Wapinzani lazima tuendelee kukosoa na hii ndio kazi yetu.
Lakini tuwe wakweli kwa haya;
1. Nchi ilisha nuka rushwa
2. Watu walifikia kiwango cha miungu
3. Dharau na jeuri ya pesa ilizidi
4. Rushwa ilikithiri
KWA SASA
1. Watu wamenyooka
2. Hofu imetawala kwa wafanyakazi wa umma
3. Angalau wanajituma
ATHARI YAKE
1. wateule wengi wanafanya kz kwa kurupuka
2. Wengi wanaonewa kwani haufanyiki utafiti kabla ya hatua
3. Mkuu amewapa wateule wake jeuri kwn hawana semina elekezi
Naye hakemei uonevu huo
4. Mengi yanafanyika kwa matamko bila kufuata sheria
Dira sahihi ikiwepo tutafika tuendako
Tatizo kubwa tulilonaro kama nchi hatuna dira, kila kiongozi anakuja na mambo yake na hayana faida kwa nchi
Kikubwa tutambue dira yetu ni nini
Kipaombele chetu tuanzie na nini
Mfano tunatatizo kubwa sana upande wa sekta ya elimu, kuanzia msingi mpaka vyuo vikuu
Watu wanamaliza chuo hawajitambui na serikali yetu haijalitambua kama hili ni tatizo
Kilimo nayo haina kipaombele chochote kile, angalia hiki kituko, watu wanalima matunda mwisho wa siku yanaoza, je kesho mkulima huyo ataendelea kulima? Bora aje mjini awe dalali
Tuna viwanda vya watu binafsi vya juisi ili kumlinda mkulima wa Tanzania, lazima azam,mo na Coca-Cola wapewa conditions za kununua matunda angalau 15% kutoka kwa wakulima, utaonana watu watakavyokuwa wanashindana kulima, watermelon

, machungwa, tango nk
Kwa hapa tulipofika Tunahitaji kuwa na upembuzi yakinifu wa nini tufanye,
Mimi naona kama bora tunapiga macktime tu