Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,971
STAA wa Arsenal, Gabriel Jesus alifanya uamuzi wa kuachana na Manchester City baada ya kocha Pep Guardiola kumfanya amwage machozi kwa kilio.
.
“Kulikuwa na mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, PSG nyumbani, na hapo Oleksandr Zinchenko alichezeshwa Namba 9. Vitu vya ajabu sana. Siku moja kabla, wala hakumtumia Zinchenko mazoezini, aliniweka mimi kama straika. Zinchenko alithubutu hata kunikejeli, kwamba ile siku alijisikia vibaya kwa ajili yangu.
.
“Saa mbili kabla ya mechi, kwenye mazungumzo ya timu, muda wakula. Alituambia timu itakavyokuwa, sikula,” alisema Jesus. “Nilikwenda moja kwa moja vyumbani na kuanza kulia, nilimpigia simu mama yangu na kumwambia: ‘Nataka kuondoka.’ Narudi nyumbani kwa sababu amemtumia Zinchenko si mimi, amemtumia beki wa kushoto kwenye fowadi. Nilivurugwa.
.
“Nilikuwa na mambo mengi sana na Guardiola na sio rahisi. Magumu sana. Sitaki kusema zaidi.” Jesus alielezea licha ya kutokea benchi na kuonyesha kiwango bora ikiwamo kufunga bao la ushindi, lakini bado alitupwa benchi kwenye mechi iliyofuatia dhidi ya RB Leipzig.
.
“Kulikuwa na mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, PSG nyumbani, na hapo Oleksandr Zinchenko alichezeshwa Namba 9. Vitu vya ajabu sana. Siku moja kabla, wala hakumtumia Zinchenko mazoezini, aliniweka mimi kama straika. Zinchenko alithubutu hata kunikejeli, kwamba ile siku alijisikia vibaya kwa ajili yangu.
.
“Saa mbili kabla ya mechi, kwenye mazungumzo ya timu, muda wakula. Alituambia timu itakavyokuwa, sikula,” alisema Jesus. “Nilikwenda moja kwa moja vyumbani na kuanza kulia, nilimpigia simu mama yangu na kumwambia: ‘Nataka kuondoka.’ Narudi nyumbani kwa sababu amemtumia Zinchenko si mimi, amemtumia beki wa kushoto kwenye fowadi. Nilivurugwa.
.
“Nilikuwa na mambo mengi sana na Guardiola na sio rahisi. Magumu sana. Sitaki kusema zaidi.” Jesus alielezea licha ya kutokea benchi na kuonyesha kiwango bora ikiwamo kufunga bao la ushindi, lakini bado alitupwa benchi kwenye mechi iliyofuatia dhidi ya RB Leipzig.