X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,604
- 1,848
Ah ah ah ah ah, huyo ndio Mtono na wengine kama yeye ambao watu wa kawaida hawawajui au hawaelewi nini maana ya kuwa Commando (mwanajeshi). Watu wengi sana wameathirika na hizi filamu za kina commando John, Rambo n.k. Wanashindwa kutofautosha ukweli na maigizo.Huyu hata mie nilimsikia kuwa alichanganyikiwa kwenye mafunzo ya Kikomandoo huko Izrael. Ila wengi wanamkubali kuwa alikuwa na uwezo wa kumuona mtu kwa nusu sekunde na atakukumbuka.
Kuna vijana waliiba mahindi na kwenda kuchoma msituni. Wengine walikaa doria wakiangalia kama kuna mtu anakuja. Walipokuja kumuona huyo, wakapotea msituni na kumuacha peke yake. Aliitisha kambi nzima ya jeshi na kuwachoropoa mmoja mmoja. Ila mwisho akajisifu kuwa kama Wanajeshi basi kashatengeneza maana jinsi vijana waliyoondoka hapo na kwa mwendo wa chui na kupotelea vichakani, hadi alijisikia raha. Kwa sababu hiyo akawaachia huku akiwaambia kuwa wasirudie tena maana yeye siku zote yupo hatua moja mbele ya KURUTA/SERVICE MAN.
Tanzania imepeleka askali wengi sana nje kwenye mafunzo ya kijeshi, na kiitelejinsia... Vijana wengi wa zamani walipelekwa Israel (Japokuwa Mwalimu alisema hatuna uhusiano nayo), Cuba, Bulgaria, Canada, Urusi, UK n.k. Naweza kusema jeshi la Tanzania ni katika jeshi bora sana katika majeshi ya Afika Mashariki na kati na haswa jeshi la Miguu.
Tumepeleka wanajeshi nchi nyingi kusaidia kuondoa madarakani au kutuliza amani kwa mtutu... Kusini mwa Afrika wanautambua mchango wa jeshi letu, haswa kule Msumbiji, Angola, Namibia, Botswana, vile vile tumepeleka majeshi Burundi, Rwanda, Comoro, Congo zote mbili, Liberia, Nigeria, Seychelles, Sierra Leone. Na kote uko jeshi letu lilifanikiwa vizuri sana... Tena linasifika kuwa ni jeshi lenye nidhamu ya hali ya juu sana na haswa kwa raiya wa hizo nchi. Nakumbuka kisa kimoja cha Waganda, haswa wale walioshuhudia vita vya Kagera (Mtukula), wanasifia wanajeshi wa TZ kuwa wakikuona kama wewe umewazidi umri basi watakuhamkia kwa Shikamoo na kisha ndio watakuuliza wapi askari wa Amini... Na kama ni kijana watakusalimia kwa Habari yako... Tofauti na walivyokuwa Askari wa majeshi mengine, na hayo si uko tu hata uko kwengine wanakozungumza Kiswahili.
Sasa wanao dharau wanajeshi wetu na hususani hao Comandos, ajue kuwa hafahamu lolote linalo endelea humo ndani ya jeshi la Tanzania. Kilichokuwa kikionyeshwa pale uwanja wa Taifa ni moja ya mazoezi ya viungo tu, na wala si mbinu za medani.
Kuna mafunzo mengi sana sana, ambayo hayafai kuonyeshwa kwa raiya wa kawaida kama mimi na wewe, kwa sababu yakionyeshwa, ni sawa na kuwafundisha waharifu...
Kwa ufupi wawaulize waliopitia kozi za kijeshi kule mufindi au Arusha (Monduli) watawaeleza vema.