa Kawe huyo siyo chaguo lao na wengi wanamtaka Adamjee kwani amelifanyia makubwa hilo Jimbo miaka ya nyuma alipokuwa Mbunge Wao. Hata mwakani Jimbo la Kawe Moto utawaka!
Naibu raisMtoto Pendwa Yupo Kaskazini Anakagua Miradi ya Maendeleo, Sasa Jiulize Anakagua kama nani..
Halafu mkuu wakati anaizumgumzia hii ishu (nadhani akiwa Chattle) alikuwa anaongea kwa upoleee. Mwanzo nikadhani ndo ishu ingemuondoa Bash boy. Maana ilikuwa na kila dalili za uhalifu, na mkuu alisema hilo. Lakini wapi! Sijui mpaka aje afanye kituko gani ndo mkuu yamfike shingoni?Nilishangaa kuona anashindana na Waziri wa Fedha kulipia furniture alizoagiza hataki kulipa kodi? Hadi Mh Rais akaingilia kati, nilishangaa sana
Mbona kama wajitoa fahamu mkuu?Tunapambana na viashiria vya kibaguzi lkn thread na comments zote ni za kibaguzi dhidi ya Gambosh siwaelewi Watu wa humu JF??