Makapuku Forum

Makapuku Forum

1981 - Luisao anazaliwa.

Beki wa kati wa Benfica na timu ya taifa ya Brazil.

Ni mmoja kati ya mabeki warefu wenye nidhamu ya hali ya juu.

Ameanza kucheza Benfica toka mwaka 2003 na ndio nahodha wao.

Anasifika pia kwa kuchomekea jezi yake muda wote wa Mchezo.
 
Kuna binti mmoja kapuku anaupelekesha moyo wangu jamani. Nimtaje nisimtaje?
a9ee325f3b5b73903da083f47efcd9f2.jpg
mtaje aisee usife na ugonjwa wa moyo
 
Leo katika Historia:

1990 - Makubaliano ya Kuziunganisha Ujerumani Mashariki na Ujerumani Magharibi yanafanywa ili Kuirudisha Ujerumani moja.

Hii ni baada ya Nchi hizo mbili kutengana muda mfupi baada ya kumalizika kwa Vita kuu ya pili ya Dunia mwaka 1945 hali iliyopelekea Kujengwa kwa Ukuta mashuhuri wa Berlin ulioziyenganisha nchi hizo.
5ef7e54139d482c989b3420d849c1a52.jpg
3d3e38618f327a52b16fe11c0c7aebe3.jpg
 
- World radio day.

Ni siku ya kimataifa ya Radio. Huazimishwa kwa kusikiliza radio kwani ndio chombo pekee ambacho kinawafikia Wananchi waliowengi.

Radio ikitumiwa vibaya huweza kusababisha maafa, mfano Chanzo cha machafuko katika nchi ya Rwanda mwaka 1994 ni Radio, ambapo watangazaji walichochea Vurugu zilizosababisha mauaji ya Kimbari.
 
1933 - Paul Biya anazaliwa.

Ni Rais wa pili wa Cameroon ambaye ndiye aliyepo Madarakani sasa.

Ameshika Madaraka ya Urais kuanzia mwaka 1982 mpaka sasa amabapo ni sawa na miaka 35 akiwa madarakani.

Ni moja kati ya Marais wa Afrika waliokaa sana Madarakani na anayetawala Kidikteta kwa Mkono wa Chuma kando ya Museveni na Robert Mugabe.
a08422d7c1b3e0170d5d03de61ae9fbd.jpg
d66dfaaac5a32d75921e08ae63af9b46.jpg
fc0789938ea8481bcd198e9c9fab502b.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom