Makapuku Forum

Makapuku Forum

WAKATI mashabiki wa Kaizer Chiefs ya Sauzi wakiujia juu uongozi wa klabu hiyo kwa kumteua kocha mzawa, Molefi Ntseki, aliyekuwa Kocha wa Yanga, Nasreddine Nabi amefunguka kilichomzuia asitue kwenye timu hiyo aliyokuwa kwenye mazungumzo nayo tangu aage Jangwani.
.
“Niliwaambia siwezi kukubaliana na maamuzi yao, kwani nilitaka wanipe nafasi ya kwenda angalau na wasaidizi wangu wawili muhimu ambao naamini watanisaidia ninavyotaka,” alisema Nabi na kuongeza;
.
“Niliona kuna ugumu hasa waliponiambia wapo watu pale wenye mikataba nao na kuivunja ni gharama kubwa, nikaona hawataweza kunisaidia nikaachana nao.”
Screenshot_20230707_152153_Instagram.jpg
 
YANGA watampokea Kocha wao Mkuu Miguel Gamondi leo Ijumaa atakayewasili nchini kuja kuanza kazi rasmi, lakini taarifa kutoka ndani ya Yanga zinaeleza Kocha huyo anashuka na majina ya baadhi ya mastaa anaotaka kuwakata katika kikosi hicho akizingatia haswa suala la umri.
Screenshot_20230707_152311_Instagram.jpg
 
INTER Miami imeanza mchakato wa kutaka kumsajili staa wa zamani wa Chelsea, Eden Hazard ambaye kwa sasa yupo huru baada ya kuachana na Real Madrid katika dirisha hili. Hazard alikuwa akihusishwa kuwa kwenye mpango wa kurudi nyumbani kwao Ubelgiji lakini ofa ya Miami huenda ikamshawishi na kubadilisha kabisa mawazo yake hayo.
Screenshot_20230707_152408_Instagram.jpg
 
CHELSEA imeanza mazungumzo na wakala wa mshambuliaji wa AS Roma, Paulo Dybala, ili kuipata huduma yake katika dirisha hili. Benchi la ufundi la Chelsea limevutiwa na kiwango cha staa huyu wa kimataifa wa Argentina alichokionyesha kwa msimu uliopita hadi akaiwezesha Roma kufika fainali ya Europa League.
.
Mkataba nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 unatarajiwa kumalizika mwaka 2025.
Screenshot_20230707_152511_Instagram.jpg
 
DECLAN Rice huenda akaenda kubadilishiwa nafasi yake ya kucheza ndani ya uwanja na Kocha Mikel Arteta. Staa huyo atakayetua Emirates kwa ada ya Pauni 105 milioni anapewa nafasi kubwa ya kwenda kuipa nguvu kubwa Arsenal katika mbio za kunasa ubingwa wa Ligi Kuu England.
.
Alipokuwa West Ham, Rice alikuwa akicheza kwenye kiungo cha wachezaji wawili, akisimama mbele ya mabeki wa kati, lakini huko Arsenal, atakwenda kucheza upande wa kushoto kwenye safu ya viungo watatu, nafasi ambayo alikuwa akicheza Xhaka.
.
Majukumu hayo mapya yatamshuhudia Rice, 24, akienda kucheza Namba 8 badala ya Namba 6, mahali ambako alitumika kwenye sehemu kubwa ya maisha yake ya soka. Rice anatazamiwa kushiriki zaidi kushambulia akitokea nyuma. Arsenal imepania kuwa tishio kwenye Ligi Kuu England msimu ujao ikiwa ishamnasa tayari Kai Havertz kutoka Chelsea na imefikia makubaliano ya kumsajili beki wa Kidachi Jurrien Timber kutoka Ajax.
Screenshot_20230707_152603_Instagram.jpg
 
Kocha Erik ten Hag amemwambia Mason Mount, 24, anamtaka awe mchezaji muhimu kwenye kikosi cha Manchester United. Kiungo mshambuliaji huyo wa kimataifa wa England alisaini mkataba wa miaka mitano kwenye kikosi hicho cha Man United akitokea Chelsea.
.
Na sasa imethibitishwa, Ten Hag amemweka Mount kwenye orodha ya wachezaji muhimu kwenye kikosi chake, alipomwambia: “Nataka uwe mchezaji muhimu kwenye timu.” Katika majibu, Mount alionekana kuwa tayari wakati aliposema: “Sawa bosi, asante. Nipo tayari.”
.
Mount atakwenda kuongeza mabao na asisti kwenye kiungo ya Man United, baada ya kufunga mara 58 na kuasisti 53 katika mechi 279 alizochezea klabu yake iliyopita.
.
Kuna matumaini makubwa Mount atakwenda kufanikiwa Man United ambako amekabidhiwa jezi Namba 7.Jezi hiyo iliwahi kuvaliwa na magwiji kama David Beckham, Bryan Robson, Eric Cantona, Cristiano Ronaldo na George Best.
Screenshot_20230707_152653_Instagram.jpg
 
Wakati huu klabu kubwa barani Ulaya zikipambana kunasa saini za mastaa wapya, tena kwa pesa ndefu ni mahali gani watapigwa za kichwa kama ilivyowahi kutokea huko na kuhesabika kama usajili wa hovyo kabisa kuwahi kufanyika?
.
Usajili wa beki Harry MAGUIRE kutoka Leicester City kwenda Man United kwa ada ya Pauni 80 milioni mwaka 2019, ulipigiwa kura na kuchaguliwa kuwa uhamisho wa hovyo zaidi kuwahi kutokea kwenye soka. Uhamisho wa Paul POGBA kurudi Man United akitokea Juventus kwa ada ya Pauni 89.3 milioni mwaka 2016 ulitajwa kushika namba mbili, wakati ule wa Liverpool walipomnasa Andy CARROLL kutoka Newcastle United kwa Pauni 35 milioni mwaka 2011 umeshika namba tatu kwenye kura za usajili wa hovyo kwenye soka.
.
Usajili mwingine wa hovyo ni ule wa Ali Dia alipojiunga na Southampton mwaka 1996 baada ya mtu mmoja kudai ni mchezaji bora wa dunia wa zamani, George Weah, hivyo Kocha Graeme Souness alishawishika na kumsajili. Usajili wa Eden Hazard wa Pauni 150 milioni kwenda Real Madrid mwaka 2019 na ule wa Chelsea ilipolipa Pauni 15 milioni kumsajili Adrian Mutu mwaka 2003 ambaye baadaye ilimwondoa baada ya kufeli kwenye vipimo vya matumizi ya dawa zinazopigwa marufuku michezoni, nao pia wamo kwenye orodha.
.
Fernando Torres kwenda Chelsea, Angel di Maria kwenda Man United na Joey Barton kwenda Rangers nao umeingia kwenye 10 bora ya usajili wa hovyo kuwahi kutokea kwenye mchezo wa soka, huku kukiwa na dili nyingine zilizofanikiwa, lakini iliyoshika namba moja ni ile ya Erling Haaland kwenda kujiunga na Manchester City kwa ada ya Pauni 51.2 milioni.
Screenshot_20230707_152745_Instagram.jpg
 
Rais wa Paris Saint-Germain, Nasser Al-Khelaifi amevunja ukimya kuhusu Kylian Mbappe. Bosi huyo ametuma meseji kali kwa mshambuliaji huyo anayegomea kusaini dili jipya.
.
Hatma ya maisha ya Mbappe imekuwa kwenye hali ya sintofahamu baada ya kufichua kwamba hataendelea kubaki kwenye timu hiyo kwa zaidi ya msimu wa 2023-24. Msimamo wake unaifanya PSG kuwa kwenye hatari ya kumpoteza bure itakapofika 2024 kama haitakuwa imempiga. Kitendo cha klabu hiyo kutaka Pauni 250 milioni kwenye mauzo ya Mbappe yamezifanya timu nyingi kurudi nyuma, lakini Al-Khelaifi alisema kwa msisitizo mchezaji huyo hawezi kuondoka bure.
.
Al-Khelaifi alisema: “Ni wazi hatutaki aondoke bure 2024. Msimamo wetu upo wazi. Kama Kylian anataka abaki, basi tunataka abaki. Lakini, hapo atahitajika kusaini mkataba mpya. Hatutaki kumpoteza bure mchezaji bora duniani, haiwezekani.” Al-Khelaifi aliongeza: “Mbappe alisema hawezi kuondoka bure. Kama amebadili mawazo, hilo sio kosa langu.”
.
Manchester United imeelezwa kuingia kwenye mbio za kumsajili Mbappe baada ya kuachana na Harry Kane.
Screenshot_20230707_152840_Instagram.jpg
 
Mashabiki wa Benfica walijitokeza kwa wingi kumpokea kwa mara nyingine kijana wao Angel Di Maria baada ya miaka 13

Kabla ya kuondoka Angel Di Maria alifunga mabao 15 ,Assist 28 na kushinda Mataji Matatu (3) akiwa Benfica.
Screenshot_20230707_153054_Instagram.jpg
 
TETESI;
Klabu ya Simba imekubali kutoa milion 600 kwa ajili ya kumnasa Mshambuliaji Fiston Mayele huku wakiandaa kitita cha sh. Milion 40 kama mshahara kwa mwezi .

Mpaka sasa Yanga wamempa ofa ya sh.milion 35 kama Mshahara na milion 150 kama nyongeza ya kuongeza mkataba mwingine.
Screenshot_20230708_050529_Instagram.jpg
 
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam, Abdulkarim Amin ‘Popat’ amekiri kuona taarifa hiyo ya klabu ya Goree, lakini amesema suala hilo litamalizwa na hakuna kitakachotibua dili la Allasane Diao kuichezea Azam msimu ujao.
.
Hata hivyo taarifa za ndani nyota huyo aliwaambia mabosi wa Azam hana mkataba alikotoka jambo lililowafanya asainishwe miaka miwili. Diao ni nyota wa nne wa Azam baada ya Feisal Salum ‘Fei Toto’, Gibril Sillah na Cheikh Sidibe.
Screenshot_20230708_050806_Instagram.jpg
 
ARSENAL katika dirisha la hili la majira ya Kiangazi 2023:

Vyuma vilivyoingia:
Leandro Trossard
Jakub Kiwior
Jorginho
Kai Havertz
Declan Rice
Jurrien Timber

Vyuma vilivyobakizwa:
Gabriel Martinelli
Aaron Ramsdale
Bukayo Saka
Reiss Nelson
William Saliba
Screenshot_20230708_051027_Instagram.jpg
 
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro @julius_mtatiro amevunja ndoa ya kinyemela ya kimila iliyokuwa imefungwa baina ya Muddy Muuza urembo wa Tunduru Mjini na Binti aliyechaguliwa kujiunga na elimu ya kidato cha tano katika Shule ya Wasichana ya Masasi.

DC Mtatiro ameongoza Vyombo vya Usalama kuwakamata Wazazi waliomuozesha Binti huyo pamoja na Washenga waliohusika na akafanikiwa kumtia mbaroni Mtuhumiwa Muddy saa 6 usiku wa kuamkia leo akiwa anaishi na Binti huyu wa Shule kinyumba kwenye Kijiji cha Muungano, Tunduru Mjini.

Mzazi wa Binti huyo amekiri kumuozesha Binti huyo kwa mahari ya shilingi 30,000 kwa madai kuwa Binti hakuwa tayari kuendelea na kidato cha tano lakini DC Mtatiro alivyomuhoji Binti huyo alikiri kutaka na kupenda kuendelea na masomo yake ikiwa atapewa nafasi hiyo.

Mtatiro ameahidi kuwa Binti huyo atasimamiwa aendelee na masomo yake na kuendeleza ndoto yake na amewaasa Wazazi wa Tunduru kuachana na mambo ya zamani ya kuoza Mabinti ambao wana nafasi ya kuwa na mchango mkubwa zaidi kwa Taifa

Watuhumiwa watano kwa ujumla wanashikiliwa na Polisi Tunduru wakiendelea kuhojiwa juu ya kula njama na kumuozesha Binti huyo.
Screenshot_20230708_051239_Instagram.jpg
 
Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) kwa kushirikiana na Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja Zanzibar zimeendesha kambi maalum ya upasuaji wa kupandikiza goti na nyonga bandia ambapo zaidi ya Wagonjwa 16 wamefanyiwa upasuaji katika kpindi cha siku tano.

Kambi hiyo imefanyika ikiwa ni muendelezo wa ushirikiano kati ya Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja na Taasisi ya MOI wenye lengo la kusogeza huduma za kibingwa na kibobezi karibu na Wananchi.

Waziri wa Afya Zanzibar, Nassor Marzui amesema kambi hii ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dkt. Hussein Ally Mwinyi la kuhakikisga Wananchi wanapata huduma za kibingwa na kibobezi bila kulazimika kuzifuata huduma hizo Dar es Salaam au nje ya nchi.

“Leo ni siku ya pekee kwani tumekutana hapa kueleza matunda ya ushirikiano kati ya Hospitali yetu ya Manzi Mmoja na Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili-MOI, kama mnavyofahamu mwezi novemba mwaka jana ushirikiano huu ulianza na leo tunashuhudia matunda yake ambapo Mdaktari bingwa na Wauguzi kutoka MOI wamekuja hapa Zanzibar kuwahudumia wananchi wetu”
Screenshot_20230708_051344_Instagram.jpg
 
Alex Saleh Mgonja (11) mwanafunzi wa darasa la tano katika Shule ya Msingi ya Mother Kelvin Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro anadaiwa kufariki dunia baada ya kujinyonga kwa kile kinachodaiwa ni katazo la kupanda gari la shule.

Mwanafunzi huyo alikutwa amejinyonga kwa kutumia kitenge cha bibi yake huku kifo chake kikitajwa kuwa na utata kwa taarifa zinazodai kuwa huenda uamuzi huo umetokana na uwepo wa katazo la kutopanda gari la shule endapo hatalipa ada.

Hata hivyo, mwanafunzi huyo ambaye ni mkazi wa Kitongoji cha Majengo, Kata ya Stesheni hakwenda shuleni siku ya Julai 5 baada ya kuambiwa kuwa hataruhisiwa kupanda gari kutokana na hajalipa ada ya muhula wa pili wa masomo.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni amesema tukio hilo limewasikitisha huku akitaka wazazi kuwa karibu na watoto wao na sio kuwaachia ndugu wengine kuwalea.

"Ni kweli kuna mtoto wa darasa la tano alikuwa anadaiwa ada shuleni, kwa hiyo akawa amemwambia mzazi wake kwamba anaomba apewe ada ili apeleke shuleni lakini mama yake alimwambia asubiri baada ya muda flani atapata hizo fedha na atalipa ada,"

Amesema mtoto huyo alikuwa haishi na wazazi wake tangu utotoni na kwamba alikuwa akiishi na bibi yake mzaa baba siku zote.

"Sasa huyu mtoto huku Same anakaa na bibi yake na hizi fedha za ada inaonekana huyu mzazi wake yuko nje ya Same sasa sijajua kulitokea malumbano au ilikuwaje, lakini huyu mtoto alikuwa akimwambia dada yake wa kazi atajinyonga hivyo hiyo siku alipata sehemu ya kujinyongea akawa amejinyonga,"

Screenshot_20230708_051524_Instagram.jpg
 
Paroko wa Parokia ya Jina Takatifu la Yesu Bukombe Padre Fabian Bundala amefariki kwa ajali baada ya gari yake ndogo kugongana na basi la Happy Nation maeneo ya Ushirombo wilayani Bukombe saa sita usiku wa Julai 6. 2023.

Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi imeeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni umakini mdogo wa dereva wa gari dogo.

Akizungumza na Mwananchi jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Kamishina Msaidizi wa Polisi ACP, Safia Jongo alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo majira ya saa sita usiku.

“Ajali ilitokea maeneo ya Ushirombo na kosa ni la dereva Padri aliyekuwa akiendesha gari dogo namba T575 CBC aliingia barabarani bila kuchukua tahadhari na kukutana na basi la Happy Nation iliyokuwa barabara kuu ndipo ajali ikatokea.

“Majeruhi kwa hali ya nje alipata majeraha ya kawaida lakini inaonyesha alipata majeraha ya ndani ambayo hayakuonekana,” amesema RPC Jongo.

Taarifa iliyotolewa kwa niaba ya Askofu wa Jimbo Katoliki Kahama Mhashamu Christopher Ndizeye, Katibu Jimbo Katoliki Kahama, Padre Abraham Maziku alisema Padre huyo alifariki dunia akiwa njiani kupelekwa hospitalini.

“Padre Fabian Bundala aliyekuwa Paroko wa Parokia ya Jina Takatifu la Yesu Bukombe na Gambera wa Seminari ndogo Malkia wa Mitume – Ushirombo alifariki dunia akiwa njiani kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, kutokea Hospitali ya Wilaya ya Bukombe iliyopo Ushirombo alikopewa matibabu ya awali,” amesema.

Alisema mara baada ya kufika maeneo ya Geita hali ilibadilika ghafla na kulazimika kuomba msaada wa kitabibu Hospitali ya Geita na wakati madaktari wakihangaika kuokoa maisha yake, alifariki.

“Tuupokee msiba huu kwa Imani kuu, tukimwombea huruma ya Mungu na msamaha wa dhambi zake, apumzike kwa amani,” amesema.

Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Gervas Nyaisonga alisema, “Tumepata taarifa na kama ilivyo desturi tumetuma pole kwa Askofu Ndizeye kwa maana yeye ndiye mfiwa kutokana na taratibu za kanisa. Mpaka sasa bado kamati yake bado hajatoa taarifa kwahiyo tunasubiri kutoka huko na ndipo tutajua taratibu zinakwendaje.”
Screenshot_20230708_051652_Instagram.jpg
 
Waziri Mteule wa Fedha Dk Mwigulu Nchemba amerejesha matumaini ya wananchi wa Kipunguni jijini Dar es Salaam ambao kwa takribani miaka 26 ( toka 1997) walisubiri ili wafanyiwe tathmini na kulipwa fidia, zoezi ambalo limekuwa na mchakato mrefu na kuhusisha viongozi mbalimbali bila mafanikio.

Matumaini hayo yamerejeshwa leo Juli 7, 2023 na waziri huyo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kipunguni kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Bibi Jela Jijini Dar es Salaam.

“Kupitia Serikali ya awamu ya Sita inayo ongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan, mchakato wa tathmini ulifanyika na kiasi cha Sh149 bilioni zimetengwa kwa ajili ya ulipaji fidia,” amesema Dk Mwigulu na kuongeza;
“Kutokana na kuanza utekelezaji wa Bajeti mpya ambayo ilisomwa hivi karibuni na taratibu zingine maana fedha hizi si haba ni nyingi, zoezi la ulipaji fidia litaanza mwezi wa tisa mwaka huu.”

“Naelewa tabu mnayopata na ndiyo maana kila siku napambana juu ya jambo hili nami siku zote nimekuwa nikisimama na nyinyi, tumeweza kusubiri kwa miaka hiyo tushindwe kuwa na subiri ya miezi miwili? Naombeni sana subira zenu nami sitawaangusha,” amesema Mwigulu.

Screenshot_20230708_051801_Instagram.jpg
 
Wafuasi wa Kiongozi wa upinzani nchini humo, Laila Odinga wamejikuta katika wakati mgumu baada ya maandamano yao kupigwa mabomu ya machozi huku baadhi yao wakikamatwa na Polisi katika maeneo mbalimbali nchini Kenya.

Polisi huko Nyahururu walimkamata aliyekuwa Gavana wa Laikipia, Ndiritu Muriithi na mwanasiasa wa Jubilee Carolyne Mwendia kwa madai ya kushiriki maandamano haramu.

Mapema asubuhi ya leo, baadhi ya waandamanaji waliifunga barabara kuu ya Thika na kufanya isipitike baada ya kuziba sehemu za barabara katika hoteli moja ya kitalii kwa kuwasha moto, japo baadaye waandamanaji hao walitawanywa na barabara kufunguliwa.

Mjini Mombasa, polisi walirusha mabomu ya machozi kuwatawanya mamia ya wafuasi wa upinzani walioandaa maandamano katika barabara ya Moi Avenue.

Seneta wa Mombasa Mohammed Faki, Mwakilishi wa Wanawake, Zamzam Mohammed na Mbunge wa Mvita Machele Mohammed waliongoza waandamanaji kuandamana hadi katikati mwa jiji hilo.

Katika mtaa wa Kimathi jijini Nairobi, kundi la waandamanaji walilazimika kukimbia ili kujilinda baada ya maafisa wa polisi kuwarushia vitoa machozi.

Hata vivyo sehemu nyingi za Nairobi, zilibaki tulivu huku wenyeji wakiendelea na biashara zao kama kawaida.

Akiwa Kamukunji, Odinga aliwaongoza wafuasi wake katika kuwakumbuka wote waliopigania mfumo wa vyama vingi nchini humo akiwataja Kenneth Matiba, Joseph Murumbi, Jaramogi Oginga Odinga na yeye mwenyewe.

"Leo haitakuwa kama siku nyingine. Tuliwaambia wakome kuingilia vyama vyetu. Sasa, wabunge 25 wa Jubilee na saba kutoka ODM wamepelekwa UDA," alisema.
Screenshot_20230708_051928_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom