Makombora kwa Forever Living Products (FLP)

Makombora kwa Forever Living Products (FLP)

Neno nalo

Member
Joined
Jun 10, 2013
Posts
67
Reaction score
54
Habari zenu!

Kwa muda sasa nimeka nikagundua humu JF kuna tabia za kuigana sana.kuna hii biashara ya mtandao ya forever living kila ikitajwa humu imekuwa ikirushiwa makombora with a lot of negativity.initially Ilikuwa inatangazwa sana ila naona kwa trend hata wahusika nayo wakakata tamaa kuileta humu maana utakuta kejeli na majungu nayo.nikajiuliza sana.

siku nilipata safari nje ya nchi katika kushangaa shangaa na kusaka company nkakutana na dada mmoja mtanzania nikafurahi sana.kuja Kudadisi kumbe alikuwa kwenye vacation na binti zake wawili ndo hadi kuja kuongelea forever akisema alijiunga mwaka juzi tu na inamlipa mil 3 sasa akasave ili aje asafiri na wanae kutalii nje ndoto iliyotimia december mwaka jana.

Nikamuuliza mbona forever inasemekana mafanikio ni ukijoin mwanzo tu? Tuliongea kwa kirefu akanihadithia kuwa ni sekretari tu analipwa laki 6 tu na ni mjane.na hakudhani angeweza kuimudu familia mwenyewe.Nilivyorudi nikaamua kuifanyia research hii kampuni nikaja gundua kuna kampuni nyingi sana za network marketing zimeingia tanzania.pia nikagundua forever is just a legit company kama nyingine nyingi na mafanikio ni juhudi

binafsi.hbinafsi.hakuna cha kujiunga mwanzo wala mwisho.watu wameanza kuiponda siku nyingi ila ajabu bado watu wanajiunga na wanafanikiwa.

nikagundua watanzania wengi ni wavivu na ni werevu wa kuongea sio kufanya.Mtu atataka aambiwe ajira zimetangazwa apeleke vyeti au ujasiriamali wa kuzalisha hela fasta.truth remains hakuna kazi rahisi.kila kazi inataka toiling.tusiwe wepesi wa kudissapoint opportunity za watu pasipo kujua undani wake.if it didn't work out for you, to someone else ndo inamsomeshea watoto shule IST where u can't even afford.

Mwingine kilimo kilimshinda akaweza forever au lsn au world ventures etc

Na kwa members wa forever,stand to what you believe inin.usiogope kutangaza unachofanya kisa unaogopa majungu ya JF.hamna haja ya kutangaza opportunity afu husemi ni nini unaacha namba utafutwe privately.hata kama ndo kwanza umeanza, be bold.network marketing is just a good businesses. Imeshakubalika huko first world.mpaka watanzania waikubalI ni miaka ijayo na nyinyi ndo mtaonekana legends who dared to try.

kwa nini uonee aibu your dreams? Nyinyi ndo mnafanya biashara idharaulike humu.njoo JF sema unafanya networking na tangaza the product.ielezee in details.wengine humu wanaponda ila hawaijui in reality.na tanzania bado inalia ajira.

To the lady who shared the business with me in Dubai asante sana. Umeniondoa kwenye kundi la wazembe to a group of few executers.ntajoin na I swear ntarudI kutoa mrmrejesho.na ntafanikiwa tu..afu niwaone waongeaji maarufu humu!


Loh!!
 
Hii biashara siijui kabisa Lakin niko na rafik zangu wanaendesha maisha na wamefanikiwa kwa hii biashara ila kwa vile na mambo Mengi sijapata kuwauliza inaendajee
 
Neno nalo hayo unayosema yanafanana sana. Ila ishu ni kuwa wangapi unaowajua personaly, wamefanikiwa na hii ishu…?
Ukichunguza unaeza usikute. Mimi kuna watu nawafaham walikuwa wanapiga hizi netwrk business na walikuwa brain washed kinoma. Humweli kitu na atakupa nondo zote unazo taka. Kuna mmoja alikuwa foreva mwingine Oriflame.
Nikasema nawapa mwaka tu nione mtafanyaje.
Wamesanda game mbayaaa, wote wawili, wakaanza ponda hii kitu wenyewe.

Inawezekana ikawa ni biashara ya muujuza kuwa inawweza hsi work out kwangu ila kwako ikawa poa.

ALL THE BEST MKUUU, PIGA HIYO BUSINESS
 
Last edited by a moderator:
mi hii biashara kinachonikera ni kudanganya wateja. unauzia watu vitamin supplement kwa bei ya juu kwa sababu tu mteja hafahamu. hakuna tofauti na kina Ndodi au Mwaka.
 
Neno nalo

Network marketing inalipa sana tu ila inataka watu wanaojielewa with good network lakini all in all forever living hailipi kihivyo kuna kampuni za network marketing ambazo kweli unaweza kuachieve ila kwa hao ilikuwa zamani sio sahv hiyo ni biashara kichaa
 
Last edited by a moderator:
Hii ndo fact ningependa kushare nanyi. 80 percent of the first time entrepreneurs fail in any other business. 60 percent fail when they try business for the second time. The number keeps on going down depending on number of trials.

Kwa hiyo mfanyabiashara wa kawaida ana nafasi zaidi ya kufanikiwa oale anapojaribu tena baada ya kufeli. Hii ni trend kwa biashara za kawaida amazo ni acceptable. Haya tuje kwenye network marketing. Kwenye network Marketing ni Market saturation.

Huwa haina nafasi ya ku grow zaidi ikifika certain limit na ndo hapo danger ya kuanguka inapokuja. Tanzania fursa zipo kibao. Kungangania Network Marketing tu ni uvivu tu wa kufikiri. Na sasa hivi zimejaa utitiri balaa :becky:
 
Hii ndo fact ningependa kushare nanyi. 80 percent of the first time entrepreneurs fail in any other business. 60 percent fail when they try business for the second time. The number keeps on going down depending on number of trials. Kwa hiyo mfanyabiashara wa kawaida ana nafasi zaidi ya kufanikiwa oale anapojaribu tena baada ya kufeli. Hii ni trend kwa biashara za kawaida amazo ni acceptable. Haya tuje kwenye network marketing. Kwenye network Marketing ni Market saturation. Huwa haina nafasi ya ku grow zaidi ikifika certain limit na ndo hapo danger ya kuanguka inapokuja. Tanzania fursa zipo kibao. Kungangania Network Marketing tu ni uvivu tu wa kufikiri. Na sasa hivi zimejaa utitiri balaa :becky:
kiuhalisia hizi biashara hazina tofauti na pyramid schemes. wameweka products za kuuza ili kuficha uhalisia wake. ni aibu sana kwa msomi kuingia kwenye huu utapeli.
 
kiuhalisia hizi biashara hazina tofauti na pyramid schemes. wameweka products za kuuza ili kuficha uhalisia wake. ni aibu sana kwa msomi kuingia kwenye huu utapeli.
Na nilisahau ku mention probability ya ku fail ni 95 percent no matter how many times you try. Sasa kitu ambacho hata ukikijaribu mara kumi chaches za ku fail ni asilimi 95 wala hakifai. Ina maanisha kwamba only 5 percent make it. (5 never make it. Hawa 5% ndo wale wa juu juu
 
Kama unajiamini jaribu labda utakuwa miongoni mwa 5% wanaoiweza/wanaosindikizwa.

Huwa hatuipondi tuu, bali tunaonyesha kwamba wasindikizaji katika biashara hizo ni wengi sana.
 
Kama unajiamini jaribu labda utakuwa miongoni mwa 5% wanaoiweza/wanaosindikizwa.

Huwa hatuipondi tuu, bali tunaonyesha kwamba wasindikizaji katika biashara hizo ni wengi sana.
ha ha ha ila sasa wao wanawadanganya kwamba it is for everyone sababu the 5 percent needs 95 percent to survive:becky:
 
ha ha ha ila sasa wao wanawadanganya kwamba it is for everyone sababu the 5 percent needs 95 percent to survive:becky:

Kila biashara is not for everyone. Ubaya wa hii ni mtu unaingia with hopes.the 95% ni wanaozamia pasipo kuifahamu kwa undani wake.humu humu JF kuna watu wamerukia kufuga na kuuza mayai ya kware wakaishia kupeperusha ndege warudi msituni. kila biashara si ya kuparamia
 
Na nilisahau ku mention probability ya ku fail ni 95 percent no matter how many times you try. Sasa kitu ambacho hata ukikijaribu mara kumi chaches za ku fail ni asilimi 95 wala hakifai. Ina maanisha kwamba only 5 percent make it. (5 never make it. Hawa 5% ndo wale wa juu juu

Hiyo ni per research ya nani? I know wengi waliogive up so many times na wakafanikiwa mbeleni. Ni devotion tu.
 
kiuhalisia hizi biashara hazina tofauti na pyramid schemes. wameweka products za kuuza ili kuficha uhalisia wake. ni aibu sana kwa msomi kuingia kwenye huu utapeli.


Hivi hata definition ya pyramid scheme waijua ndugu? Nasikitika u miongoni wa watanzania wale wale nnowasema.read books ndugu and do research.have basis on everything you speak.uspeak.utafika mbali sana.
 
Hivi hata definition ya pyramid scheme waijua ndugu? Nasikitika u miongoni wa watanzania wale wale nnowasema.read books ndugu and do research.have basis on everything you speak.uspeak.utafika mbali sana.
pyramid schemes ni kama Deci. sasa wale wa Deci ukiingiza kuuza na kununua unapata FLP NA GNLD.
 
Hiyo business ni shidaaaa! Kutokamo Inge work out kama wange base kununua na kuuza kama wewe na siyo network ya kusukuma watu wengine, na Kwa kipato cha kawaida huwezi kuuzia watu wengi cause product zao nizamatajiri tu, ukitaka supplement kanunue 21century, wana supplement zote kama za Forevor na bei ambayo ni affordable Kwa kila mtu.
 
Hiyo ni per research ya nani? I know wengi waliogive up so many times na wakafanikiwa mbeleni. Ni devotion tu.
Wewe unawajua wengi sawa ila kuna kitu kinaitwa statitistics na ndo kipimo kizuri cha kujua succes kwa population sio unahesabau marafiki zako tu. Wewe unawafahamu watu wote Tanzania nzima wanaofanya hii biashara? Ndo maana tunatumia available stats.
 
Kila biashara is not for everyone. Ubaya wa hii ni mtu unaingia with hopes.the 95% ni wanaozamia pasipo kuifahamu kwa undani wake.humu humu JF kuna watu wamerukia kufuga na kuuza mayai ya kware wakaishia kupeperusha ndege warudi msituni. kila biashara si ya kuparamia

Kama si for every one why kwa nini mnamshawishi kila mtu aingie na kumjaza hewaa kichwaani aaamini atafanikiwa? Mbona statement zako zinagongana:becky:
 
Back
Top Bottom