Makapuku Forum

Makapuku Forum

Klabu ya Yanga imethibitisha kukamilisha usajili wa Mshambuliaji raia wa Ghana Afidh Konkoni kwa Mkataba wa miaka miwili.

Konkoni (23) akiwa na Benchem Utd msimu uliopita alifanikiwa kufunga mabao 15 katika Ligi Kuu ya Ghana.
Screenshot_20230730_073558_Instagram.jpg
 
Rasmi: Boca Juniors wamekamilisha usajili wa Edinson Cavani na amesaini mkataba hadi Desemba 2024.

Screenshot_20230730_073652_Instagram.jpg
 
Aston Villa haitamsajili winga wa Sporting Lisbon na Ureno Pedro Goncalves, 25, kwa sababu ofa ya juu ya Villa ni £38.6m ambayo ni pauni milioni 30 pungufu ya bei ya Sporting wanayotaka. (Recorg)

Screenshot_20230730_073737_Instagram.jpg
 
Newcastle United imemuuza winga Mfaransa Allan Saint-Maximin, 26, kwa Al-Ahli ya Saudi Pro League kwa £30m. (Mail

Saint-Maximin ataungana na wenzie
Edouard Mendy
Roberto Firmino
Riyad Mahrez
Ryad Boudebouz

Screenshot_20230730_073825_Instagram.jpg
 
Chelsea wamekataa ombi la Juventus la kutaka kumsajili kwa mkopo mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 30, kwa sababu wanataka kumuuza kabisa. (Tuttosport)

Screenshot_20230730_073929_Android%20System.jpg
 
Paris St-Germain wanakaribia kukamilisha dili la kushtukiza kumsajili winga wa Ufaransa Ousmane Dembele kutoka Barcelona. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ana kifungu cha kuuzwa cha £42.8m ambacho kinamalizika Jumatatu. (ESPN)

Screenshot_20230730_074104_Instagram.jpg
 
Inter Miami itajaribu kupanga mechi ya kirafiki dhidi ya Barcelona itakayochezwa kwenye Uwanja wa Nou Camp ambapo itamruhusu Lionel Messi kuwaaga vizuri mashabiki miamba hiyo. Medsi aliondoka miaka miwili iliopita baada ya Barcelona kushindwa kumlipa mshahara kutokana na kanuni za sheria za pesa kuwabana.
.
Mmiliki mwenza wa Inter Miami David Beckham, Jorge Mas wa klabu ya Inter Miami aliweka wazi anatamani kuandaa mechi ya kirafiki ambayo itawakutanisha Messi na mashabiki wa Barcelona.

“Matumaini yangu Messi atapata nafasi ya kuwaaga mashabiki wa Barcelona vizuri, anastahili kupewa heshima anayostahili, nitafanya juu chini kumsaidia mpango huu ufanikiwe kwa sababu anasahili,” alisema bosi huyo.

Endapo mechi hiyo kirafiki itachezwa Nou Camp itabidi kusubiri hadi ukarabati wa uwanja huo ukamilike na mechi za nyumbani za Barcelona zitachezwa katika Uwanja wa Olympic msimu ujao.
Screenshot_20230730_074213_Instagram.jpg
 
Kocha wa Chelsea, Mauricio Pochettino amewasilisha majina ya mastaa watatu ambao anataka mmoja kati yao asajiliwe katika dirisha hili.
.
Mastaa hao ni pamoja na wa Crystal Palace Michael Olise, 21, staa wa Olympique Lyon Rayan Cherki, 19 na kiungo wa Ajax Mohammed Kudus, 22.
.
Chelsea imepoteza wachezaji wengi dirisha hili imepanga kusajili staa mmoja kati ya hao ili kuweka sawa eneo lake la kiungo ambalo limeondokewa na Mason Mount, Kai Havertz na Christian Pulisic. Chelsea imewekeza nguvu zaidi kutaka kumsajili Kudus lakini fundi huyu anadaiwa kutamani zaidi kutua Arsenal ama Man United.
.
Cherki ambakisha misimu miwili kwenye mkataba wake, inaelezwa Chelsea ilituma maskauti Ufaransa kumtazama. Kuhusu Olise, Chelsea imewasilisha ofa ya Pauni 38 milioni kwa Palace ili kumnasa kwani mkataba wake unamruhusu kuondoka kwa Pauni 35 milioniioni ili kuishawishi Palace.
Screenshot_20230730_074331_Instagram.jpg
 
Paris Saint-Germain inataka kukamilisha usajili wa winga wa Barcelona, Ousmane Dembele leo Jumapili au kabla ya siku ya kesho Jumatatu haijamalizika kwani kwenye mkataba wake kuna kipengele kinachomruhusu kuondoka kabla ya Jumatatu ikiwa timu inayomhitaji italipa Pauni 42.8 milioni.
.
Mkataba wa sasa wa Dembele na miamba hiyo ya Camp Now unatarajiwa kumalizika mwakani.
Screenshot_20230730_074423_Instagram.jpg
 
Chelsea imelimwa faini ya Pauni 8.6 milioni na Bodi ya UEFA baada ya kuvunja sheria na kanuni ya matumizi ya pesa chini ya aliyekuwa mmiliki wa klabu hiyo Roman Abramovich.
.
UEFA ilithibitisha taarifa hiyo Ijumaa iliyopita ikidaiwa kwamba Chelsea ilituma taarifa za matumizi ya pesa ambayo haikukamilika. Taarifa hiyo ni kuanzia mwaka 2012 hadi 2019 kipindi Chelsea ilikuwa chini ya bilionea huyo raia wa Russia.
.
Chelsea haitakumbana na adhabu nyingine zaidi ya kulimwa faini ingawa Bodi ya Ligi Kuu England itafanya uchunguzi kuhusu sakata hilo.
.
Chelsea haishiriki michuano ya Ulaya msimu ujao baada ya kumaliza msimu ikiwa nafasi ya 12 ikiwa na pointi 45.
Screenshot_20230730_074525_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Julai 27, 1984 huko Kisarawe Pwani, nyumba mbele kisha mabanda ya uani nipo President pichani alifika duniani, wao walimuita Mtoto, shule ikampa jina la Mwanafunzi, Madrasah ikamwita Muislam na chuo ikasema ni Mwanafunzi, elimu ikambatiza Mhandishi na Wananchi wakampa kura za Urais.

Heavy is the head that wears the crown! Alizaliwa miezi mitatu tu baada ya Edward Sokoine kuaga dunia pale Morogoro, alizaliwa mwaka mmoja kabla ya Mwalimu kuachia madaraka na Umoja wa Kisoviet ulikuwa unaanguka kwa haraka sana, wazazi walimwita baraka.

Literally unaitazama picha ya Rais wa Ikulu tatu kama Mzee Shabaan Robert angekuwa hai angesema “Rais ana Ikulu moja ila Rais Hersi ana amezulu Ikulu tatu, Magogoni (TZ), Kamuzu Palace (Malawi) na Ikulu ya Zanzibar, wahadithi wakiona rahisi wala sio najisi waende wao wajihisi rahisi” sio rahisi.

Rais Msela anayeishi kama Mwanamapinduzi Ahmed Ben Bella, hata Mswahili atavaa suti, hata Maasai ataingia kazini na shuka, hata Gangster hulegeza macho ukimpa cotton buds! Tayari amewasha sigara usimtume Mtoto utamuuwa mapafu, dropping bars bila motorcars.

Hii ni history making kuacha majina! The Kisarawe Legend ameweka Ligi Kuu kabatini, FA kabatini, Ngao kabatini na Medali ya CAF kabatini! Mafanikio ni nini? You are looking at greatness! The walking work of art.

Screenshot_20230730_075535_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Miaka ya 1980 Serikali ya Hispania ilianza mchakato wa kuhakikisha mabadiliko kwenye mifumo ya taasisi, ambapo iligusa mpaka mpira wa miguu ambapo timu zote zilipaswa kuwa Kampuni (PLCs) kasoro timu nne pekee za Ligi Kuu, nazo ni Real Madrid, Barcelona, Osasuna na Bilbao zikasalia kuwa za Wanachama.

Walitaka kuondokana na stori nyingi kwenye mfumo wa Wanachama! Mfumo huu una shida sana pasipo elimu klabu zingekuwa maskini.

Simba na MO nani mwenye hisa nyingi? Jibu ni Simba ambao ndio Wanachama, Yanga na GSM nani mwenye hisa nyingi? Jibu ni Yanga ambao ni Wanachama! Je hawa Wanachama kupitia mfumo huo wanachangia chochote? Wapo active ama dormant? Majibu kaa nayo.

Mashabiki na Wanachama wa Simba na Yanga ninyi ndio Maboss wa hizi timu lakini wangapi wana kadi za Uanachama ama Ushabiki za Yanga? Jibu ni wachache sana, klabu zote za Wanachama duniani mtaji ni watu wake, je ninyi ni mtaji? Mnaifaidisha klabu?

Simba lets talk! Suala la Wanachama wapya limestuck maana yake waliopo ndio Mtaji je huo mtaji unatumika? Wanalipa ada za Uanachama kwa wakati? Je sasa hivi kuna kadi za Mashabiki je tupo hima kuzichukua ili kunufaisha klabu? Majibu yoote chukua kisha kaa nayo!

Viongozi wa Simba na Yanga lets talk! Ninyi mna nafasi ya kubadili mitazamo ya hawa watu! Linapokuja suala la maslahi duniani kote taasisi kubwa hukaa chini kwa pamoja kuweka mipango ya pamoja na kuja na majibu ya pamoja, bila kujali utofauti wa mitazamo.

Linapokuja suala la upinzani Simba na Yanga mnawazidi Madrid na Barcelona? Lakini watazame suala la SuperLeague hawa Wanaume wawili walisimama mbele ya dunia bila kuogopa, watazame suala la Haki za maudhui wanaume hawa wawili walivosimama mbele ya LA LIGA, tena kwa kauli ya pamoja, wanaijua nguvu yao!

Simba akiweka elfu10, Yanga wanapaswa kuweka elfu10! Kaeni kwa kauli moja tu kwenye maslahi yenu, msiishie sifa za full house huko mmeshapita ni tabia za klabu ndogo, ninyi hamna uhasama kuzidi Milan na Inter lakini watazame yanapokuja maslahi, hizi klabu ni utajiri kama Viongozi mkiamua kutoendeshwa na presha za nje, jaribuni tuone.

Screenshot_20230730_075832_Instagram.jpg
 
Huyu ndie Franco, alikuwa na watoto 18, watoto 17 walikuwa wa kike...alizaa na wanawake 14..!

"'Umesikia jinsi anavyokuongelea vibaya kwa watu
Kwanini usitafute kazi yako Mario", hayo ni maneno ya Franco Luambo kwenye wimbo wake wa Mario.

Mario kilikuwa ni kisa cha kweli mwanaume msomi aliyekuwa ana ishi na kulelewa na wanawake huko Ureno.

Unapomtaja Franco hauwezi kuacha kuutaja wimbo wa Mario, unaachaje kuutaja wimbo uliouzwa zaidi ya kopi laki 2. Franco hakuwa Mario, alifanya kazi kwa bidii na kuachia ngoma juu ya ngoma, kuna mwaka mwamba huyu alitoa album 12 karibu kila mwezi alikuwa anatoa album moja.

Mpaka sasa watu wanabishana kuhusu idadi kamili ya album alizotoa Franco, wengi wanasema alitoa albums 85, na wengine wanasema alitoa album 150.

Nyimbo nyingi za Franco zilihusu maisha ya kila siku hasa mapambano ya ukoloni. Jina lake lilikuwa maarufu na kutamkwa na karibu kila mtu katika bara zima la Afrika.

Franco alizaliwa mwaka 1938 huko Kongo enzi za ukoloni wa Wabelgiji. Franco hakuwa msomi sana, aliacha shule akiwa na miaka 10 baada ya baba yake kufariki. Alijifundisha kupiga gitaa na kuanza kulisha familia katika umri huo mdogo.

Alikuwa rafiki mkubwa wa Rais wa Zaire Mobutu, hata hivyo urafiki wao haukudumu sana ukageuka uadui wa paka na panya.

Licha ya uadui wao, baada ya Franco kufariki Mobutu alitangaza siku 4 za maombolezo.

Franco alifariki mwaka 1989, alikuwa na umri wa miaka 51, vyanzo vingi vinasema Franco alifariki kutokana na ugonjwa wa UKIMWI.

Katika uhai wake Franco alibahatika kupata watoto 18, miongoni mwao watoto wakike walikuwa 17 na mmoja wa kiume. Alizaa na wanawake 14...!
Screenshot_20230730_213952_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom