Shimba ya Buyenze
JF-Expert Member
- Dec 22, 2014
- 183,582
- 1,105,417
Nisikudanganye Mtumishi. Mimi siyo mwanasheria na kusema kweli mbali na kujua haki zangu za msingi kama raia wa Jamhuri ya Tanzania sijui cho chote kuhusu sheria.Za asubuhi mkuu umeamkaje?vipi hali yako?pole Mungu aendelee kukuimarisha.
Nimesoma ujumbe wako natamani kuelewa zaidi,unisaidie kufafanua hapo,khs kesi kufanana na Bashite,napenda kujifunza ili pia nipate maneno ya kuwaeleza wanielewe na wachukukuliw hili suala kwa kulielewa,hivi wapo njiani wanakuja,nadhani usiku nitakuwa nao hapa
Umesema kuwa walifeli kidato cha nne wakafanya mbinu wakabadili matokeo yao kinyemela (wakagushi vyeti) na matokeo hayo feki ndiyo yakawafanya wapate nafasi ya kuendelea na masomo yao mpaka wakapata ajira; na leo kosa lao walilofanya zamani ndiyo limesababisha watumbuliwe. Sijui tafsiri ya kisheria lakini nadhani kubadili matokeo kinyemela ni kosa. Kama kuna kapuku mwanasheria anaweza kutufafanulia zaidi.
Nimesikia TLS chini ya Tundu Lissu imewashauri wafanyakazi wote wanaoamini kuwa wametumbuliwa kimakosa waungane wafungue class action suit dhidi ya serikali na TLS itawapa msaada wa kisheria bure. Wanaweza kupata ufafanuzi wa kosa lao kisheria (kama wametenda kosa) na watajua cha kufanya baada ya hapo. Washauri wawasiliane na TLS au mwanasheria ye yote angalau wajue kosa lao limekaaje kisheria...and then they can go from there.
Bashite yeye alipiga ziro form 4 akanunua cheti cha mtu mwingine. Hawa matokeo hayakutosha wakajazia jazia kinyemela kwa majina yao yale yale. Sijui yupi ana kosa kubwa zaidi ya mwingine. Uwe na amani mtumishi na wape pole sana. Waambie wasikate tamaa. Maisha ni lazima yaendelee ati! Mungu Atawafungulia milango mingine!