Makapuku Forum

Makapuku Forum

Ni kweli kabisa
Sasa nasubiria mahafali tu ambayo naamini wote mtashiriki
Karibu tena. Uliondoka kabla sijawa mwenyeji sana hapa Makapuku. Wakati ule nilikuwa nachungulia tu na kupotezea. Kamwe sikuota kuwa siku moja patakuja kuwa kimbilio langu la kuondoa stress na kujifunza mambo mbalimbali kuanzia historia (Dikteta Mussolini anatusomesha sawa sawa), muziki (tunafundishwa na Obe), Habari za magazetini (Shululu), top ten pamoja na Je Wajua (Madenge na makapuku wengineo), Mambo ya imani (Mtumishi Blessed Hope anahakikisha hatuendi motoni), Ulimbukeni wa Mapenzi (Shedede na "mkewe") pamoja na utani na vichekesho visivyo na mwisho kutoka kwa akina Shunie, Husna, Tumosa, Sakayo na mumewe) na makapuku wengine.

Hongera kwa kumaliza masomo na karibu tena. Bila shaka tutafaidika na ulichojifunza huko Israeli. Hata kama ni zile ishu za jamaa wa Mossad we tumegee tu. Blessings!
 
bhinamu nisamehe kwa niaba ya kapuku wote ..yaani hapa ndo nimepata upenyo wa kulala kidogo nikapita kwa familia yangu pendwa

shangazi yako sijiu aliyemtolea ya moyoni kule ndo kamficha wala sielewii ,,
Umeruhusu mlinzi akaozwa ndoa ya mkeka sasa waifu kapotea. Japo mlinzi yule alikuwa bomu na mtoro lakini alikuwa anasaidia saidia.

Anyway, kabla hajapotea Shunie alikuwa analalamika kuwa hakuwa OK na akawa anamuomba Mama Mchungaji amuombee. Natumaini huko aliko hajambo. Ukiongea naye mwambie she is also in my prayers!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom