Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20230708_053053_Instagram.jpg
 
Usiniite Mfalme, Niite Daudi (Kisa cha Daudi na Mke wa Uria)-2

Tulipoishia.. Bethsheba Mke wa Uria anampa taarifa kwamba mwezi huu hajaona siku zake...!

Endelea...

“Usihofu mama, mimi ndie Mfalme wa Israel na vyote vilivyomo hakuna mtu yoyote aliyeko juu yangu. Kama niliweza kumuuwa Goliath kwa mkono wangu, sina wa kumuogopa” Daudi alisema huku anamvuta Bethsheba kifuani kwake.
“Sawa Daudi, nakuamini mpenzi” Bethsheba aliyaongea kwa sauti ya chini kama ananong'ona

Mapenzi yalimnogea Daudi kuliko Israel yenyewe. Daudi alikuwa hasikii lolote kwa penzi tamu la mke wa mtu. Alikuwa hakumbuki tena zile amri za Musa. Wala haikuimbuki ile amri inayokataza kuzini wala ile inayokataza kumtamani mke mtu.

Bethsheba pia alikuwa amenogewa na penzi la Mfalme. Ni mwanamke gani asiye utamani Umalikia. Ni nani? Ndivyo ilivyokuwa kwa mke wa Uria.

Usiku baada ya mke wa Uria kuondoka. Daudi alikwenda kulala. Alishtuka kutoka usingizini huku mapigo ya moyo yakienda mbio. Aliamka na kukaa kitandani huku anageuka geuka
kwa hofu kubwa. Ndoto ndio iliyo muogopesha.

Daudi aliota kuwa alikuwa porini anawinda. Ghafla Simba akatokea akaupiga mkuki wake ukadondoka chini, Daudi akakimbia lakini Simba akayavuta mavazi yake. Mavazi ya kifalme yakamvuka. Daudi akabaki uchi.

Daudi hakujua maana ya hii ndoto. Lakini akahisi ina uhusiano na kitendo chake cha kulala na mke wa mtu.

Daudi akaamka, akamuita mpambe wake.
“Hakikisha barua hii inamfikia Yoabu kabla jua halijachomoza” Daudi alimwambia yule mpambe huku anamkabidhi barua

Yoabu ndie alikuwa kamanda wa kile kikosi cha maaskari hodari wa Daudi. Wakati huu alikuwa vitani tena vita ilikuwa imepamba moto.

Saa tatu asubuhi ujumbe ule ulimfikia Yoabu. Yoabu aliusoma. Ulikuwa ujumbe mfupi sana kuliko ujumbe wowote aliowahi kuupokea kutoka kwa Mfalme Daudi.
Ujumbe ulisomeka hivi:
“KABLA JUA HALIJAZAMA, URIA MHITI AWE AMEFIKA KWENYE MAKAZI YANGU”

Yoabu alimwita Uria na kumwambia “Uria unaitwa na Mfalme haraka sana”

Uria aliondoka kurudi Jerusalem huku akiwa na kikundi kingine cha watu kumi wa kumlinda. Yoabu asingeweza kumuacha aende mwenyewe. Asingefika je. Hasira ya Mfalme Daudi angeibabaje.

Itaendelea...
Screenshot_20230708_132900_Instagram.jpg
 
'Ukijaribu kujiua usipokufa nitakunyonga'- Kiduku..!

Rais na mtawala mkuu wa Korea Kaskazini Kim Jong-un amewaonya raia wa nchi hiyo kuacha mara moja tabia ya kujiua kwa sababu kufanya hivyo ni uhaini dhidi ya ujamaa. Rais huyo ambaye nchi za Magharibi zimekuwa zikimwita ni dikteta amewaambia raia wa nchi hiyo kwamba iwapo mtu atajaribu kujiua lakini hatokufa basi atanyongwa hadharani..!
Screenshot_20230708_133219_Instagram.jpg
 
Amehukumiwa kifungo cha maisha jela mara 90..!

Mahakama nchni Marekani imemhukumu Patrick Crusius kifungo cha maisha jela mara 90 baada ya kutiwa hatiani kwa mauaji ya watu 23.

Mwaka 2019 Patrick alivamia supermarket ya Walmart na kushambulia watu waliokuwa wanafanya shopping na kuuwa watu 23 na wengine 36 kujeruhiwa.

Patrick alikuwa analenga hasa watu wenye asili ya Kilatino. Hukumu hiyo inamaanisha kwamba Patrick atatoka gerezani siku akiwa kwenye jeneza. Kwa sasa Patrick ana umri wa miaka 24....!!
Screenshot_20230708_133349_Instagram.jpg
 
'Ukijaribu kujiua usipokufa nitakunyonga'- Kiduku..!

Rais na mtawala mkuu wa Korea Kaskazini Kim Jong-un amewaonya raia wa nchi hiyo kuacha mara moja tabia ya kujiua kwa sababu kufanya hivyo ni uhaini dhidi ya ujamaa. Rais huyo ambaye nchi za Magharibi zimekuwa zikimwita ni dikteta amewaambia raia wa nchi hiyo kwamba iwapo mtu atajaribu kujiua lakini hatokufa basi atanyongwa hadharani..!View attachment 2681918

Tobaaa
 
CONFIRMED: Uongozi wa Simba umefikia makubaliano ya kumtoa kwa mkopo beki wa kati Joash Onyango kwenda klabu ya Singida Fountain Gate hadi mwisho wa msimu wa 2023/24.

Onyango amebakiza mkataba wa mwaka mmoja ndani ya Simba SC.
Screenshot_20230708_145420_Instagram.jpg
 
Timu ya Kagera Sugar imeanza mazungumzo na beki wa Ihefu, Juma Nyosso (39) ili akaitumikie msimu ujao. Nyota huyo aliyewika na timu mbalimbali zikiwemo za Simba, Geita Gold na Mbeya City anahitajika kurudi kwenye timu hiyo ambayo awali aliwahi kuitumikia kwa mafanikio makubwa kati ya 2017 hadi 2020.
.
Hatua hiyo ya Kagera Sugar, inajiri baada ya viongozi wa Ihefu kuonekana wazi kutokuwa na mipango na beki huyo anayetumia nguvu na akili kuwadhibiti washambuliaji.
Screenshot_20230708_145526_Instagram.jpg
 
CORAZONE KUTIMKIA BURUNDI
.
Kiungo wa Simba Queens, Corazone Aquino inaelezwa yupo mbioni kutua Buja Queens ya Burundi inayojiandaa na michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati mwezi ujao. Nyota huyo wa Harambee Starlets, timu ya taifa ya Kenya ameonekana akifanya mazoezi na timu hiyo.

Screenshot_20230708_145637_Instagram.jpg
 
ABDI BANDA:
.
“Sijaweza kukubaliana nao kwa sababu hatujadiliana sasa baada ya kuona wanaleta mambo ambayo sijakubaliana nayo, niliamua kufungua kesi FIFA ili nikapate haki yangu,” alisema.
.
Aidha Banda aliongeza bado ana mkataba wa mwaka mmoja uliobaki na klabu hiyo na wakati kesi hiyo ikienda kusikilizwa atarudi Afrika Kusini kutafuta timu kabla ya maamuzi hayo.
.
Katika barua ya FIFA iliyotolewa kuhusu sakata hilo, Chippa imetakiwa kuwasilisha utetezi wao kuhusu kesi hiyo Julai 18 huku hukumu ikitarajiwa kutolewa rasmi Septemba 18 mwaka huu.
.
Ikiwa Banda atashinda kesi hiyo inayosimamiwa na mwanasheria wake, Lyrique de Plessis raia wa Ungereza basi Chippa itabidi imlipe fidia ya Randi 4.5 milioni ambazo ni Sh 572 milioni.
Screenshot_20230708_145859_Instagram.jpg
 
Sports Arena

Kocha Mkuu wa Yanga, Miguel Gamondi ametua nchini usiku wa kuamkia leo, lakini kitu ambacho mashabiki wanapaswa kukijua ni kwamba beki wa kulia Djuma Shabani huenda muda wowote akapewa Thank You ili kupisha jembe jipya Jangwani.
.
Chanzo changu cha kuaminika kutoka ndani ya Yanga kinasema kuna asilimia kubwa Djuma Shabani kwenda maji na inatajwa kinachomponza ni kudaiwa ni mmoja ya wachezaji waliokuwa wakiendesha migomo ya chini chini, huku mwingine akitajwa Yannick Bangala.
Screenshot_20230708_150043_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom