Jezi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan imeuzwa kwa Sh. 10,000,000 katika mnada maalum wa kibegi pamoja na jezi zilizopelekwa kileleni mwa Mlima Kilimanjaro uliofanyika katika Ofisi za Azam TV.
Jezi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Philip Mpango imeuzwa kwa TSh. 3,000,000 kwa Sandland Omary 'Sandland The Only One', Jezi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Mwinyi imeuzwa Tsh. 5,000,000 kwa Hasa Clearing and Forwarding.
Jezi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa imeuzwa kwa Sh. 4,000,000 kwa S & Sons LTD na Jezi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Ackson imeuzwa kwa Sh. 2,500,000 kwa Tawi la Simba Makini .
Jezi ya Rais wa Heshima wa klabu, Mohamed Dewji 'Mo' @moodewji imeuzwa Sh. 2,000,000 na Duka la Vifaa la Michezo la Romario Sports na Kibegi kilichokuwa na jezi na kupelekwa juu ya kilele cha Mlima Kilimanjaro kimeuzwa kwa Sh. 2,500,000 kwa Saleh Majapa.
View attachment 2704336