Makapuku Forum

Makapuku Forum

HESHIMA
1 PETRO 2

17 Waheshimuni watu wote .wapendeni ndugu Mcheni Mungu.Mpeni heshima Mfalme.
Heshima,Utii,Upendo ni tabia ya kimbingu Tumerithi kutoka kwa Yesu Kristo.Alitii hadi mauti ya msalaba .
Bila Upendo ni ngumu kuonesha Heshima na Utii wetu kwa Mungu na ndugu zetu pia
Mtii Mungu kupitia Tabia yako,lugha zako,mavazi yako,,mienendo,mawazo,muda wako,mali yako,jamii inayokuzunguka
Usione aibu kumtangaza Mungu kisa watu watakuonaje,lazima watu waheshimu msimamo wako kwa Mungu wako,Mungu wetu ni mwema anatupenda sanasana na kutupigania

Tuombe:Mwenyezi Mungu Baba wa Mbinguni asante kwa kutufikisha umbali huu na kutuamsha salama,tunaomba ututakase makosa yetu yote,Bariki kazi zetu zote za mikono yetu siku ya leo,tupe kukupenda wewe kwa moyo,nguvu na akili zetu zote .Siku ya leo ifanye iwe baraka tukuone wewe.
Tunawakumbuka wasafiri,wafiwa,wagonjwa,wanafunzi,watoto,wazee , makapuku wote na wenye shida mbalimbali .Asante Baba kwa maana utatenda.Amina


MBARIKIWE
asante mama mchuchu ubarikiwe na ww
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom