Makapuku Forum

Makapuku Forum

1969 - Lucas Radebe anazaliwa.

Beki wa kati wa zamani wa Kaizer Chiefs, Leeds United na timu ya taifa ya Afrika Kusini.

Ni wakati alipokuwa Leeds United iliyokuwa inashiriki EPL, Radebe alijitengenezea Jina kubwa katika Dunia ya mpira.

Alichaguliwa kuwa kepteni wa Leeds United na kumfanya kuwa Mwafrika wa kwanza kuwa nahodha katika timu ya ligi kuu Uingereza. Alikuwepo kwenye kikosi kilichofika nusu fainali ya Uefa Champions League mwaka 2001 akiwa na akina Rio Ferdinand, Alan Smith, Mark Viduka, Harry Kewell nk

Alitwaa ubingwa wa mataifa ya Afrika mwaka 1996 katika ardhi ya Nyumbani.
e6fe4f7fae878cd0ff1d6fc7c35c40f1.jpg
6648d03cddc06d32f180d6b2df8a1155.jpg
2eeb6235a41359353e46b0c70b361502.jpg
mkuu akiwa na akina Benni Mc Carthy na Mark Fish si walichukua AFCON 96?
Halafu wakasumbua WC 98 Au nimekosea?
...
 
Mwekahazina umejionea mwenyewe matokeo ukwaju kabisaaaaaaaaaaa

Mukongo aka Baba mchungaji ulichokisema kimetokea japo mm nilikuwa sijui kama kitakua kiama kama ilivotokeaa ....

Ila mkuu ndo maana kipindi tunaipitia mapema ilinichukua mda kudadavua kibibi hiki ....anyway kwanza pole kwa Dortmund ila na Leo Siku ila Juve wewe

Twende sawa kidogo mkuu ..... Juventus 3-0 Barcelona.

Moja ya vitu vilivyowafanya Juventus kutoka na clean sheet ni nidhamu yao ya kufanya making katika eneo lao, team work pia.... Wanapopoteza mpira wanafanya pressing za haraka kuziba mianya katika eneo lao, na ndio maana mara nyingi Barcelona walikuwa hawajui wafanyaje wanapofiki nje ya box la Juventus sababu wanakuta teyari pameshajaa.....

W-formation (3:4:3) inafeli ugenini..... Huu mfumo kuna wakati unakupa unachotaka kama patterns zitafanya kazi kisawa sawa na kama utakutana na timu itakayo shindwa ku unloack mipango yako.... Pamoja na kuwa na utatu wa MSN Bado katika mchezo wa Leo fc Barcelona walihitaji kutumia mipira ya kupiga nje ya box..... Ndio maana mipira michache iliyopigwa na Barcelona nje ya box la Juventus ilikuwa na madhara kuliko mipira iliyoingia ndani ya box kama penetration pass.

Miracle appear at one.... Wenye mizimu yao ndivyo husema angalia mchezo uliopita alipita kwa jumla ya goli 6-5.... Hii inaonyesha ubora wa fc Barcelona ulivyo chini katika michezo ya ugenini ila pia Barcelona udhaifu wao mkubwa unaanzia katika eneo la kiungo mpaka kwa back line yao... Na ndio maana wanaruhusu goli nyingi zaidi japo nao wanafunga pia.

Paul dybala alikuwa anacheza nyuma ya mshambuliaji wa mwisho Gonzalo Higuan na mbele ya viungo wawili Pjanic na Khedira akiwa katikati ya Mario mandzukic na Juan Cuadrado.... Huyu dybala ndiye mchezaji aliyekuwa free uwanja kwa upande wa Juventus.... Aina ya mguu anaotumia, aina ya uchezaji wake, namna alivyofunga magoli yake hakuna cha kushangaa..... Eneo alilokuwepo namna alivyopokea mpira alivyo turn na angle aliyompeleka Ter Stegen ni kazi ya mguu wa kushoto tu kwa goli la kwanza....

Goli la pili la dybala sijui Pique alikuwa anawaza nini maana mpira mpira ulipopitishwa na eneo alilokuwepo unaendelea kumpa credit mpigaji..... Hii miguu hata ile timu yetu inaikosa 100%.

Kwangu man of the match ni Georgia Chiellin..... Making nzuri kama mtu wa mwisho, bloking na interception ndani ya box lake ni ushujaa wa kiwango cha juu....

Barcelona wanapoteza mchezo wa pili mfululizo ndani ya siku 4.... Timu ina uchovu sana na hii inatokana na ufinyu wa kikosi.

Tusubiri kiwanja cha miracle labda kuna chochote kitu.....ila

mwenye kujua au kuwa na kumbukumbu atukumbushe ....Hivi Messi mara ya mwisho kumfunga huyu bwana lini ???
09fbe5d485bbcd8b04f6a5188ef42c88.jpg
Kwenye fainali ya 2015 nafikiri nitareview
 
1980 - Samuel Doe anaongoza mapinduzi nchini Liberia baada ya kumpindua na kumuua Rais William Tolbert Jr.

Anadumu miaka 10 kabla ya yeye kupinduliwa na kuuwawa kinyama kwa kukatwa baadhi ya sehemu za mwili wake kama vile Masikio, mikono nk
061879a05087fe2cbf336fd8c0c4de4c.jpg
4b9b2cefe04ce661272964fc08dd8827.jpg
7f98599328a2ca5be5a0cacef5154b32.jpg
29a9ebe65e18081772bef9a924501b7f.jpg

Ndo Dikteta kilaza zaidi kutokea duniani alikuwa na cheo cha koplo(V mbili)
......
 
1984 - Edward Sokoine anafariki Dunia katika Ajali ya gari huko Dumila, Mkoani Morogoro.

Leo ni miaka 33 tokea kifo chake.

Alikuwa ni Waziri Mkuu wa Tanzania mara mbili, kipenzi cha Wanyonge na watanzania wengi.
Vita yake dhidi ya Uhujumu Uchumi ilipamba moto kiasi cha kufanya walanguzi kumuogopa vibaya.

Alifariki baada ya gari alilopanda kupata ajali ya kugongwa na gari la Mkimbizi wa Afrika Kusini aliyejulikana kama Dumisane Dube.

Alitajwa kama mtu ambaye angemrithi Nyerere kwenye Urais mwaka mmoja baadae 1985 mara baada ya Nyerere kutangaza kung'atuka.

Ajali yake mpaka leo imebaki kuwa na utata wa hali ya juu.

Chuo Kikuu cha Kilimo na Ufugaji mjini Morogoro, Sokoine University of Agriculture ( SUA ) , kimepewa jina lake kama kumuenzi.
e1c3dfe79a857fbc9c09feec13d49f18.jpg
0385ccb3db47fb838015f62e5668b054.jpg
a90ed80c254dcc0413783cef401723cf.jpg
bdc3911b873b708aa9ee6e0045979686.jpg

Aliwahenyesha wahujumu uchumi mpaka wakaamua kumwaga sukari ya magendo mtoni hadi kufanya maji yawe matamu
.....
 
Ilikuwa usiku, hatimae kumekucha!ni upendeleo tuu wa Mwenyezi Mungu kwa majaaliwa haya, sifa na utukufu ni zake,tuzidi kuomba huruma zake atujaalie kutumia wakati kwa kutenda yampendezayo ili kupata kheri duniani na kesho kwenye ufalme wake, nawatakia wepesi ktk kazi za mikono yenu,siku njema!
Amen... We pray the same to u
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom