Makonda is almost so damn right!

Makonda is almost so damn right!

Status
Not open for further replies.
Makonda ana kiburi cha uzima.
Yeye anaamini Magogoni ndio Mbinguni.
Kwa kazi aliyokabidhiwa Makonda na familia ya Magufuli (Namaanisha kazi ya kifamilia) si rahisi Magufuli kchukulia hatua. Labda kazi hiyo akabidhiwe mwingine na ndo utakuwa mwisho wa Makonda iwapo Magufuli hatajali kuvujishwa kwa siri za familia.
 
Linalosemwa na wengi linasemwa na Mungu.
Makonda jishushe uwe kama binadamu wenzako.
Utambue kuwa Piere Liquidi ni Kiumbe wa Mungu kama wewe.
Na kunawakati wewe ulikuwa kama huyo Liquidi.
Unafikia mahali unamwita binadamu mwenzako mtu wa hovyo hovyo.
Unajua kwanini Mungu alimwumba Liquidi ?
Makonda unadharau iliyopitiliza sana.
Bado una muda wa kujirekebisha, fanya hivyo.
Ukibadilika watu watakupenda tena.
Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu.
 
Huyu kijana mwenzetu kabebewa mbeleko la aina yake. Makosa anayoyafanya hadharani bila kukemewa, kuonywa na kuadabishwa Kama wanavyofanyiwa viongozi wengine kwake ni ndoto kwenye awamu hii hii inayosifiwa kwa kutenda haki. Makonda amefanya mengi ya kuudhi na kuvunja sheria.

Ni Makonda aliyevamia clouds, ni Makonda aliyetukana bunge, ni Makonda aliyetuhumu watu hadharani kwa dawa za kulevya na kuharibia watu haiba zao, ni Makonda anayebaguwa wachaga.

Hata hivyo ni muda mrefu watu wamesema hakuna hatua yoyote anayochukuliwa zaidi ya kupongezwa na kukingiwa kifua. Makonda huyu habadiliki na anarudia makosa Yale Yale.

Sasa anasemwa hadharani na katibu mkuu wake wa chama, na makanisani. Anasemwa na Kila kundi la jamii. Si wapinzani, si chama tawala, si maaskofu, si wanahabari, si wanajamii peke yao lkn anasemwa na Kila kundi.

Hilo taulo la kumbeba Makonda limechoka, limetoboka. Sasa ni wakati kumbadilishia mbeleko. Wakati ni Sasa kabla hajaendelea kulitia hasara taifa.
 
Huyu ataendelea kuwa RC wa Dar na ninasikia ana mpango wa kugombea jimbo la Kawe. Akiwa mbunge anaweza kuwa waziri wa mambo ya ndani.

Wala huyu asikutishe katu. Tumewaona wengi tuu dunia ya Tanzania. Umesahau wakina Ridhiwani walikuwa wanaitwa THE Prince? Umesahau akina Nape etc..walipokuwa kwenye peak? Where are they now?

CHA KUTAMBUA NI KWAMBA KILA KITU KINA MAJIRA! Kuna wakati wa Mvua. Kuna wakati wa Jua.

Let Bashite enjoy his fame at the moment. Mda ukifika atarudi alipokuwa. Hao akina Le Mutuz si kwamba wana urafiki na Bashite. Wao wanataka access na wenye madaraka with associated benefits. Mengine ni ubatili na unafiki.
 
Mkulu namuonea huruma tu.
Ikija kwa huyu na wengine wasiomsikiliza wanampatia picha mbaya wakijua hawezi kuwatenda chochote. Ni kama hajali kuna Raisi nchini naye ndio amembeba na hamtishitishi. Shame

Watendaji wake wengi ni aibu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom