Makapuku Forum

Makapuku Forum

Magazeti ya leo August 5, 2023
Screenshot_20230805_063839_Opera%20Mini.jpg
 
KATI ya vipigo vikubwa zaidi kwenye Ligi Kuu ni vya mabao 8, ambapo Yanga iliifunga RTC Kagera 8-0 mwaka 1998, Simba iliifunga Coastal Union 8-1 (Mei 8, 2019), pia Simba iliifunga Singida United 8-0 (Machi 11, 2020).

……….
Screenshot_20230805_065148_Instagram.jpg
 
WAKATI straika Kylian Mbappe akisumbua vichwa vya mabosi wa PSG hatma yake ikiwa haijulikani, taarifa zinadai mabosi wa klabu hiyo wapo kwenye mchakato wa kumsajili mshambuliaji wa Benfica, Goncalo Ramos mwenye umri wa maika 22, katika dirisha hili ili akaongeze nguvu eneo la ushambuliaji.
.
Ramos ambaye msimu uliopita alifunga mabao 27. Alionyesha kiwango bora kwenye fainali za Kombe la Dunia zilizofanyika Qatar akiwa na timu yake ya taifa ya Ureno na kuwavutia vigogo vya barani Ulaya. Hata hivyo, changamoto kubwa inatajwa kufanikisha dili hilo ni kiasi cha fedha ambacho Benfica inakihuitaji.
.
Inadaiwa klabu hiyo inataka Pauni 80 milioni ili kumwachia straika huyo ambaye mkataba wake unamalizika mwaka 2025. Kuna uwezekano mkubwa PSG ikamsajili staa huyu hata kabla ya kumpiga bei Mbappe kwani hata kama staa atabaki huenda asitumike kwenye kikosi.
Screenshot_20230805_065307_Instagram.jpg
 
Mchimbaji wa Madini ya Ruby katika Kata ya Mundarara, Wilaya ya Longido Mkoa wa Arusha Sendeu Laizer amemkabidhi nyumba aliyomjengea pamoja na gari (Noah) aliyomnunulia Mwenyekiti Mstaafu wa Kijiji hicho, Akwilino Nyikini kama shukrani kwa kufanya kazi nzuri katika kipindi cha uongozi wake.

Nyikini amemshukuru Laizer na Wananchi wote kwa ujumla kwa namna walivyotambua mchango wake alioutoa wa kusaidia Jamii katika kipindi cha uongozi wake ambapo amewaahidi kuendelea kuwapa ushirikiano hata katika kipindi ambacho hayupo katika uongozi.

Sendeu amesema kuwa amemkabidhi vitu hivyo kwa kutambua mchango wake katika Jamii huku pia akimshukuru Rais wa Tanzania Samia Hassan kwa kuruhusu uchimbaji wa madini wenye tija nchini.

Mwenyekiti huyo alikuwa akiishi kwenye nyumba ya udongo Kijijini hapo kabla ya kujengewa nyumba hii mpya ya iliyojengwa kwa bati.
Screenshot_20230805_065434_Instagram.jpg
Screenshot_20230805_065454_Instagram.jpg
 
Liliani Msuya, mama mzazi wa watoto wanne waliofariki katika ajali ya gari, mkoani Pwani, akionekana mwenye majonzi na akilia kwa uchungu nyumbani kwake kijiji cha Kisangeni, Wilaya ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro.
Screenshot_20230805_065618_Instagram.jpg
Screenshot_20230805_065639_Instagram.jpg
 
Mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la Shangwe Lodrick (35) Mkazi wa Bangwe Kata ya Izia Manispaa ya Sumbawanga Mkoani Rukwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kukutwa na bunduki aina ya Shotgun iliyotengenezwa kienyeji.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Shadrack Masija amesema "Kupitia taarifa fiche Askari walifika nyumbani kwa Mtuhumiwa kukiwa na taarifa za kwama anajihusisha na matukio ya uhalifu ambapo walifanya upekuzi na kumkuta na silaha hiyo kinyume na sheria"

Polisi wamesema bunduki hiyo ilikuwa inatumika kupora fedha kwenye vituo vya mafuta na maduka yanayotoa huduma za miamala ya kifedha.
Screenshot_20230805_065855_Instagram.jpg
 
Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma maarufu akiongozana na Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole @hpolepole wametembelea bustani iliyotengwa na Serikali ya Cuba kwa ajili ya mashujaa wa Afrika katika Mji wa Havana nchini Cuba (African Heros Park).

Mwinjuma ametembelea eneo hilo kukagua sehemu ambayo itawekwa Sanamu ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ambapo mpaka sasa Nchi mbalimbali zimekwishaweka sanamu za Mashujaa na Viongozi wao kama vile Kenya, Afrika Kusini, Misri, Namibia na DRC.

Hata hivyo, Tanzania bado haijaweka sanamu ya Mwalimu Julius Nyerere katika Bustani hiyo ambapo Ubalozi wa Tanzania nchini Cuba kwa kushirikiana na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo zimeendelea na mchakato huo ambapo upo katika hatua za mwisho kukamilika na Mwinjuma ameahidi kusimamia mchakato huo uweze kukamilika kwa haraka.

Kila mwaka Nchi husika inapoadhimisha siku ya uhuru Mabalozi hualikwa kuweka mashada aidha, wakati wa siku ya Afika Mabalozi wa Afrika hukutana hapo kusherehekea.
Screenshot_20230805_065947_Instagram.jpg
 
Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi na Utaratibu wa Shughuli za Utalii Zanzibar Adil Fauz amesema Serikali ya Zanzibar imekataza Wageni (Watalii) kutoa zawadi hasa kwa Watoto wadogo, kwenye viwanja vya ndege na bandarini Zanzibar na kwamba hata mabango ya kukataza hilo yapo.

Akiongea na ZBC leo amesema Adil amesema “Serikali ishazungumza na kukataza Wageni kutoa zawadi hasa kwa Watoto wadogo Zanzibar na kwenye viwanja vya ndege na Bandari mabango ya kukataza hilo yapo, ukitaka kutoa zawadi basi ni lazima ufuate njia sahihi ikiwemo kufika Serikalini maana hatuwezi kujua vitu unavyogawa vina madhara gani"
Screenshot_20230805_070048_Instagram.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Dunia ina mengi sana na kila mtu hutafuta njia ya kujipatia kipato ili mkono uende kinywani, wakati wewe umekaa bila kazi na kusema hakuna ajira, wala hauna mtaji wa kufanya biashara ili ujikwamue kimaisha fahamu kuwa kuna mtu ambaye kabuni mbinu ya kujipatia kipato kwa kutunza siri na kutoa siri za marehemu.

Wahenga walisema kufa kufaana, sasa basi vifo vya watu wengine vyamfaa mwanaume mmoja kutoka Australia anayefahamika kwa jina la Bill Edgar ambaye amejizolea umaarufu na kujipatia kipato kwa kutunza siri za watu na kisha kuzitoa baadaye kwa familia baada ya mtu huyo kufariki.

Inafahamika kuwa kuna siri ambazo mtu yeyote hatamani watu wengine wazifahamu kumuhusu yeye, lakini kupitia Bill unaweza kuitunza na kisha baadaye akaisimulia kwa familia na marafiki wakati wa mazishi yako.
Screenshot_20230805_073118_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom