Shaffih Dauda
SEHEMU YA PILI
Watu wa Marekani wakaona thamani ya Ligi ya England duniani, wakakubaliana hii ni sehemu sahihi ya kuwekeza. Wakatengeneza mpango kazi wa namna ya kuingiza mpira wa miguu nchini kwao kwa kwao si mchezo pendwa mbele ya American Football, basketball na baseball!
Ndipo walipoamua kuanzisha Major League Soccer [MLS], na wao ili kuifanya Ligi yao iwe maarufu wakatumia mbinu kama zilizotumiwa na England [kuchukua wachezaji wenye majina makubwa] lakini wao pia wana malengo ya kutengeneza timu ya taifa imara.
Kwa hiyo wanachukua wachezaji wenye majina ili kuamsha soko lakini pia kuvutia vijana wadogo kuingia kwenye soka lakini vilevile kuvutia wawekezaji kuwekeza kwenye miundombinu.
Leo Marekani wakiia timu ya taifa karibu nusu ya wachezaji wanatoka Ulaya tena kwenye timu kubwa zinazoshiriki Ligi kubwa! Maana yake wamefanikiwa.
Kwa sasa mchezo wa soka umeshakuwa maarufu Marekani, sasa wafanya biashara wenye nguvu Marekani waliokuwa wamewekeza kwenye michezo mingine [American Football na Basketball] wameingia kwenye soccer.
Kama haitoshi wamepenya na kuingia hadi Ulaya na kuanza kuzinunua timu, leo hii mmiliki wa Man United ni raia wa Marekani, mmiliki wa Liverpool ni raia wa Marekani, Arsenal ukiangalia wamiliki wa hisa nyingi miongoni mwao ni raia wa Marekani ukienda Ufaransa!
Kwa miaka ya hivi karibuni mataifa ya kiarabu ni wapinzani wa Marekani kwenye masuala ya biashara na uchumi! Na wao wameanza kuingia kwenye soka.
Waarabu wao wameanzia juu kwa maana ya wawekezaji kuanza kununu klabu [PSG, Man City, Newcastle Unite], sasa hivi wameamua kuacha athari chanya kwenye klabu za mataifa yao.
Kwa hiyo wameanza kupeleka watu kwenye nchi zao kwa ajili ya kujenga mifumo na kutengeneza timu zao na mpira wao ili kushambulia kwenye kiwanda hiki ambacho kinaonekana kimechangamka kwenye biashara na kina zidi kukua.
Saudi Arabia ni nchi yenye utajiri mkubwa utokanao na mafuta na gesi kwa hiyo miaka kadhaa ijayo tutaona matokeo ambayo sio wao tu watanufaika bali watu wengi duniani
DIGALA

.