Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mshambuliaji wa Kimataifa wa Senegal Sadio Mane (31) amejiunga na Club ya Al Nassr ya Saudi Arabia kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea FC Bayern Munich ya Ujerumani.

Mane anayeenda kucheza timu moja na Cristiano Ronaldo atakuwa akilipwa mshahara wa pound 650,000/= (Tsh Bilioni 2 kwa wiki).

Toka Ronaldo aende Saudi Arabia Wachezaji wengi wamekimbilia huko akiwemo Roberto Firmino, Riyad Mahrez, Neves, Ng’olo Kante, Mendy, Koulibaly, Karim Benzema na sasa Sadio Mane.
Screenshot_20230802_070049_Instagram.jpg
 
Jeshi la Myanmar limetangaza kupunguza miaka sita kutoka kwenye kifungo cha miaka 30 cha Kiongozi wa Nchi hiyo aliyeondolewa madarakani, Aung San Suu Kyi.

Msemaji wa Jeshi Zaw Min Tun, amesema miaka hiyo imeondolewa katika kifungo chake baada ya tangazo kwamba amesamehewa katika kesi tano zinazomkabili lakini bado Kiongozi huyo wa zamani anakabiliwa na kesi 14 licha ya msamaha huo wa Jeshi, kumekuwa na hofu kuhusiana na hali ya kiafya ya Suu Kyi, wiki iliyopita Jeshi lilimhamisha kutoka Jela na kumpeleka katika jengo la Serikali.

Itakumbukwa mwaka 1991, Aung San Suu Kyi alikabidhiwa tuzo ya amani ya Nobel akiwa chini ya kifungo cha nyumbani na alisifiwa kwa kuwa mfano mzuri wa kutetea wanyonge, mwaka 2015 aliongoza Chama chake cha National League for Demoracy NLD kupata ushindi katika uchaguzi wa wazi uliokuwa na ushindani mkali nchini Myanmar katika kipindi cha miaka 25

Aliwahi kuwekwa kizuizini kwa miaka 15 kati ya mwaka 1989 na 2010 ambapo harakati zake za kuleta Demokrasia katika Taifa hilo ambalo limekuwa likitawaliwa kijeshi zilimfanya kuonekana kama nembo ya kimataifa ya upinzani wa amani wakati wa ukandamizaji.

Licha ya ushindi wake mkubwa mwaka 2015 , katiba ya Myanmar ilimzuia yeye kuwa Rais kwasababu ana Watoto ambao ni wa Mataifa ya kigeni.
Screenshot_20230802_070424_Instagram.jpg
 
Askari wa Uhifadhi, katika Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi, Samwel Edward Nassari amefariki dunia baada ya kugongwa na nyati katika eneo la Mbula lilipo katika hifadhi hiyo, wilayani ya Same, Mkoa wa Kilimanjaro.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamishna Msaidizi Hifadhi ya Mkomazi, Emmanuel Moirana amesema tukio hilo limetokea leo Jumanne Agosti Mosi, 2023 wakati askari huyo akitekeleza majukumu yake.

"Mtumishi mwenzetu amefariki leo baada ya kugongwa na nyati wakati akiwa kwenye majukumu yake ya kazi," amesema Moirana.

Naye Kamishna wa Uhifadhi Tanapa, William Mwakilema ametuma salamu za pole kwa familia, watumishi wote wa Jeshi la Uhifadhi, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia kifo cha askari huyo.

Screenshot_20230802_070548_Instagram.jpg
 
Mary Mushi (30) mkazi wa Kibosho Kirima, Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, ameuawa kwa kukatwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake, kwa kile kilichodaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Tukio hilo litokea usiku wa kuamkia Jumatatu Julai 31, mwaka huu, ambapo inadaiwa kuwa, watu waliofanya unyama huo walimpigia marehemu simu, saa tatu usiku na kisha kuondoka nae, ambapo baada ya mauaji hayo waliutupa mwili wake shambani kwao.

Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, Simon Maigwa leo jumanne Agosti 1,2023, amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo na kueleza kuwa, wanamshikilia mtuhumiwa mmoja, na kwamba uchunguzi unaendelea ili kuwakamata wote waliohusika na tukio hilo.

Kamanda amesema taarifa za awali zinaonyesha kuwa tukio hilo limesababishwa na wivu mapenzi na kwamba uchunguzi bado unaendelea.

“Ni kweli kuna tukio hilo na tunamshikilia mtu mmoja, tunaendelea kufuatilia watu wengine, lakini taarifa za awali zinaonyesha kuna viashiria vya wivu wa mapenzi,” amesema kamanda Maigwa.

Akizungumzia tukio hilo, Rachel Mushi ambaye ni mama wa marehemu, amesema alibaini mtoto wake kuuawa baada ya watoto wa waliokuwa wakipita asubuhi kwenda shule, kuona mwili wake ukiwa umetupwa shambani.

“Watoto wa shule walisema kuna mtu amefia barabarani eneo la shambani, sasa nilipoenda nikakuta ni mwanangu,” amesema.

Screenshot_20230802_070921_Instagram.jpg
 
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akiwahutubia wananchi Katoro na Busanda, Mkoa wa Geita katika mwendelezo wa Operesheni +255 Katiba Mpya, Okoa Bandari Zetu.

Operesheni hiyo ilianzia Bukoba, Mkoani Kagera, Julai 28, 2023 kisha kusambaa mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Katika mkutano wa leo Jumanne, Agosti 1, 2023, Mbowe pamoja na mambo mengine, amewaongoza kupiga kura ya wazi ya kuukataa mkataba wa uwekezaji na uendelezaji wa bandari baina ya Serikali ya Tanzania nay a Dubai.

Mbowe amesema Chadema hawapingi uwekezaji lakini wanachokitaka ni mkataba wenye maslahi ya umma.

Screenshot_20230802_071053_Instagram.jpg
 
Ripoti ya 'Tanzania in figures 2022' inayotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imeonyesha kuwa kiwango cha uzalishaji na unywaji bia kimeongezeka Tanzania hadi kufika lita milioni 456 kwa mwaka 2022 ikilinganishwa na lita milioni 380 mwaka 2021.

Kiwango hicho ni sawa na ongezeko la asilimia 20 kwa kipindi hiko cha mwaka mmoja.
Screenshot_20230802_071206_Instagram.jpg
 
Minza Maduhu (92) Mkazi wa Mtaa wa Mwakibolo, Wilaya ya Bariadi, mkoani Simiyu, ameuawa na kisha kunyofolewa macho na watu wasiojulikana.

Tukio hilo limegunduliwa jana Julai 31, 2023; ambapo mwili wa kikongwe huyo ambaye alikuwa akiishi peke yake, ulipokutwa na mjukuu wake ambaye alikuwa akienda kumhudumia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Edith Swebe, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuahidi kulingumzia zaidi baada ya kupokea taarifa kamili kutoka kwa wasaidizi wake.

"Jeshi la Polisi linaandaa taarifa kamili itakayotolewa kwa vyombo vya habari baadaye," amesema Kamanda Swebe alipoulizwa kuhusu mauaji hayo.

Akisimulia tukio hilo, Anna Maduhu, ambaye ni mjukuu wa kikongwe huyo, amesema alimkuta bibi yake akiwa amelala kitandani huku damu zikiwa zimegandana kichwani.

"Tulikubaliana niwahi kuja asubuhi ili nikasage mahindi, huwa nina kawaida ya kuja, kisha ninamuita dirishani, na yeye ananifungulia mlango alafu ninaendelea na kazi, lakini siku hiyo hakufungua nilipotazama mlangoni ulikuwa umefungwa kwa nje," amesimulia Anna.

Ameongeza kuwa baada ya kufungua mlango aliingia chumbani na kumkuta bibi yake akiwa amelala, aliendelea kumuita bila mafanikio, ndipo alipotumia mwanga wa simu kumulika na kumuona akiwa ameinamisha kichwa uvunguni na damu zikiwa zimeganda kitandani.

Kijana mkubwa wa familia hiyo Gulinja Mahangila amesema baada ya kupata taarifa ya tukio hilo alifika nyumbani kwao na kukuta mwili ukiwa umelala kichwa kikiwa kimeinamia uvunguni.

"Nilipofika nilichungulia mahala kichwa kilipokuwa kimeinamia, ndipo nilipoona damu zimeganda na tundu kwenye eneo la jicho hivyo nikatoa taarifa kwa mwenyekiti wa mtaa," amesema Gulinja.

Akizungumza baada ya kufanya uchunguzi wa mwili Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Bunamhala, Praygod Charles, amesema chanzo cha kifo cha bibi huyo ni kuvuja damu nyingi.

"Mwili wake ulikuwa na jeraha karibu na sikio na macho yote mawili hayakuwepo, baada ya vipimo; mwili umekabidhiwa kwa familia kwa ajili ya taratibu nyingine za maziko," amesema.

Screenshot_20230802_071316_Instagram.jpg
 
Mapacha wa mwaka mmoja wamefariki baada ya nyumba yao kuteketea kwa moto katika Kijiji cha Magulilwa wilayani Iringa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Allan Bukumbi amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo na kwamba wanaendelea na uchunguzi zaidi.

Pacha hao, Eliza na Erick Msigwa walipoteza maisha yao kwa nyakati tofauti ambapo mmoja anadaiwa kupoteza maisha wakati nyumba ikiteketea, na mwingine wakati akikimbizwa hospitalini kwa ajili ya kutibu majereha ya moto.

Watoto hao waliofariki Julai 30, 2023 na wamezikwa jana Julai 31, 2023 kijijini kwao Magulilwa.

Akizungumza na Mwananchi Digital nyumbani kwao, mama wa watoto hao, Warda Msisi amesema kabla ya kufikwa na mauti aliwalaza wanaye ndani ya nyumba hiyo kisha akaenda dukani kununua sabuni.

“Duka lenyewe haliko mbali na sikuchukua muda mrefu, nilipokuwa narudi nilishangaa kuona watu wamekusanyika nyumbani kwangu, nikaona moshi kumbe nyumba inaungua,” amesema na kuongeza;

“Nilishtuka kwa sababu watoto walikuwa ndani lakini nikawa nimechelewa, mmoja alikauka kabisa na mwingine alikuwa bado hai ila naye aliniacha. Sina kingine kinachoniumiza ni hawa watoto tu, sielewi ilikuwaje na sijui chanzo cha moto ni nini hadi sasa.”

Baba wa watoto hao Stanley Msigwa, amesema alipata taarifa za nyumba yake kuungua kwa moto wakati akiendelea na kazi zake za kila siku mbali na nyumbani kwake.

“Kuna watu waliniambia nyumba yangu inaungua lakini nikabisha kwa sababu ni ya bati, niliwaza inaunguaje? Wakasema ni kweli hivyo nikatoka mbio kuja na kuona ni kweli. Kilichoniumiza zaidi ni wanangu, mmoja alipookolewa nilijua anaweza kusalimika lakini naye akafariki,” alisema.
Screenshot_20230802_071419_Instagram.jpg
 
Mwili wa mtu mmoja miongoni mwa watu 13 waliozama ziwa Victoria umepatikana.

Mwili huo ni wa mtoto wa kike, umepatikana na kuletwa nchi kavu leo Jumanne Agosti Mosi saa 7.25 mchana.

Hivi sasa mwili huo unafanyiwa ukaguzi wa kitabibu katika kijiji cha Mchigondo baada ya kukaa majini kwa takribani siku tatu.

Juhudi za kutafuta watu wengine zinaendelea zikihusisha Jeshi la Zimamoto, Polisi Kikosi cha Wanamaji, wavuvi na wenyeji wa eneo hilo.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara, Agostino Magere amesema katika uokoaji huo, jeshi hilo limeleta boti mbili pamoja na askari 22 kutoka Mara na Mwanza.

Aidha, amesema utafutaji wa watu hao unakumbwa na changamoto kadhaa ikiwemo hali mbaya ya hewa, kina kirefu na mkondo wa maji ambao unaweza kuwa chanzo cha watu hao kusombwa na kupelekwa mbali na eneo la tukio.

Mkuu wa Mkoa Mara, Said Mtanda amesema Serikali itagharimia maziko ya watu hao baada ya miili kupatikana.

"Serikali itatoa usafiri kwaajili ya kuwasafirisha wapendwa wetu hadi sehemu ambayo familia itakuwa imeamua lakini pia tutatoa ubani wa Sh1 milioni kwa kila familia," amesema.

Mkuu wa mkoa huyo amesema Serikali ilitamani watu wote waliozama wapatikane wakiwa hai, hata hivyo matumaini hayo yanazidi kufifia, huku akiahidi kuwa Serikali itaendela lufanya kila liwezekanlo ili watu wote waliozama wapatikane.

Tukio la kuzama mitumbwi hiyo limetokea katikati ya ziwa Victoria wakati mitumbwi hiyo iliyokuwa na watu 28 kupigwa dhrouba na kuzama Julai 30 saa 12.30 jioni.

Watu hao ambo wengi wao ni watoto walikuwa wakitoka kwenye ibada katika Kanisa Takatifu la Mungu wa Kiroho (KTMK), katika kijiji cha Mchigondo kueleka kitongoji cha Bulomba kijiji cha Igundu wilayani Bunda.
Screenshot_20230802_071637_Instagram.jpg
 
Leandro Trossard ana matumaini ya kucheza safu ya kiungo mshambuliaji lakini huenda Mikel Arteta asimpange nafasi hiyo anayoipenda msimu utakapoanza. Arenal ipo bize kuhakikisha inampata Mohammed Kudus kutoka Ajax kwa Pauni 40 milioni anayecheza nafasi hiyo, hivyo itakuwa ngumu kwa Trossard.
.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji mara kwa mara alikuwa tishio akitokea benchi lakini Arteta alimpanga nafasi tofauti akiwa na uzi wa Arsenal. Trossard anaweza kucheza winga zote mbili kama mshambuliaji, lakini nyota huyo hakuficha na kudai alijiunga na Arsenal akiwa na matumaini ya kucheza nafasi ya kiungo mshambuliaji.
.
“Najisikia vizuri kucheza nafasi tofauti lakini kama wangeniambia kuchagua nafasi ningechagua kucheza nyuma ya mshambuliaji kwa sababu ndio napamudu zaidi. Lakini itategemea na mfumo wa timu.”
Screenshot_20230802_071833_Instagram.jpg
 
Nyota wa zamani wa Man United, Wayne Rooney alimtaka Mason Greenwood kuhama kutokana na uonevu anaofanyiwa. Rooney amesisitiza Old Trafford hakuna mustakabali wa kueleweka na aanze kutafuta timu mapema kabla ya dirisha la usajili kufungwa.
.
Rooney Bado ana imani kwenye kiwango cha nyota huyo kuwa ana uwezo wa kucheza timu yoyote kubwa na kupata nafasi kikosi cha kwanza kutokana na kasi aliyonayo, umri, na uwezo wakufumania nyavu.
.
Rooney alinukuliwa akisema “Nadhani kilichopo kwa sasa ni Mason kutoka nje ya United na kutafuta changamoto nyingine nje na hapo ili kulinda kipaji chake na kazi yake na siyo kusalia kwenye kikosi ambacho hukitumikii.
Screenshot_20230802_071942_Instagram.jpg
 
Inaelezwa kikao kati ya mabosi wa Bayern Munich na mwenyekiti wa Tottenham Hotspurs kilienda vizuri na kwa sasa vigogo hao wa Munich wanajiandaa kuwasilisha ofa nono ambayo itaenda kuvunja rekodi yao ya usajili na kumfanya Kane kuwa mchezaji ghali zaidi kuwahi kutokea kwenye viunga vya Munich.
.
Taarifa kutoka Sky Sports zinaeleza Munich ipo tayari kutoa Pauni 100 milioni ambayo inahitajika na Spurs ili kuipata huduma ya Kane. Mchezaji ghali zaidi kuwahi kusajiliwa na Bayern hadi sasa ni Lucas Hernandez ambaye zilitumika Pauni 68 milioni kumchukua akitokea Atletico Madrid.
.
Kane ambaye alipewa ofa ya kusaini mkataba mpya wa kuendelea kusalia Spurs kwa kuwa mkataba wake wa sasa unamalizika mwisho wa msimu huu, alikataa na kusisitiza anahitaji kuondoka.
.
Hatma yake inadaiwa kuamuliwa kwenye kikao cha mwisho kilichofanyika jana na inaelezwa Spurs wapo tayari kumuuza lakini sio chini ya pauni 100 milioni.
Screenshot_20230802_072047_Instagram.jpg
 
TOTTENHAM imepanga kutumia pesa ambazo watazipata baada ya kumuuza Harry Kane kwenye usajili wa kiungo wa Barcelona na Ivory Coast, Franck Kessie, 26 na beki wa timu hiyo, Clement Lenglet, 28, ndani ya dirisha hili katika usajili ambao unaweza kuwagharimu zaidi ya Pauni 60 milioni kwa wachezaji wote hao wawili. Mkataba wake unamalizika mwaka 2026.
Screenshot_20230802_072243_Instagram.jpg
 
FISTON MAYELE:

“ Nimeufuatilia usajili wa Yanga ambao wengi wachezaji nawafahamu akiwemo Maxi, ni kiungo mshambuliaji mwenye uwezo mkubwa wa kufunga na kutengeneza nafasi za mabao.”

“Lakini niwaonye kuwa Ligi Kuu ni ngumu, kwani timu nyingi zinaipania Yanga zinapokutana nayo, hivyo ni lazima wawe fiti kwa kufanya mazoezi mengi zaidi,” alisema Mayele ambaye ametimkia Pyramids ya Misri.
Screenshot_20230802_072336_Instagram.jpg
 
Aliyekuwa Mshambuliaji kinara wa Mabingwa wa Soka Tanzania Bara Young Africans, Fiston Kalala Mayele amesema anaamini siku moja atarudi tena kuitumikia timu hiyo kutokana na sapoti na mafanikio makubwa aliyoyapata akiwa na miamba hiyo katika kipindi cha misimu miwili mfululizo.

Mshambuliaji huyo juzi Jumapili (Julai 30) alitambulishwa rasmi kwenye timu yake mpya ya Pyramids FC ambayo amejiunga nayo kwa mkataba wa miaka mitatu, huku Young Africans ikinufaika kwa kubeba kitita cha Sh bilioni 2.8 kutokana na mauzo yake.

Akizungumza akiwa nchini Misri Mshambuliaji huyo alieleza kuwa ameondoka Young Africans kwa nia njema na lengo lake ni kwenye kusaka changamoto mpya kwa ajili ya maisha yake na familia yake.

“Haya ni maamuzi magumu kwangu, uongozi ulipambana kuhakikisha nabaki, tulifanya vikao vingi lakini maamuzi yangu niliamua kuondoka ingawa siyo kwa ubaya nashukuru viongozi wamenielewa na kunikubalia ombi langu naamini ipo siku nitarudi tena Young Africans,” amesema Mayele.

“Rais Hersi amekuwa msaada mkubwa sana kwetu, amekuwa na ukaribu wa hali ya juu kwa timu yake mara kadhaa tumekuwa tukisafiri naye iwe ndani au nje ya nchi, hii imechangia wachezaji kupata hamasa ya kupambana,” amesema Mayele.
Screenshot_20230802_072428_Instagram.jpg
 
Kiungo Mshambuliaji kutoka nchini Zambia na klabu ya Simba SC, Clatous Chama aibuka na kutamka kuwa ujio wa kiungo Willy Onana utaifanya timu hiyo, ifunge mabao mengi katika msimu ujao.

Onana ni kati ya viungo waliosajiliwa na Simba SC kwa ajili ya msimu ujao ambao wamepanga kurejesha makombe yote pamoja na kufika hatua ya Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika.

Akizungumza mjini Ankara-Uturuki, Chama amesema kuwa kwa siku chache ambazo amekaa kambini na Onana ameona ana kitu kikubwa ambacho atakifanya Simba SC msimu ujao 2023/24.

Chama amesema kiungo huyo anaonekana ana uchu wa kufunga mabao muda wote akiwa mazoezini na katika michezo ya kirafiki.

Ameongeza kuwa kikubwa kiungo huyo apewe ushirikiano mzuri kwa mashabiki ambao anaamini ndio watakaomfanya awe bora zaidi.

“Nipongeze usajili ambao umefanywa na viongozi wangu, kiukweli utatupa mafanikio makubwa msimu ujao.

“Nimefurahishwa na ubora wa kila mchezaji uwanjani, kati ya hao yupo Onana ambaye nimemuona anapenda sana kufunga kila anapopata mpira.

“Kikubwa mashabiki wampe muda wa yeye kuonyesha kipaji chake katika msimu katika kufanikisha malengo yetu,” amesema Chama.
Screenshot_20230802_072528_Instagram.jpg
 
Uongozi wa Mabingwa wa Soka Tanzania Bara Young Africans wala hauna presha licha kuondoka Mshambu ya wao tegemeo, Fiston Kalala Mayele, kwani umeweka wazi kuwa mshambuliaji wao Kennedy Musonda anaweza kuwa mfungaji bora wa msimu ujao na atavunja rekodi kibao za washambuliaji waliopita.

Musonda kwa sasa ndiye Mshambuliaji tegemeo ndani ya Young Africans mara baada ya Mayele kuuzwa huku pia wakimshusha Hafizi Konkoni raia wa Ghana kama mbadala wake jambo ambalo mashabiki wengi wamekuwa na hofu kubwa.

Akizungumza jijini Dar es salaam Ally Kamwe ambaye ni Afisa Habari wa Young Africans amesema kuwa: “Watu wanamuona Musonda kama ni mshambuliaji wakawaida sana lakini mimi niwaaambie kuwa yule mtu anajua sana kufunga na anajua sana mpira na msimu ujao watamtambua.

“Sisi wala hatuna presha na Young Africans ya msimu ujao ukiona kuna mtu anaondoka, basi fahamu huyo ambaye anakuja ni moto wa kuotea mbali kuliko hata yule ambaye ameondoka,” amesema kiongozi huyo.
Screenshot_20230802_072623_Instagram.jpg
 
Kocha wa mabingwa wa UEFA CL 2022/23 Pep Guardiola amesema

“Saudi Arabia imebadilisha sana soko ,miezi michache iliyopita wakati Cristiano anaenda Saudia ,hakuna mtu aliyefikiria kuwa wachezaji wengi wa juu wangecheza huko na katika siku zijazo, wengi zaidi wataenda.

Ndio maana vilabu vinahitaji kufahamu kinachoendelea na kujipanga zaidi “
Screenshot_20230802_073006_Instagram.jpg
 
Kocha mkuu wa Atletico Madrid Diego Simeone amenukuliwa akisema haoni cha ajabu ambacho Mbappe atafanya endapo atajiunga na Real Madrid

“Mnataka kusema Mbappe ataifanya Madrid kuwa imara ? sisi tumeshinda ubingwa wa La liga dhidi ya Messi ,Xavi,Sanchez,Bale ,Ronaldo,Benzema ! ongeleeni mpira sio majina”
Screenshot_20230802_073127_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom