Makapuku Forum

Makapuku Forum

Leo sitaleta kipengele cha " Leo katika Historia "

Kama kuna mtu yuko tayari anaweza akanisaida.
Sawa mkuu ubarikiwe,itabidi tujifunze kuandaa hivi vitu,Mungu atusaidie tuwe na skills tofauti za kuwezesha haya mambo,mimi nitaomba ukipata nafasi unielekeze namna ya kupata niwe nasaidia wakati mngine,ubarikiwe mkuu
 
Mwisho wa segment moja ndio mwanzo wa segment nyingine.

Kwa ushirikiano mnono kabisa wa BlessedHope na Obe (Jorowe)
Tunakwenda kupata Unbelievable Fact (UF)
Asante kwa kutushirikisha mimi na Obe kudhamini segment hii ubarikiwe
Leo tutaangalia zaidi vilevi twende sawa
9ce336e9ef45def476fdc8ec9263b1e9.jpg
 
ZABURI 46

1 Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu,Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.

Mungu kwetu ndiyo kimbilio katika kila shida mkimbilie yeye atakupa msaada ambao hujawahi pata mahali popote.
simama imara katika imani yako.
Omba kwa bidii.
Jitie nguvu kuwa unaweza kumuomba Mungu lolote naye atakutia nguvu ambayo hujawahi kuipata maishani mwako.
Ni yeye alikuumba.

Anajua idadi ya siku zako hapa duniani.
Anajua mahitaji yako yote Anajua kuingia kwako na kutoka kwako.

Mkimbilie yeye.

Atakutia nguvu.

Atakupa msaada.

Mateso yatakoma.

TUOMBE:
Baba wa mbinguni asante kwa siku mpya ya leo,asante kwa kutuamsha salama tukiwa wazima na afya njema,karibu majumbani mwetu Baba,makazini mwetu,kwenye mashamba yetu,kwenye biashara zetu,kwenye ndoa zetu,kwenye uchumba,kwenye masomo,mawazoni mwetu,linda mifugo yetu Baba mwema.

Ponya wagonjwa Baba kwa namna ya pekee tunamkumbuka Mondray mkono wako ukamguse umponye awe mzima mwili na roho.

Farijiwafiwa,tunawaombea marehemu wote wapumzike kwa amani,waongoze wasafiri nchi kavu,majini na angani wafike salama,bariki vijana wetu wote kidato cha sita wanaoendelea na mitihani wakumbushe yote Baba mwema,wasaidie wenye mashaka na changamoto mbalimbali wakumbatie Baba waondoe mashaka wape nguvu mpya.

Tuimarishe tukupende,tukuheshimu,tukutegemee,tukutwishe fadhaa zetu ni wewe peke yako ambaye una jibu la maswali yetu yote.

Asante Baba kwakuwa utatenda sawa na mapenzi yako,tunaomba yote katika jina la Yesu Mpatanishi na mwokozi wetu Amen

NAWATAKIA SIKU NJEMA

MBARIKIWE SANA
Ameen mama mchuchu asante kwa sala ya asbh ubarikiwe sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom