Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mkuu Bitoz kwenye kombe la Dunia la mwaka 1990 pale nchini Italy, kuna matukio mengi ya kukumbukwa japo Kombe la Dunia lile wataalam wanasema ndio michuani mibovu ya kombe la Dunia kwa kuwa timu nyingi zilienda kupaki basi na kufanya mpira usiwe wa burudani bali wa mbinu zaidi na haishangazi kuona magoli yaliyofungwa yalikuwa machache sana.

Baadhi ya matukio ya kukumbukwa ni kama yafuatayo.
 
1924 - Zelmar Michelini anazaliwa.

1976 - Zelmar Michelini anafariki Dunia.

Alikuwa ni mwandishi wa habari kutoka nchini Uruguay.

Aliuwawa kutokana na misimamo yake katika kazi yake.

Ni mmoja kati ya watu maarufu wachache kuzaliwa na kufariki tarehe na mwezi unaofanana.
Aendelee kupumzika kwa amani
 
Kweli matukio yanafanana sana.

Kikosi kile cha Marehemu kocha Bruno Metsu hakika kiliushtua Ulimwengu wa soka.

Wachezaji mahiri kama Tony Silva, Omar Daf, Khalilu Fadiga, Nahodha Aloiu Cisse ( kocha wa sasa ), Ferdinand Colly, Papa Bouba Diop, Hussein Diouf, Henry Camara na wengineo hakika kilikuwa ni kikosi cha dhahabu.
3e6906f53289fb784582a4b283b5ef3c.jpg
e4776354c6b67b42caa88c08ea0f5228.jpg
9b5dc6e1c88aac98aac3cc8c5140b675.jpg
Ufaransa aliondolewa kwa aibu kwenye hatua ya makundi bila kuambulia hata kagoli kamoja nafikiri
.
.
.
Tukutane baadaye mdau
Nikutakie siku njema
.......
 
6. Katiak Mechi ya Nusu Fainali baina ya England dhidi ya Ujerumani, Paul Gascoine Gazza alipata kadi ya njano iliyomfanya kama England ingefuzu fainali angeukosa mchezo huo.

Hali hiyo ilimfanya Gazza kutumia muda mwingi wa mchezo akimwaga chozi, na picha za kulia kwa Gazza zikawa maarufu hiyo ni baada ya umaridadi mkubwa alioufanya katika mchezo huo.

Bahati mbaya, England akaenda kufungwa kwenye matuta na kutolewa.
 
7. Katika Nusu Fainali ya Argentina dhidi ya Mwenyeji Italia iliyofanyika katika uwanja wa San Paolo jijini Naples nyumbani kwa timu ya Napoli, Diego Armando Maradona aliomba mashabiki wake wa Napoli wampe sapoti kwa kushangili Argentina.

Mashabiki wakagoma, wakaonyesha uzalendo kwa kuishangilia timu yao ya Italia, lakini haikufua dafu, Italy alitolewa na Argentina akaingia fainali.
 
8. Fainali ya kombe la Dunia ilikiwa ni Argentina Vs Ujerumani.

Ambapo ilikuwa ni marudio ya fainali ya mwaka 1986 iliyofanyika Mexico.

Safari hii Ujerumani alilipa kisasi kwa kuifunga Argentina bao 1-0 na kutwaa ubingwa huo.

Hayi ni mambo kadhaa ya kukumbukwa ambayo niliona nishee nanyi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom