Makapuku, wikend ndo tunainza hivi kwa kujiburudisha na nyuzi za gitaa kutoka kwa magwiji mbalimbali Afrika. leo tunaye mkongwe mwingine tena.
Salif Keita, huyu utamtambua kwa sauti yake adhimu lakini pia kwa kuwa ni mwanamuzi mwenye albinism. Tatizo la ngozi yake halijamfanya asiwe mahiri katika kile anachokifanya, muziki.
Keita keshafanya ziara zenye mafanikio makubwa sehemu nyingi duniani na album yake ya M'Bemba ilitwaa tuzo kadhaa ikiwemo ya BBC.
Kama walivyo magwiji wengine wa Mali, Salif alifanya 'korabo' na gwiji la kora Toumani Diabate na leo nakuacha nao uburudike