Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mpango wa Chelsea kutaka kubadilishana mchezaji na pesa na Juventus katika dirisha hili umegonga mwamba baada ya Juve kuhitaji zaidi ya Pauni 35 milioni na Romelu Lukaku ili kumtoa Dusan Vlahovic kwa matajiri hao wa Jiji la London.
.
Matumaini ya Chelsea hapo awali yalikuwa ni kumtoa Lukaku na kiasi kidogo cha pesa ambacho hakitazidi Pauni 20 milioni ili impate Vlahovic anayeonekana kuwa ni pendekezo la Kocha Maurico Pochettino.
.
Chelsea bado inatafuta straika lakini kwanza inapambana kumuondoa Lukaku kikosini ili kupata pesa na nafasi ya kusajili staa mwingine kwani ikisajili kabla ya mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji hajaondoka gharama za mshahara zitakuwa kubwa na Pochettino ameshaweka wazi kwamba hana mpango wa kumtumia katika msimu ujao wa Ligi Kuu England.

Screenshot_20230805_073443_Instagram.jpg
 
Dada wa mwanamuziki Céline Dion Claudette ameweza kufunguka kwa mashabiki taarifa kuhusu afya ya mwimbaji huyo huku akipambana na ugonjwa adim wa Stiff Person Syndrome (SPS),ambao ni hali adimu ya neva wenye sifa za ugonjwa wa autoimmune.

Dada huyo Amefichua kwamba "hawawezi kupata dawa yoyote" ya kutibu ugonjwa huo lakini anasema "kuwa na matumaini ni muhimu."

Mwimbaji huyo wa Kifaransa wa Canada mapema mwaka jana aliwaambia wafuasi wake zaidi ya milioni 5 wa Instagram hali hiyo inamfanya misuli yake ikaze bila kudhibitiwa. Pia imemfanya kuwa na ugumu wa kutembea na kuimba, alisema, akimaanisha kuwa hataweza kushiriki maonesho yaliyopangwa nchini Uingereza na Ulaya.
-
Screenshot_20230805_170554_Instagram.jpg
 
Katika kuendelea kuhakikisha bidhaa ya mafuta ya petroli inapatikana kwa uhakika maeneo yote nchini, Chama cha Waagizaji na Wasambazaji Mafuta Tanzania (TAOMAC) wamekutana na Waziri wa Nishati, January Makamba katika ofisi ndogo za Wizara ya Nishati Jijini Dar es Salaam.

Katika kikao hicho, TAOMAC wametoa taarifa ya mwenendo wa biashara ya mafuta duniani na hapa nchini pamoja na kuwasilisha changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya mafuta hususani suala la upatikanaji wa dola za Marekani ambapo wamesema m uhaba wa dola za marekani katika soko la fedha unapelekea Waagizaji kupunguza kiasi cha mafuta wanachoagiza kuepuka kuagiza mzigo na kushindwa kuulipia kwa wakati.

Wamesema jambo hilo linaongeza gharama za uendeshaji wa biashara na kuathiri bei ya mafuta kwa mteja wa mwisho, Makamu Mwenyekiti wa TAOMAC Salim Baabde amesema “Biashara yetu inafanyika kwa kutumia Dola za Marekani na inapotokea dola inakuwa adimu sokoni inaathiri moja kwa moja bei ya uagizaji ambayo mwisho wa siku inaathiri bei ya mafuta kwa Mtumiaji wa mwisho”

Kwa upande wake Waziri Makamba amewashukuru kwa ushirikiano waliutoa kuhakikisha kwamba Nchi inapata mafuta muda wote, Waziri Makamba amesema kwamba mlango wake uko wazi wakati wote kwa ajili ya mashauriano.
Screenshot_20230805_170959_Instagram.jpg
 
Klabu ya Simba imewasisitiza wale wote ambao hawajanunua tiketi, kesho wasisogee eneo la Uwanja wa Benjamin Mkapa kwa ajili ya Simba Day ili kupunguza usumbufu usio wa lazima na badala yake wanashauriwa kufuatilia kupitia TV.

Meneja wa Habari na Mawasiliano, Ahmed Ally @ahmedally_ akiongea Dar es salaam leo amesema “Kama huna tiketi kaa nyumbani Jeshi la Polisi Iinasisitiza ili kupunguza usumbufu usio wa lazima, ambao hawana tiketi wanaweza kufatilia kupitia Azam TV”

“Tunawashukuru Wanahabari kwa namna mlivyotuunga mkono tangu mwanzo mpaka hapa na hatimaye utamaduni wa kununua tiketi siku ya mwisho umeisha”

“Ni kazi kubwa ndugu zangu Wanahabari mmefanya kwa kueleza faida ya kununua tiketi mapema, Simba inauthamini mchango wenu”
Screenshot_20230805_171130_Instagram.jpg
 
Gavana wa Mombasa, Abdulswamad Nassir, amepata pigo baada ya Bunge la Kaunti kukataa kumwidhinisha Ofisa Mkuu mteule wa Idara ya Kawi na Mabadiliko ya Tabianchi.

Kwa mujibu wa mtandao wa Taifa leo, Gavana alikuwa amemteua John Kiprop katika nafasi hiyo, lakini madiwani wengi wamemkataa wakishangaa aliteuliwaje wakati hajui Kiswahili, mambo yahusuyo wadhifa huo na Kaunti ya Mombasa.

Kwenye mjadala mkali katika bunge la kaunti hiyo, baadhi ya madiwani, wameshangazwa na hatua ya mtu mwenye utajiri wa Sh41 milioni (pesa ya Kenya) kusaka ajira aina hiyo.

Mwakilishi wa Wadi Chaani, Kaunti ya Mombasa, Franklin Makanga, amenukuliwa akisema mteule huyo hajui Kiswahili ambayo ni lugha inayotumiwa zaidi Mombasa, na pia hajui mitaa ya mji huo.

“Hajui Changamwe, Chaani wala Bangladesh iko sehemu gani. Ataleta mabadiliko gani hapa Mombasa? Hafai na ninaomba bunge hili lisimpitishe,” amesema.

Kwa upande wa Mwakilishi Wadi ya Kadzandani, Fatma Kushe, amewataka madiwani wenzake kufanya uamuzi huru kuhusu watu wanaoteuliwa huku akisema: “Kama mtu hafai, hafai. Tusiogope mtu yeyote,” amesema.

Hata hivyo kwa upande wake Leila Nyache, ambaye ni Mwakilishi Wadi ya Kipevu, aliunga mkono uteuzi wa Kiprop huku akisema ni sifa za elimu yake zilizosababisha ateuliwe kwenye nafasi hiyo.

Nyache hakuwa peke yake, kwani Mwakilishi wa Junda, Sylvester Kai, amesema: “Kutoka Baringo isiwe sababu ya kumnyima nafasi hii. Hakuna sheria ambayo inamzuia mtu yeyote kufanya kazi mahali kokote. Si lazima awe mkazi ama mzaliwa wa Mombasa, tuache ubaguzi.”

Hata hivyo baada ya mjadala huo mkali, bunge la kaunti hiyo, lilikataa kumuidhinisha Kiprop kuitumikia nafasi aliyokuwa ameteuliwa na Gavana Nassir.

Screenshot_20230805_171245_Instagram.jpg
 
Hatimaye Neech Msuya, aagwa rasmi na ndugu, jamaa na marafiki, waliohudhuria ibada iliyofanyika katika Kanisa la KKKT, usharika wa Kijitonyama.

Ibada hiyo imefanyika kabla ya mwili wa Neech kusafirishwa kwenda Ugweno mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya maziko.

Neech na dada zake watatu ambao ni Diana, Sia na Dk Norah, walifariki baada ya kupata ajali iliyotokea wilayani Chalinze, juzi Ijumaa Agosti 2, 2023.

Ajali hiyo ilitokea wakati wanandugu hao wakiwa njiani kuelekea mkoani Kilimanjaro, kwenye maziko ya Mohamed Jaffary Msuya, mtoto wa baba yao mdogo.

Taarifa ya familia imeeleza kuwa baada ya familia kurejea kutoka katika maziko ya Neech huko Ugweno, dada zake watazikwa Agosti 8, 2023, kwenye makaburi ya Ununio kwa Kondo yaliyopo Wilaya ya Kinondoni, mkoani Dar es Salaam.
Screenshot_20230805_171441_Instagram.jpg
 
Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Kusini, imesema kuwa watu wanaotumia dawa ya ‘Vega’ bila kuwa na tatizo la shinikizo la damu, wako hatarini zaidi kupoteza nguvu za kiume na hivyo kushindwa kabisa kushiriki tendo la ndoa.

Akizungumza na Mwananchi Digital katika banda la maonyesho ya kilimo Nanenane, Mkaguzi wa Dawa TMDA Kanda ya Kusini, Elias Magambo, amesema kuwa matumizi ya dawa hiyo yanaongezeka kwa kasi, hali ambayo inaweza kuchangia vijana hao kutokuwa na nguvu kabisa.

“Hii dawa maarufu kama vega, imekuwa ikitumiwa na wanaume hasa vijana wadogo, kwaajili ya kuongeza nguvu za kiume, wakidai kuwa wanaenda kuwakomesha wanawake. Na wamekuwa wakiambizana na hivyo kufanya matumizi yake kuongezeka, hali ni hatari kwa vijana wadogo,” amesema Magambo.

Mkaguzi huyo wa dawa, ameongeza kusema: “Kwakweli hii dawa haifai kutumiwa kwakuwa inaweza kusababishia matatizo ya baadae kwa watumiaji kushindwa kushiriki tendo la ndoa na wenzi wao bila kuipata dawa hiyo…huathiri nguvu za kiume.”

Kwa mujibu wa Magambo, dawa hiyo ni maalum kwa watu wenye matatizo ya presha, hivyo wanatumia ili kuongeza msukumo wa damu mwilini, na iwapo itatumiwa na mtu asiyekuwa na ugonjwa huo, dawa hiyo humuongezea msukumo wa damu kwa kiasi kikubwa, na ndipo mtumiaji huhisi kuongezeka kwa nguvu za kiume.

Kwa upande wake Amina Hussein, mkazi wa Lindi, amesema kuwa wanaume wengi wamekuwa na tabia hiyo ya kutumia dawa za kuongeza nguvu za kiume, na kwamba jambo hilo limekuwa kama ni desturi.

“Wengi hufanya hivyo kama kutukomoa na wakiona sifa sisi kuwasifia bila kujali afya zao, nadhani hili linaweza kusababisha tukapoteza wanaume wanaojiamini ndani ya nyumba na matokeo yake ni janga” amesema Amina.
Screenshot_20230805_171720_Instagram.jpg
 
Waziri Mkuu wa zamani wa Pakistan, Imran Khan, amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela kwa tuhuma za rushwa, baada ya kupatikana na hatia ya kuuza zawadi za Serikali kinyume cha sheria.

Kiongozi huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 71 ambaye ametakiwa pia kutojihusisha na masuala ya siasa kwa kipindi cha miaka mitano, ameshutumiwa kutumia vibaya nafasi yake tangu mwaka 2018 hadi 2022 kwa kununua na kuuza zawadi katika milki ya Serikali ambazo zilipokelewa wakati wa ziara nje ya nchi.

Wakati kesi hiyo ikisomwa, Khan hauwepo mahakamani lakini alikamatwa akiwa nyumbani kwake huko Lahore.
Screenshot_20230805_171831_Instagram.jpg
 
Dada wa mwanamuziki Céline Dion Claudette ameweza kufunguka kwa mashabiki taarifa kuhusu afya ya mwimbaji huyo huku akipambana na ugonjwa adim wa Stiff Person Syndrome (SPS),ambao ni hali adimu ya neva wenye sifa za ugonjwa wa autoimmune.

Dada huyo Amefichua kwamba "hawawezi kupata dawa yoyote" ya kutibu ugonjwa huo lakini anasema "kuwa na matumaini ni muhimu."

Mwimbaji huyo wa Kifaransa wa Canada mapema mwaka jana aliwaambia wafuasi wake zaidi ya milioni 5 wa Instagram hali hiyo inamfanya misuli yake ikaze bila kudhibitiwa. Pia imemfanya kuwa na ugumu wa kutembea na kuimba, alisema, akimaanisha kuwa hataweza kushiriki maonesho yaliyopangwa nchini Uingereza na Ulaya.
-View attachment 2709275
Kuna movie inaitwa LOVE AGAIN ya 2023

Celine Dion yupo humo ndani na afya njema kabisa, bado najiuliza ni yeye kweli au siye sababu kwenye washiriki wa movie huyo ni yeye mwenyewe Celine Dion.
 
Pichani ni moja ya vivutio vikubwa kwenye banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye Maonesho ya Nanenane Nzuguni Jijini Dodoma ambao ni kuku aina ya Brahama wenye asili ya Saudi Arabia na kwa pamoja (wawili) wanauzwa shilingi milioni 1.

Wizara ya Mifugo imesema hao ni kuku wa pili kwa ukubwa Ulimwenguni ambao hufikia mpaka uzito wa kilo 7 na ni kuku wa mapambo na biashara na ni rahisi kufuga kwasababu hufugwa kwa njia za asili kama kuku wengine.

Kuku Jike anaanza kutaga mayai akiwa na umri wa miezi 6 na hutaga mayai yasiyopungua 20 na huweza kuishi mazingira yoyote.

Kuku hao walikuwa sita kwenye maonesho na tayari wanne wameuzwa na kwa sasa wamebaki wawili.
20230806_082831.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom