Makapuku Forum

Makapuku Forum

1949 - Bunge la Israel maarufu kama " The Knesset " laanza rasmi vikao vyake kwa mara ya kwanza.
f44a9944b28d1c0f61671fef656e72ae.jpg
814e96ef29da46513b01e3d3bc207b0d.jpg
 
1913 - Jimmy Hoffa anazaliwa.

Alikuwa ni Kiongozi wa zamani wa vyama vya Wafanyakazi huko Marekani.

Baada ya kuongoza Mgomo wa kudai Maslai ya Wafanyakazi huko Marekani, alipotea katika mazingira ya kutatanisha mwaka 1975.

Baada ya msako wa miaka kadhaa wa kumtafuta bila mafanikio akatangazwa amefariki Dunia mwaka 1983.

Mpaka leo haijulikani Hoffa alipotelea wapi, je ni nani alihusika na kifo chake pia imebaki kitendawili.
 
1951 - Kevin Keegan anazaliwa.

Mchezaji na Kocha wa zamani wa Uingereza, ambaye amezifundisha klabu za Man City, Newcastle mara mbili.

Alikaribia kuchukua ubingwa wa EPL mwaka 1997 akiwa na Newcastle United kabla ya kuzidiwa dakika za Mwisho na Man Utd.
 
1913 - Jimmy Hoffa anazaliwa.

Alikuwa ni Kiongozi wa zamani wa vyama vya Wafanyakazi huko Marekani.

Baada ya kuongoza Mgomo wa kudai Maslai ya Wafanyakazi huko Marekani, alipotea katika mazingira ya kutatanisha mwaka 1975.

Baada ya msako wa miaka kadhaa wa kumtafuta bila mafanikio akatangazwa amefariki Dunia mwaka 1983.

Mpaka leo haijulikani Hoffa alipotelea wapi, je ni nani alihusika na kifo chake pia imebaki kitendawili.
5b91958366759a928b44f5ccbf33ae58.jpg
89f549e191712a3b37c39de2105b4d85.jpg
 
1987 - Edinson Cavani anazaliwa.

Mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Uruguay ambaye anakipiga katika klabu ya PSG.

Mmoja kati ya Washambuliaji bora wa kizazi hiki, japo ameshindwa kuwa na uelewano mzuri na Luis Suarez katika Timu ya Taifa.
 
Mussolin5 kwa kuongezea tu;

1867 mvumbuzi wa Kijapan sakichi Toyoda alizaliwa. Akiwa mbobezi kwenye uvumbuzi na umiliki wa viwanda vya kufuma nguo, ndiye mwanzilishi wa Toyoda Automatic Loom Works. Baadaye mwanaye alijikita kwenye masuala ya utengenezaji wa magari, na ndipo jina Toyota (lilionekana kutamkika kiurahisi zaidi kuliko Toyoda) lilipojitokeza na kupata mafanikio zaidi.

56a1d8417da8ef747ed8437f7849fad0.jpg
 
1989 - James Bond anafariki Dunia.

Alikuwa ni mtaalam wa viumbe hai hasa ndege. Alikuwa ni raia wa Marekani.

Jina lake lilichukuliwa na kuanza kutumika katika mfululizo wa Filamu za Kijasusi zijulikanazo kama James Bond.

Mtunzi wa filamu za James Bond, ndugu Ian Fleming alipenda sana kufatilia kazi za James Bond hasa kwa kutazama Vipindi vyake na kusoma vitabu vyake hasa vinavyohusu Ndege, hali hiyo ilipelekea akalipenda sana Jina la James Bond na kuliomba alitumie katika Filamu zake alizozitunga akianza na ile Casino Royale ya mwaka 1953.

Hivyo mwenye jina la James Bond alikuwa ni mtaalam wa ndege ambapo jina lake likaenda kutumika katika filamu za kijasusi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom