Makapuku Forum

Makapuku Forum

Hili ndo likawa PIGO kubwa kwa Yanga. Huwezi amini walihangaika kufukua mafaili ya zamani kupata picha ambazo wao pia walipeleka jezi mlimani. Wakasahau kwamba wao walipeleka jezi, siyo walizindua.
.
Wakasahau kwamba wao wana tamasha linakuja. Wakaacha kucheza ngoma yao, wakaanza kucheza ngoma ya Simba...wakawa wameingia kwenye mtego. Na Simba walivyokuwa makini...wakapeleka kibegi cha jezi mlimani na kuhakikisha kinazungumziwa njia nzima. Matokeo yake safari ya kibegi ikawa kubwa kuliko ya tamasha.
.
Hatimaye kikafika kileleni...jezi zikazinduliwa. Yanga na watu wote wakaanza kuzichambua jezi za Simba...kosa jingine. Tamasha limekaribia lakini hakuna anayelikumbuka sio Ally Kamwene, siyo Priva wala Manyara wote wako bize na jezi za Simba.
.
Kama kuna watu wa kulaumiwa, basi Yanga tujilaumu wenyewe. Hatukuwa na mkakati madhubuti wa kujaza uwanja...na tulizidiwa sana maarifa na wapinzani wetu, Simba. Angalia kilichotokea, tamasha lilipofika, Simba wakakaa kimya...hakuna tweet za Mo wala Barbara. Chama yuko Uturuki. UMAFIA.

Screenshot_20230726_051753_Instagram.jpg
 
Mwekezaji wa Simba naye alicheza sana na akili za Yanga. Alikuja na mkakati wa kutoa matamko yenye utata kupitia mitandao ya kijamii ambayo yaliwasisimua zaidi Yanga na kuwapotezea dira. ‘Nakaribia kukata tamaa’ kilikuwa kifungu cha maneno kilichowashughulisha zaidi Yanga kuliko tamasha lao.

Inajulikana kwamba matatizo ya mmoja ni sherehe kwa mtani mwingine hivyo ilikuwa habari njema kwa Yanga. Lakini hawakuwa makini kubaini kwamba labda ulikuwa mtego. Kabla hawajakaa sawa akaibuka Barbara naye na tweet zake za mafumbo...akapiga mule mule.
.
Yanga wakajikuta wanapata raha kama ya mtumia dawa za kulevya, anastarehe huku anajiangamiza. Siku zinazidi kwenda na tamasha linakaribia...lakini wao hawakushtuka.
Screenshot_20230726_051851_Instagram.jpg
 
Iwe kweli au mtego, sakata la Chama liliwateka watu wa Yanga na kusahau kabisa kwamba wanatakiwa kuhamasisha watu wao kwa ajili ya tamasha. Wasemaji, wahamishaji wao na wale vijana wa mitandao ya kijamii, wote walikuwa ‘bize’ kumzungumzia Chama.
.
Habari zilisema Chama hataki kwenda Uturuki kuungana na wenzake kwa ajili ya maandalizi ya kabla ya msimu hadi aongezewe maslahi. Yanga wakalibeba hilo zima zima na kulifanya ajenda, badala ya kuelekeza nguvu zao kwenye kulitangaza tamasha lao.
Screenshot_20230726_051943_Instagram.jpg
 
STRAIKA wa FC Lupopo, Mtanzania George Mpole anautazamia msimu ujao kufanya makubwa kwenye Ligi Kuu ya Congo, baada ya ligi iliyopita kufutwa, hivyo hakupata muda mzuri wa kucheza kama ilivyokuwa matarajio yake.
.
Tayari Mpole amejiunga na timu na amenieleza kwamba ligi hiyo itaanza mwezi ujao, hivyo anajipanga kuhakikisha anafanya kazi nzuri na anaipeperusha vyema bendara ya Tanzania kwa kuonyesha kiwango cha juu.
Screenshot_20230726_052446_Instagram.jpg
 
Bosi wa Singida Fountain Gate (SFG), Japhet Makau amesema usajili wa Benard Morrison ni suala la muda tu na mashabiki wakae kwa kutulia kwani mambo mazuri yanakuja zaidi msimu huu.
.
Morrison alipewa Thank You na Yanga na inadaiwa tayari amemalizana na SFG kwa ajili ya kuitumikia msimu ujao wa Ligi Kuu na mashindano ya kimataifa ambapo watashiriki Kombe la Shirikisho Afrika.
.
Makau alisema kuwa; “Ishu ya Morrison tusubiri Agosti 2, ambapo tutatambulisha kikosi chetu. Sisi tuna imani nae na atafanya vizuri na atacheza kwa jinsi ambavyo kocha atamtumia, naamini wachezaji tuliowasajili wanaenda kufanya vizuri kwenye timu yetu.”
Screenshot_20230726_052544_Instagram.jpg
 
DROO ya hatua mbili za awali za mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho Afrika msimu ujao, inachezeshwa leo huko Cairo, Misri kuanzia saa 8:00 mchana, lakini kabla hata haijafanyika, CAF, wameibeba Simba katika mambo mawili.
.
Kwanza ni kuiweka katika kundi la timu 10 ambazo zitafuzu moja kwa moja kwenda katika raundi ya kwanza ya mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika bila kucheza raundi ya awali ambapo ikifanya vizuri hapo itatinga hatua ya makundi tofauti na timu nyingine ikiwemo Yanga ambayo itaanza hatua ya awali. Katika chati hiyo, Simba inashika nafasi ya sita ikiwa na pointi 35, huku inayoongoza ikiwa ni Al Ahly ambayo ina pointi 83.
.
Wakati Simba ikitinga moja kwa moja katika raundi ya kwanza, watani wao Yanga wataanzia katika raundi ya awali ambayo watapangwa kucheza na vibonde wengine kati ya timu 43 ambao nao wataanzia katika hatua hiyo. Ukiodoa kutinga moja kwa moja katika raundi ya kwanza, Simba imepiga bao lingine la kisigino ambalo ni lile la kuanza kwa kucheza ugenini katika hatua hiyo kisha kumalizia nyumbani.
Screenshot_20230726_052742_Instagram.jpg
 
Simba imesajili kipa Mbrazil Jefferson Luis akitokea Resende ya nchini kwao akitarajiwa kuwa namba moja au mshindani mkubwa wa Aishi Manula.
.
Usajili wa Jefferson umezua maswali kutokana na daraja alilotoka lakini hii ni sababu itakayomfanya acheze Simba. Jefferson atapata vibali vya kucheza nchini kutokana na Brazil kuwepo na mfumo wa ligi kuchezwa kwa majimbo na yeye kutokea Resende timu inayoshiriki Daraja la Kwanza ya jimbo la Rio de Janeiro, ambayo ni miongoni mwa ligi za madaraja matatu ya juu nchini humo.
Screenshot_20230726_052929_Instagram.jpg
 
STRAIKA wa Atalanta, Rasmus Hojlund, 20, anadaiwa kuwaambia watu wake wa karibu kwamba kabla ya mwezi huu kumalizika atakuwa amekamilisha dili la kujiunga na Manchester United.
.
Rasmus ambaye ameshafanya makubaliano binafsi na Manchester United, dili lake limekuwa likicheleweshwa na kiasi kikubwa cha pesa kinachohitajika na Atalanta ambao wanahitaji zaidi ya Pauni 70 milioni ili kumuachia mdun-guaji huyo aende Old Trafford
Screenshot_20230726_053036_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom