Farhan Kihamu Jr
MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA, WAINATAKA PEPO HAWATAKI KUFA.
Atatokea Shabiki ghafla tu atahoji ile MOSPORTS kwenye jezi ya Simba imetoka wapi mbona hatujui imekuwaje, ile MO Foundation vipi mbona Tajiri anajaza tu matangazo yake.
Shabiki mwingine atahoji tu ile HAIER kwenye jezi ya Yanga mgongoni imekuwaje, ile GSM FOAM pesa ipo wapi, hitimisho utasikia Tajiri anatupiga sana.
Ni Shabiki huyo huyo atataka Simba imrejeshe Miquissone, atahitaji Yanga ipambane Mayele abaki, itataka Feisal alipwe mafao makubwa anayotaka ama Simba ifike fainali CAF, ni Shabiki huyo huyo bila yeye kutaka kuwa sehemu ya mchakato.
Shabiki huyo huyo atadai elfu 10 ni kubwa sana, lakini atazitaka timu zifike level ya Al Ahly, Mamelodi, Zamalek! Hajali Mashabiki na Wanachama wa Zamalek wanachangia vipi mchakato wa timu zao, hajali kuwa mtoto mdogo Al Ahly analipa karibia 104K ya Uanachama, ambapo hukh kwetu ni kadi za watu wanne.
Hajali kuna Mwachama wa Al Ahly analipa kadi Million 100, ana tiketi ya msimu, jezi zote za klabu na vifaa vyake! Hilo yeye hajali, anataka matunda bila kuwa sehemu ya mchakato, wanataka furaha bila kuwa sehemu ya maumivu,
Mwekezaji hawezi kuumia kirahisi anapohitaji na yeye ajipooze utasikia kelele.
Utasikia uchumi wa nchi zao na wetu sio sawa, haufanani! Basi hili ndio jibu la swali kuwa hatufanikiwi mbele yao kwakuwa wana nguvu kiuchumi, basi tukitolewa huko tusipigizane kelele wala tusiwasumbue Viongozi wa hizi timu kwakuwa tumekubali hatuwawezi na sisi ni Feeder, kila kinachotokea ni fluke! Si ndio maana yake?
Nje na hapo Viingilio vipande, kadi za Wanachama na Mashabiki zigombaniwe kama njugu ili upande huu wa wengi (majority) uongeze kwenye mifuko ya MO na GSM, kama hatutaki wapeni uhuru Matajiri, waweke pesa na waweke chochote wanachotaka ili timu ziendelee kusogea kwakuwa tunaukataa maumivu ya mchakato, tunaitaka pepo ila tunaogopa kufa.
Katazame Real Madrid, Al Ahly, Bayern Munich, Dortmund, Zamalek na timu zingine ambavyo Mashabiki na Wanachama wanazipa faida timu zao, ndio Maboss na wana nguvu sana.