Makapuku Forum

Makapuku Forum

Wanawake wanapenda harusi na wanachukia ndoa na wanaume wanapenda ndoa na wanachukia harusi, harusi ni sherehe ya siku moja na ndoa ni agano takatifu ambalo hudumu milele.

Wengi walipenda harusi ila walipoingia kwenye ndoa hawakuwa na furaha sababu walipenda zaidi kuvaa gauni/suti za harusi kuliko kuwa tayari kuyavaa majukumu ya ndoa na uwajibikaji .

Ndoa nyingi za mbwembwe huwa na mwisho mchungu na hasa pale wahusika walioingia kwenye ndoa kwa hitaji moja la kuoa/kuolewa sababu ya msukumo wa wazazi au pesa za muda mfupi au kushika mimba na kuwa kiunganishi cha ndoa .

.

Wanawake/Wanaume wanapenda kuzaa ila wanachukia malezi na ndio maana unakuta msichana mwenye mtoto ana miaka 23 ila mtoto wake analelewa na mama yake na yeye anakula ujana sababu hawezi kulea mtoto wake mwenyewe ,wanaume wengi wanajua kuzalisha ila kutunza hawawezi na akifanikiwa kutunza jua hawezi kulea mtoto.
karibu sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom