Makapuku Forum

Makapuku Forum

Farhan Jr

Zipo wapi nyakati? Wakati ambao Dr Leakey Abdallah anaichukua Roma, Italia ama Venice Mji Ua mpaka sebuleni ama bandani kwako, zipo wapi nyakati wakati Fundi huyu alikuwa anaufanya mpira uvutie kuufuatilia hata kama hujawahi kufika Ulaya, zipo wapi nyakati?

Zipo wapi nyakati nauliza? Wakati mpira tunatazama kwenye nyungo kubwa za wavu? Wakati huo DTV, ITV na baadae Channel 10 tunatulia Champions League! Usiku wa maajabu ya kutisha pale Istanbul, Uturuki penye Etugru sasa hivi! Nyakati ambazo saa 3:45 Usiku wenye baiskeli, wenye tochi za Kaida na betri za National wanasaka kijiji chenye TV watazame mbungi.

Zipo wapi nyakati? Ambapo Mbalamwezi inamulika kuangaza njia za Wapenzi wa soka kufika bandani, milio ya Tembo na Simba lakini sauti za Wahafidhina wa Liverpool wakiimba Fields of Anfield Road zilivutia zaidi, wakati huo Ricardo Kaka anapiga pass kuliko Dobi, zipo wapi nyakati kipindi Andrea Pirlo anakupa Wema Sepetu mbele ya TV yako?

Gone are the days! Wakati Nemanja Vidic anacheza huku anavuja damu, aliwahi kuvunjika Mtu pale Anfield anaitwa Bill Shankly na aligoma kukaa kwenye machela, aliwaambia ni aibu uzi wa Liverpool na Mwanaume kutoka Liverpool kubebwa juu ya kitanda, zipo wapi nyakati?

Zipo wapi nyakati wakati Legend Edo Kumwembe anatawala Ukurasa namba 17 za nyuma ya pazia akimuelezea TH14 Babu Choggo kutoka visiwa vilivyosahaulika La Desarade? Kalamu ilishikwa na ikamwaga wino mzuri kama ambavyo Dada mwenye hamu atashika kalamu ili itoe wino mweupe, ziko wapi nyakati?

Zipo wapi nyakati? Baada ya kutoka bafuni na picha ya @thebestfetty unaenda darasani kutazama daftari lako ulojaza picha za Wababe kama Taribo West, Jay Jay Okocha, Dinho Gaucho, The Original Ronaldo ama Samuel Etoo, zipo wapi nyakati?

Zipo wapi nyakati wakati Cristiano Ronaldo anafunga ndoa na mabeki pale EPL mpaka Ashley Cole aliketi, zipo wapi nyakati za usiku wa baridi kali pale Stoke City, unamtazama Delap ama Shawcross wamekunja sura, wapi Blackburn ya Benjani Mwaruwari ama Wigan ya Amri Zaki? Zipo wapi nyakati? Kabla ya kizazi cha pressing, overlapping na 4-4-2 Diamond

Screenshot_20230801_054856_Instagram.jpg
 
Aliyewahi kuwa DJ wa CloudsFM Steven Mdoe maarufu kama DJ Steve B amefariki dunia leo katika Hospitalini Dar es salaam huku chanzo kikitajwa kuwa ni kupanda kwa presha.

Amstrong Mdoe ambaye ni Kaka wa Marehemu ameiambia @AyoTV_ kuwa Steve B ambaye alikuwa akisumbuliwa na figo toka mwaka 2019 alipelekwa Hospitali juzi na kuwekwa ICU baada ya presha kupanda na baadaye kupanda zaidi na kumsababishia kupoteza fahamu kwa siku tatu kabla ya kufariki.

"Steve B alipoteza fahamu kwa siku 3 ambapo jioni ya leo saa 10 akafariki, alikuwa na tatizo la figo kwa miaka minne tangu 2019 lakini figo sio chanzo cha kifo chake, taratibu za mazishi bado tunazungumza tupange utaratibu lakini tunapokea rambirambi kwa namba 0678689383"

"Steve hakuwa na Mke wala hajaacha Mke na wala Mtoto, hatuna taarifa za Mtoto wake" ——— amemalizia Armstrong Mdoe. #TutaonanabaadaeSTEVEB View attachment 2704337
Apumzike kwa amani..
 
"Tulimsajili Emile Heskey kwa pauni milioni 11, Arsene Wenger alimsajili Thierry Henry kwa pauni milioni 11. Tulimsajili Nick Barmby kwa pauni milioni 6, Arsenal wakamsajili Robert Pires kwa pauni milioni 6. Wenger alikuwa gwiji katika soko la usajili." alisema Jamie Carragher kuhusu tofauti kati ya Liverpool na Arsenal.
View attachment 2702638
Sawasawa..
 
Aliyewahi kuwa DJ wa CloudsFM Steven Mdoe maarufu kama DJ Steve B amefariki dunia leo katika Hospitalini Dar es salaam huku chanzo kikitajwa kuwa ni kupanda kwa presha.

Amstrong Mdoe ambaye ni Kaka wa Marehemu ameiambia @AyoTV_ kuwa Steve B ambaye alikuwa akisumbuliwa na figo toka mwaka 2019 alipelekwa Hospitali juzi na kuwekwa ICU baada ya presha kupanda na baadaye kupanda zaidi na kumsababishia kupoteza fahamu kwa siku tatu kabla ya kufariki.

"Steve B alipoteza fahamu kwa siku 3 ambapo jioni ya leo saa 10 akafariki, alikuwa na tatizo la figo kwa miaka minne tangu 2019 lakini figo sio chanzo cha kifo chake, taratibu za mazishi bado tunazungumza tupange utaratibu lakini tunapokea rambirambi kwa namba 0678689383"

"Steve hakuwa na Mke wala hajaacha Mke na wala Mtoto, hatuna taarifa za Mtoto wake" ——— amemalizia Armstrong Mdoe. #TutaonanabaadaeSTEVEB View attachment 2704337
Dah,my brother,my neighbourhood, R.I.P Dj Skills
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom