Makapuku Forum

Makapuku Forum

Magazeti ya leo August 4, 2023.
Screenshot_20230804_063144_Opera%20Mini.jpg
 
Mshambuliaji mpya wa Yanga, Hafiz Konkoni amesema anahitaji muda kidogo kuzoea mazingira ya Tanzania na Ligi hiyo ili kuanza kuonyesha makali yake kwenye timu hiyo na amekataa kufananishwa na Fiston Mayele.
.
Nyota huyo amewataka mashabiki wa Yanga kuwa na subira naye na kumuamini yeye na wachezaji wengine ili waweze kufanya vizuri na kusaidia timu kufikia malengo yake msimu ujao wa 2023/2024.
.
Konkoni raia wa Ghana awali alikuwa chaguo la pili katika mchakato wa usajili nyuma ya Mcameroon, Emmanuel Dikongue, ambaye dili lake lilikufa baada ya kushindwana katika maslahi.
Screenshot_20230804_064908_Instagram.jpg
 
Kama kuna kitu ambacho Gamondi amewashtua mabosi wake ni uamuzi wake wa kugomea mechi ambayo mabosi wake walitaka timu hiyo ikipige dhidi ya AS Vita ya DR Congo Jumapili, lakini akawaambia hakuna mchezo huo, labda upigwe Avic na hakuna shabiki kuingia.
.
Vita wako hapa nchini lakini Gamondi amegomea wao kucheza Chamazi na Yanga. Gamondi amewaambia mabosi wa Yanga kwamba atafutiwe mechi nyingine kwa timu ya ndani kisha wakipige kambini na sio Chamazi kwa kuwa atakuwa amekwenda kuuza silaha wakati Ngao ya Jamii ni wiki ijayo.
.
Tayari mabosi wa Yanga wameshachukua maelekezo hayo ambapo Arena nafahamu huenda JKU wakashuka mjini kutoka Unguja Zanzibar kuja kujipima na mabingwa hao, na Jumapili hakutakuwa na mechi kama ilivyotangazwa awali.
Screenshot_20230804_065012_Instagram.jpg
 
Tume ya Ushindani wa Biashara (FCC), imesema suala la uwekezaji wa klabu ya Simba tatizo lipo kwa upande wa wanachama wa klabu hiyo na si Mwekezaji Mohamed Dewji ‘Mo’.
.
Tume hiyo ilisema kila upande ulipewa majukumu kwa ajili ya kukamilisha mchakato huo na mwekezaji amekamilisha kwa upande wake lakini upande wa mashabiki umekwama.
.
Akizungumza jana jijini Dodoma, Mkurugenzi Mkuu wa FCC, William Erio alisema anashangazwa na kinachozungumzwa sasa kwenye vyombo vya habari kuwa mwekezaji amekwamisha uwekezaji huo. Alisema mwekezaji kwa upande wake alitekeleza kile alichotakiwa kufanya kukamilisha mchakato huo na upande wa wanachama nao walipewa mambo ya kuyakamilisha lakini mpaka sasa wameshindwa.
Screenshot_20230804_065131_Instagram.jpg
 
Jeshi la Polisi Mkoani Pwani limethibitisha vifo vya Watu wanne (Ndugu wa Familia moja) ambao wamefariki baada ya gari aina ya Toyota Prado walilokuwa wamepanda wakitokea Dar es salaam kwenda Same, Kilimanjaro kugongana uso kwa uso na Scania lililokuwa linatokea Arusha kwenda Dar es salaam.

RPC wa Pwani Piusi Lutumo amesema ajali imetokea saa nane usiku wa kuamkia leo eneo la Mapatano Kata ya Mbwewe Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani na waliofariki ni Dereva wa Prado Neech Msuya (45-50), Mfanyakazi wa Benki ya ABSA na Mkazi wa Dar es salaam pamoja na Watu watatu waliokuwa kwenye gari hilo ambao ni Dayana Mageta(40-45), Norah Msuya (40-45) na Ndugu mwingine wa kike.

Kamanda Lutumo amesema chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa Toyota Prado ambaye alihama upande wake na kugongana uso kwa uso na Scania “Mili ya marehemu wote imehifadhiwa katika Zahanati ya Lugoba kwa ajili ya uchunguzi na kutambuliwa na Ndugu”
Screenshot_20230804_065304_Instagram.jpg
Screenshot_20230804_065326_Instagram.jpg
Screenshot_20230804_065350_Instagram.jpg
 
Club ya soka ya Simba imetangaza kumalizika kwa tiketi za mzunguko za Simba Day siku ya Jumamosi Jijini Dar es salaam ambako itacheza na Power Dynamo ya Zambia.

"Historia imeandikwa, kwa mara ya kwanza tiketi za mzunguko zimemalizika siku 3 kabla ya tukio.... kawaida Mzunguko humalizika siku ya tukio lakini safari hii mzunguko zimeisha mapema tena zimeisha kabla ya madaraja mengine wakati mara zote mzunguko ndo huwa za mwisho, asanteni sana wana Simba tukutane Simba Day" ——— ameandika @AhmedAlly_
Screenshot_20230804_065525_Instagram.jpg
 
Jeshi la Polisi Mkoani Pwani limethibitisha vifo vya Watu wanne (Ndugu wa Familia moja) ambao wamefariki baada ya gari aina ya Toyota Prado walilokuwa wamepanda wakitokea Dar es salaam kwenda Same, Kilimanjaro kugongana uso kwa uso na Scania lililokuwa linatokea Arusha kwenda Dar es salaam.

RPC wa Pwani Piusi Lutumo amesema ajali imetokea saa nane usiku wa kuamkia leo eneo la Mapatano Kata ya Mbwewe Halmashauri ya Chalinze Mkoani Pwani na waliofariki ni Dereva wa Prado Neech Msuya (45-50), Mfanyakazi wa Benki ya ABSA na Mkazi wa Dar es salaam pamoja na Watu watatu waliokuwa kwenye gari hilo ambao ni Dayana Mageta(40-45), Norah Msuya (40-45) na Ndugu mwingine wa kike.

Kamanda Lutumo amesema chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa Toyota Prado ambaye alihama upande wake na kugongana uso kwa uso na Scania “Mili ya marehemu wote imehifadhiwa katika Zahanati ya Lugoba kwa ajili ya uchunguzi na kutambuliwa na Ndugu”
View attachment 2707728View attachment 2707730View attachment 2707731
Wapumzike kwa amani

Madereva tuwe tunapumzika kabla ya kuanza safari
 
Mshambuliaji mpya wa Yanga, Hafiz Konkoni amesema anahitaji muda kidogo kuzoea mazingira ya Tanzania na Ligi hiyo ili kuanza kuonyesha makali yake kwenye timu hiyo na amekataa kufananishwa na Fiston Mayele.
.
Nyota huyo amewataka mashabiki wa Yanga kuwa na subira naye na kumuamini yeye na wachezaji wengine ili waweze kufanya vizuri na kusaidia timu kufikia malengo yake msimu ujao wa 2023/2024.
.
Konkoni raia wa Ghana awali alikuwa chaguo la pili katika mchakato wa usajili nyuma ya Mcameroon, Emmanuel Dikongue, ambaye dili lake lilikufa baada ya kushindwana katika maslahi.View attachment 2707717
Kila la kheri Konkoni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom