Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,341
- 51,905
Bila shaka Mko Pouwa!
Makonda amesema mbele za Watu kuwa hatalipa Kisasi, kumaanisha kuwa kundi kubwa la Watu analoliambia kuwa hatalipa Kisasi linajua mabaya aliyofanyiwa Makonda.
Hapo kwa upande wangu nimeachwa kidogo kwa sababu sijui nini na kina nani walimfanyia ubaya Makonda mpaka kufikia hatua ya kusema hatalipa kisasi(akimaanisha amesamehe).
Mandela yeye kwa upande wake alisema amesamehe na hatalipa kisasi na wote tunajua nini kilitokea na wabaya wake ni kina nani.
Yesu alipokuwa anasulubishwa naye aliongea maneno hayahaya ya Makonda, hadharani kuwa Mungu awasamehe(asimlipie kisasi) kwa sababu hawajui watendalo. Na wabaya waliomsulubisha walikuwa wanafahamika. Halikadhalika na Stephano aliyekuwa anapigwa Mawe mpaka kufa.
Lakini Kwa Makonda nimeachwa Njia panda, au kuna taarifa imenipita. Sasa nataka yeyote anayejua atuambie ni nini kibaya ambacho Makonda alifanywa ambacho alitakiwa alipe kisasi lakini ameamua kusamehe? Na waliomfanyia huo ubaya ni kina nani?
Ukizingatia kuwa Yeye ndiye ambaye analaumiwa na kushutumiwa kwa ubaya.
Nipo hapa,
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Makonda amesema mbele za Watu kuwa hatalipa Kisasi, kumaanisha kuwa kundi kubwa la Watu analoliambia kuwa hatalipa Kisasi linajua mabaya aliyofanyiwa Makonda.
Hapo kwa upande wangu nimeachwa kidogo kwa sababu sijui nini na kina nani walimfanyia ubaya Makonda mpaka kufikia hatua ya kusema hatalipa kisasi(akimaanisha amesamehe).
Mandela yeye kwa upande wake alisema amesamehe na hatalipa kisasi na wote tunajua nini kilitokea na wabaya wake ni kina nani.
Yesu alipokuwa anasulubishwa naye aliongea maneno hayahaya ya Makonda, hadharani kuwa Mungu awasamehe(asimlipie kisasi) kwa sababu hawajui watendalo. Na wabaya waliomsulubisha walikuwa wanafahamika. Halikadhalika na Stephano aliyekuwa anapigwa Mawe mpaka kufa.
Lakini Kwa Makonda nimeachwa Njia panda, au kuna taarifa imenipita. Sasa nataka yeyote anayejua atuambie ni nini kibaya ambacho Makonda alifanywa ambacho alitakiwa alipe kisasi lakini ameamua kusamehe? Na waliomfanyia huo ubaya ni kina nani?
Ukizingatia kuwa Yeye ndiye ambaye analaumiwa na kushutumiwa kwa ubaya.
Nipo hapa,
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam