Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,838
- 50,543
Kuna nyakati huwa sielewi ni kwa nini Kuna mfanano wa karibu sana Kati ya ambayo hutokea kwenye siasa za Tanzania na Marekani.
Tarehe 18/05/2009 Jakaya Mrisho kikwete akiwa Rais wa Tanzania, alikuwa ndiye kiongozi wa kwanza kutoka Afrika kukutana na Obama tangu alipochaguliwa mwaka 2008. Ilishangaza kweli kweli.
Kabla ya kukutana na Kikwete Obama alikutana na viongozi toka mataifa yale tu yenye manufaa na maslahi makubwa kwa Marekani.
Leo Marekani inaongozwa na Donald Trump mmarekani ambaye anavunja kila tamaduni ya kiuongozi iliyowekwa kwenye nchi hiyo.
Trump hajawahi kuwa na historia yoyote ile ya kimaadili wala kiungozi... Lakini wamarekani wamemchagua mara mbili.
CCM kwa sasa imepwaya Sana kihaiba na watu wenye sifa za kimaadili mbele ya jamii hawapo. Huwezi pata mtu ndani ya CCM anayeaminiwa na watanzania kwamba ana maadili yanayofaa kuwa kiongozi.
Lakini kama ilivyokuwa kwa Republicans wa Marekani kuwa na Trump, CCM nao wanaye Paul Makonda.
Watu wengi wasioyaangalia mambo kwa kina hawaoni jinsi Makonda anavyoichora ramani yake ya kufanya CCM isiwe na mbadala mwingine ndani ya chama hicho zaidi yake.
Pamoja na shutuma zote anazoelekezewa Makonda, bado yeye kila wakati anaonekana kama nyota ing'aayo ndani ya CCM.
Mzee njaa a.k.a Pascal Mayalla alishawahi kuandika bandiko lake kuhusu Makonda, ukilisoma ukiwa umemakinika, utaelewa ninachosema.
Hofu yangu tusiporekebisha mifumo yetu ya kiuchaguzi, iko siku Makonda atakuwa Rais wa nchi yetu. Na siku hiyo ikifika... OLE WETU!
Tarehe 18/05/2009 Jakaya Mrisho kikwete akiwa Rais wa Tanzania, alikuwa ndiye kiongozi wa kwanza kutoka Afrika kukutana na Obama tangu alipochaguliwa mwaka 2008. Ilishangaza kweli kweli.
Kabla ya kukutana na Kikwete Obama alikutana na viongozi toka mataifa yale tu yenye manufaa na maslahi makubwa kwa Marekani.
Leo Marekani inaongozwa na Donald Trump mmarekani ambaye anavunja kila tamaduni ya kiuongozi iliyowekwa kwenye nchi hiyo.
Trump hajawahi kuwa na historia yoyote ile ya kimaadili wala kiungozi... Lakini wamarekani wamemchagua mara mbili.
CCM kwa sasa imepwaya Sana kihaiba na watu wenye sifa za kimaadili mbele ya jamii hawapo. Huwezi pata mtu ndani ya CCM anayeaminiwa na watanzania kwamba ana maadili yanayofaa kuwa kiongozi.
Lakini kama ilivyokuwa kwa Republicans wa Marekani kuwa na Trump, CCM nao wanaye Paul Makonda.
Watu wengi wasioyaangalia mambo kwa kina hawaoni jinsi Makonda anavyoichora ramani yake ya kufanya CCM isiwe na mbadala mwingine ndani ya chama hicho zaidi yake.
Pamoja na shutuma zote anazoelekezewa Makonda, bado yeye kila wakati anaonekana kama nyota ing'aayo ndani ya CCM.
Mzee njaa a.k.a Pascal Mayalla alishawahi kuandika bandiko lake kuhusu Makonda, ukilisoma ukiwa umemakinika, utaelewa ninachosema.
Hofu yangu tusiporekebisha mifumo yetu ya kiuchaguzi, iko siku Makonda atakuwa Rais wa nchi yetu. Na siku hiyo ikifika... OLE WETU!