Mie sikuona hayo mambo jana maana huku Sikonge hizo TV zenu hazifiki.
Ila kwa kusoma unachoandika hapo chini, basi nagundua kuwa umelishwa sana hadi kuvimbiwa chakula kiitwacho CNN.
Una tatizo kuwa hata JKT au Mgambo hukupitia. Umeonysha kufahamu mambo kadhaa ila yote ni kupitia CNN.
Kwanza lazima ujuwe kuwa vita ya sasa inapiganwa kwenye INTERNET na UCHUMI. Hizi nyingine ni za wala CNN.
Hizo silaha zote unazosema, kama zingelitumika LIBYA, basi leo hii Ghadaffi angelikuwa bado yupo hai. Vita haipiganwi angani ila ardhini. Kabla hujaenda vitani, lazima ufahamu adui yako kajipanga vipi. Hapo ndipo hizo DRONE, Satelite na ndege za kijasusi hutumika. Ila zote hizo, husaidia tu kuweka NJIA ya Komandoo ili waende kulisoma vizuri eneo husika.
Kila ikitokea vita, Komandoo ndiye huwa MSINGI wa kushinda vita. Hata USA walipotaka kumuuwa Osama, kwa nini hawakupeleka hizo DRONE zako zikamuuwe? Duniani, hivi vikosi vipo vingi sana na si kuwa vimeisha kwa sababu kuna Drone sasa. Vikosi vipo na wanakula mazoezi ya hali ya juu ili kukabiliana na mabadiliko ya dunia. James Bond huwa ni kielelezo kizuri ingawa ile ni FILM tu hasa kwenye Silaha na ujuzi wa kutumia New Technology.
Mwisho kumbuka, ni MJINGA au TAAHIRA aitwaye Komandoo atakuja na kukuonyesha UJUZI wake wote. Hilo hata JKT wanafundishwa kuwa, mkiwa kwenye KIKOSI na mpo vitani, ni marufuku kutumia silaha KUBWA KULIKO ZOTE mlizonazo. Silaha pekee huwa inakushtaki kuwa mpo wangapi. Hii ikiwa na maana, ukisikia Light Machine gun, unajua ni watu kiasi gani, ukisikia Heavy M.G. au RPG, pia unaelewa ni kikosi gani hicho na hiyo inaenda hadi kwenye kutumia Vifaru au Mizinga.
Wale jamaa kama kweli ni Makomandoo na siyo Wanafunzi, basi kama wanaVIFARU, jana umeona SubMachine Gun (SMG).
Kama kweli wale ndiyo makomandoo wa tz na ule upuuzi walio uonyesha pale uwanjani ndiyo walichagua mambo ya hatari ktk mafunzo yao bas ni upuuzi mtupu hakuna lolote ni uhalo na ushuzi 2.
Jaman 2achen kushabikia vi2 visivyo kuwa na msingi hv kwa dunia ya leo ule upupu uliyo onyeshwa na makomando unaweza ukalisaidia taifa kweli??
Labda wa2mike kwa kukamata vibaka na mateja wanao2sumbua mtaani.
Ikiwa majambaz 2 wanao 2mia siraha kal huwa wanasumbua vyombo vye2 vya usalama kwa ajiriya mafunzo ya kimagumashi.
Kwa wale wote wanaowasifu na kuwapamba kwa ule uharo walio ufanya pale uwanjan ni kipi kilicho wakuna.
Kama ni zile mbao lain za dali kuvunjiwa mwilin mwao bas wamasai wapo juu kwani huvunja zile fimbo zao kwa kuipiga pajan.
Na kama ni kupasua vile vigae koko njoen huku uswailin wa2 wanapasua nazi kwa kutumia two nakozi.
Kama kwa kuruka juu na kupiga tobi geri(tikitaka) wale walio kuwa kwenye kampen za kara pina watatoa ushahidi wa kutosha au kama kuna mtu alisha wahi kuja taifa uwanja wa basketi wakati wa mashindano ya shotokan karet hatashangaa.
Jaman narudia tena kama wale ndiyo makomandoo wa tz bas yabid tusikitike sana.Zile mbinu ni za miaka ya 30 au 40 na cyo dunia ya leo ya dot com.
Ni vita gan utakayopigana leo hii muanze kushikana shikana.
Dunia ya leo watu wanafanya vita kwa ndege zisizo kuwa na ruban je hawa vimbora wetu wataweza?!
Au ni zile mbwembwe za kukimbia wamebeba mabeg ndiyo mnawasifu nenden ubungo mkakutane na TEMBO anaekimbia amebeba begi lenye matofari ya block ndan.Na kukimbia kutoka ubungo mpaka mbez na kurudi.