Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki Ni Maisha.

Habari Makapuku, ninakuletea tena kipengele chetu cha muziki tukijikita zaidi kwenye gitaa. Hata hivyo leo ni siku ya tofauti kidogo, maana ndiyo kwanza tumemaliza kuwasindikiza watanzania wenzetu 35 waliofariki kwa ajali huko mkoani Arusha. Mungu awapumzishe panapostahili hili tukitafakari namna ya kuepukana na ajali zinazoepukika.

Mkumbuke hatujasahau kilichotokea shule ya Shauritanga (nilipoteza rafiki yangu wa karibu sana).

Leo tutaangalia zaidi mapigo ya 'violin' na hasa kuendana na tukio la leo. Nilipandisha clip hizi mapema na sioni ubaya kurudia moja na hasa ile iliyopigwa na wanabendi ndani ya meli ya Titanic. Wimbo wanaoupiga unaitwa KARIBU ZAIDI NA WEWE upo kwenye nyimbo za Tenzi, kwa kiinglishi unaitwa Nearer My God to Thee.



Tuko pamoja sana. Love

Ameen binamu asante sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom