Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mashabiki wa Yanga waanadai kitu pekee ambacho kimesalia kwenye kikosi chao ni kusajiliwa kwa mshambuliaji anayejua kufunga na hilo nalo limeisha baada ya mabosi wao kumshusha kimyakimya mshambuliaji Emmanuel Mahop kutoka Canon Yaounde.
.
Unavyosoma taarifa hili tayari Mahop yupo nchini kuanza maisha mapya Yanga akija kuchukua nafasi ya mfungaji bora, Fiston Mayele anayeondoka zake
.
Rekodi ya Mahop ndiyo iliyowashawishi mabosi wa Yanga kumaliza haraka dili hilo baada ya kufanikiwa kufunga jumla ya mabao 15 katika mechi 20 za Ligi ya Cameroon.
.
Straika huyo anakwenda kufunga usajili kwa wachezaji wa kigeni ambapo tayari Yanga ilibakiza mtu mmoja pekee kufikisha wachezaji 12, ambao wanahitajika kikanuni.
Screenshot_20230726_085845_Instagram.jpg
 
TOTTENHAM Hotspur imekubali kuwapiga bei Davinson Sanchez kwenda Spartak Moscow, imeripotiwa. Klabu hizo mbili zimefikia makubaliano ya ada ya Pauni 13 milioni kwa ajili ya huduma ya beki huyo wa kati.
.
Makubaliano binafsi baina ya mchezaji na Spartak Moscow bado hayajafikiwa, huku Spurs inasikilizia atakachoamua.
.
Sanchez amekuwa kwenye kikosi cha Spurs tangu 2017, aliponaswa kutoka Ajax kwa Pauni 42 milioni. Alicheza mechi 205 katika klabu hiyo na kufunga mabao matano.
Screenshot_20230726_090012_Instagram.jpg
 
IKIWA itafanikiwa kumuuza Kylian Mbappe kwenda Saudi Arabia, PSG itatumia kiasi hicho cha pesa kulipa Pauni 100 milioni na kumsajili straika wa Tottenham, Harry Kane katika dirisha hili licha ya ukweli kwamba akili ya Kane inafikiria kujiunga na Bayern Munich pekee.
.
PSG imekuwa ikitajwa kutaka kumsajili Kane tangu dirisha hili lilipoanza lakini kuna wakati iliachana na mpango huo kutokana na kiasi kikubwa cha pesa kinachohitajika na Spurs ili kumuuza. Ili kumpata mkali huyo wa mabao wa kimataifa wa England, PSG itawahitaji kuweka ofa nono zaidi na kuharakisha mchakato kwani ripoti zinadai Kane yupo kwenye harakati za kutafuta nyumba jijini Munich.
.
Mbali ya Kane, taarifa zinadai kwamba PSG huenda ikatumia pesa hiyo pia kumsajili straika wa Napoli, Victor Osimhen kama mbadala wa staa huyu. Kane ambaye mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu ujao, anataka kuondoka Spurs kwa ajili ya kuchezea timu itakayompa nafasi ya kushinda mataji
Screenshot_20230726_090058_Instagram.jpg
 
Kiungo mkata umeme wa Fiorentina, Sofyan Amrabat, 26, amefikia makubaliano na Manchester United juu ya kutua Old Trafford kwa mkataba wa miaka mitano.
.
Amrabat ambaye alikuwa akihitajika na Barcelona katika dirisha lililopita amezivutia timu nyingi kutokana na kiwango alichoonyesha kwenye Kombe la Dunia mwaka jana na pia kuiongoza timu yake kufika fainali ya Europa Conference League.
Screenshot_20230726_090155_Instagram.jpg
 
PARIS Saint Germain imekubali ofa itakayovunja rekodi ya dunia ya Pauni 259 milioni kutoka Al Hilal kwa ajili ya kumsajili supastaa Kylian Mbappe, imeripotiwa. Imedaiwa klabu hiyo ya Saudi Pro League imempa Mbappe ofa ya mshahara wa Pauni 11.6 milioni (Sh 36.6 Bilioni) kwa wiki.
.
Ofa hiyo ya Al Hilal itapiku ile rekodi ya uhamisho ya Pauni 198 milioni iliyokuwa ikishikiliwa na supastaa Neymar. PSG watapata faida ya Pauni 100 milioni kwenye mauzo hayo ya Mbappe, ambaye wenyewe walimsajili kwa Pauni 162 milioni kutoka Monaco.
.
Baada ya kukubali ofa hiyo, PSG sasa wamewapa ruhusa Al Hilal kuzungumza na mchezaji Mbappe. Kwa ofa hiyo ya Al Hilal ina maana wao wapo tayari kumlipa Mbappe mshahara wa Pauni 604 milioni kwa mwaka mmoja na hapo mkataba wao utakuwa umefika tamati wakimruhusu kwenda bure huko Real Madrid anakotaka kwenda kucheza.
Screenshot_20230726_090255_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom