Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Kusini, imesema kuwa watu wanaotumia dawa ya ‘Vega’ bila kuwa na tatizo la shinikizo la damu, wako hatarini zaidi kupoteza nguvu za kiume na hivyo kushindwa kabisa kushiriki tendo la ndoa.

Akizungumza na Mwananchi Digital katika banda la maonyesho ya kilimo Nanenane, Mkaguzi wa Dawa TMDA Kanda ya Kusini, Elias Magambo, amesema kuwa matumizi ya dawa hiyo yanaongezeka kwa kasi, hali ambayo inaweza kuchangia vijana hao kutokuwa na nguvu kabisa.

“Hii dawa maarufu kama vega, imekuwa ikitumiwa na wanaume hasa vijana wadogo, kwaajili ya kuongeza nguvu za kiume, wakidai kuwa wanaenda kuwakomesha wanawake. Na wamekuwa wakiambizana na hivyo kufanya matumizi yake kuongezeka, hali ni hatari kwa vijana wadogo,” amesema Magambo.

Mkaguzi huyo wa dawa, ameongeza kusema: “Kwakweli hii dawa haifai kutumiwa kwakuwa inaweza kusababishia matatizo ya baadae kwa watumiaji kushindwa kushiriki tendo la ndoa na wenzi wao bila kuipata dawa hiyo…huathiri nguvu za kiume.”

Kwa mujibu wa Magambo, dawa hiyo ni maalum kwa watu wenye matatizo ya presha, hivyo wanatumia ili kuongeza msukumo wa damu mwilini, na iwapo itatumiwa na mtu asiyekuwa na ugonjwa huo, dawa hiyo humuongezea msukumo wa damu kwa kiasi kikubwa, na ndipo mtumiaji huhisi kuongezeka kwa nguvu za kiume.

Kwa upande wake Amina Hussein, mkazi wa Lindi, amesema kuwa wanaume wengi wamekuwa na tabia hiyo ya kutumia dawa za kuongeza nguvu za kiume, na kwamba jambo hilo limekuwa kama ni desturi.

“Wengi hufanya hivyo kama kutukomoa na wakiona sifa sisi kuwasifia bila kujali afya zao, nadhani hili linaweza kusababisha tukapoteza wanaume wanaojiamini ndani ya nyumba na matokeo yake ni janga” amesema Amina.
View attachment 2709286
VEGA kama VEGA... hela isakwa kwa jasho sanaaa..
 
Farhan Jr

Mbele ya Mashabiki 60,000 mbele ya Amiri Jeshi Mkuu, mbele ya Karia wa Karume, mbele ya Chalamila wa Dar Es Salaam! Danny Alves wa Matombo, Morogoro! Shomari Kapombe alikuwa na mechi yake binafsi! First touch kama Mchizi Rick Ross wa Mayback kwenye yatch! Mtawaimba wote ila hizo verse zenu basi Kapombe leo ndio Chorus!

Kocha wangu Robertinho kutofanya mabadiliko ya Shomari Kapombe na Mohamed Hussein kuna kitu amemaanisha, acha tujipe muda ila ana maana yake kubwa sana ambayo imenifikirisha sana, wamemaliza zote! Ina maana wataendelea kucheza sana.

Natamani kukiri kuwa Fabrice Ngoma ni Mtu sana, natamani kukubali Che Malone ni Kitasa sana, natamani kusema tuna Kipa imara sana ila napata ukakasi kwakuwa Dynamos hawakuwa ile timu ya kutupa ile mechi tuliyoitaka sana, walikuwa ‘unga’ sana.

Kuanzia kati mwa uwanja kwenda mbele Simba ni timu sana, ina watu sana hata akikosa Mtu flani huoni pengo sana, wanacheza kwa kupokezana! Onana anajua sana, Kramo dakika chache sana ila amepambana, Saido na Chama wanajuana sana!

Homeboy Aishi ugua pole na urejee haraka sana! Kesho kijiweni nitaanza ubishani wangu timu ipi ina ‘Mademu’ wakali sana maana Simba leo nimeona visu vya hatari sana, haki ya nani maua yalijaa sana
Screenshot_20230807_051707_Instagram.jpg
 
Wazazi wa aliyekuwa mfanyakazi wa benki ya ABSA Tanzania, Neech Msuya wakiweka shada katika kaburi la mtoto wao leo Jumapili Agosti 6, 2023 wilayani Mwanga.

Neech pamoja na ndugu zake watatu walifariki dunia Agosti 2, 2023 katika ajali ya gari iliyotokea Chalinze mkoani pwani.

Screenshot_20230807_052503_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom