Makapuku Forum

Makapuku Forum

Edo Kumwembe

“Unapoona kina Miquissone wanarudi kutoka Cairo kuja Dar es salaam halafu Samatta anatoka Genk anakwenda Athens basi ujue kazi imefanyika. Kazi ambayo sijawahi kuona mchezaji wa kizawa akiifanya. Kazi ambayo sijawahi kuona hata wageni wanaifanya.
.
Kucheza nje kunahitaji mambo mengi nje ya soka la uwanjani. Nimewahi kumtembelea Samatta mara kadhaa na ukweli ni unahitaji moyo mkubwa kutamba Ulaya katika maisha yale ya baridi na mahitaji makubwa ya utimamu wa mwili na akili. Sio kila mchezaji wa Kitanzania anaweza. Haijalishi una kipaji kiasi gani, ukweli ni kwamba kucheza soka katika kiwango cha Ligi kuu Ulaya unahitaji kujitoa.
.
Lakini haishangazi pia kuona kuna wachezaji ambao hapa wanachukuliwa kama mastaa lakini wakienda nje wanashindwa kutamba. Kuna maeneo ambayo ligi yetu bado ni nyepesi na haina ushindani mkubwa kiasi cha kumwandaa mchezaji wa Tanzania kutamba moja kwa moja mbele ya safari yake.

Kina Clatous Chama walitamba Tanzania kisha wakaenda nje. Mambo yakawa magumu. Waliporudi wameendelea kuwa Wafalme” - Edo Kumwembe [Mwanaspoti]

Screenshot_20230726_051348_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom