Makapuku Forum

Makapuku Forum

BANDA AOMBA CHAKE ASEPE
.
Winga Peter Banda anadaiwa kugoma kupelekwa kwa mkopo katika timu nyingine akitaka avunjiwe mkataba kama hayupo kwenye mipango ya klabu hiyo.
.
Awali ilielezwa Banda alikuwa akitakiwa na Azam FC, lakini dili hilo linadaiwa kufa kimya kimya baada ya kusajiliwa Mgambia, Djibril Sillah. Banda anashinikiza alipwe chake asepe kama hayupo kwenye mipango ya kocha Roberto Oliveira.

………………
Screenshot_20230630_160502_Instagram.jpg
 
WAKALI HAWA
.
03—EDINE Dzeko ni mmoja kati ya wachezaji wawili pamoja na Cristiano Ronaldo (Ligi Kuu England, La Liga, Serie A), waliofikisha mabao 50 katika walau ligi tatu tofauti kati ya tano kubwa za Ulaya.
Screenshot_20230630_160637_Instagram.jpg
 
ASTON Villa inadaiwa kuwa kwenye rada za mwisho za kumsajili beki kisiki wa Villarreal, Pau Torres mwenye umri wa miaka 26, katika dirisha hili. Staa huyo wa kimataifa wa Hispania kwa sasa yupo kwenye mwaka wa mwisho wa mkataba wake na anaonekana kutamani zaidi kutua England kuungana na Unai Emery. Msimu uliopita alicheza mechi 39 za michuano yote.
Screenshot_20230630_160744_Instagram.jpg
 
Ocean Gate, wamiliki wa chombo kilicholipuka na kuuwa abiria wote watano wiki iliyopita wametangaza tena tour nyingin...sasa hivi ni kwenda kwenye kisiwa cha Azore kilichoko huko Ureno. Kisiwa hiki kipo katika eneo ambalo misingi (tectonic plate) inayobeba mabara matatu inapokutana.

Kutokana na jiografia yake eneo hili huwa linakumbwa na Volcano za mara kwa mara tena zenye nguvu kubwa.

Tetemeko limewahi kutokea eneo hilo na kuuwa karibu watu elfu 5 mwaka 1522..sasa Ocean Gate wanataka kupeleka watu kwenda kutalii eneo hilo ambalo liko umbali wa kilomita 1400 kutoka mjini Lisbon Ureno... safari ni mwakani mwezi wa 5..nauli yake ni Shilingi Milioni 600 tu...!!
Screenshot_20230630_190459_Instagram.jpg
 
Huyu Bwana anaitwa Ike Ekweremadu... alikuwa Seneta katika Bunge la Nigeria.

Mwaka jana Ike pamoja na mkewe Beatrice Nwanneka Ekweremadu walimsafirisha kijana wa kiume mwenye umri wa miaka 21 kwa jina Daniel kutoka Nigeria kwenda Uingereza kwa madai kwamba walikuwa wanampeleka kumtafutia kazi na wangempa pesa Shilingi milioni 21 hivi kwa ajili ya kuanzia maisha. Kumbe jamaa alikuwa amepanga kwenda kumtoa figo ili apandikiziwe binti wao ambaye figo zake zilikuwa zimefeli.

Baada ya kufika hospitali na kijana kufanyiwa maandalizi ya upasuaji akashtuka, akasema mimi nimeletwa kufanya kazi mbona mnanisainisha upasuaji tena.

Madaktari wakamwambia we si mmekubaliana unakuja kuchangia figo. Figo tena.

Daniel akapiga kelele. Polisi wakafanya uchunguzi na kuwafungulia mashtaka Seneta Ike, mkewe pamoja na daktari waliyeshirikiana kuchora mchongo huo.

Seneta amehukumiwa kifungo cha miaka 9 jela, mkewe miaka 4 na daktari miaka 10.

Kijana huyo aliiambia mahakama kwamba hataki kufungua hata kesi ya kuomba fidia kwa sababu hataki kitu chochote kutoka kwa hao watu kwa sababu wana roho mbaya.

Kwa sasa Daniel anaishi mafichoni huko Uingereza. Kwa sheria za Uingereza mtu anayepaswa kuchangia viungo anapaswa kuwa ndugu wa karibu au mtu ambaye mmekuwa katika mahusiano kwa muda mrefu mfano mke au mume...!
Screenshot_20230630_205603_Instagram.jpg
Screenshot_20230630_210401_Instagram.jpg
 
Watu 49 wamefariki dunia baada ya lori kupoteza mwelekeo na kuyaparamia magari mengine pamoja na watembea kwa miguu kwenye makutano ya barabara moja yenye shughuli nyingi mashariki mwa Kenya.

Picha za televisheni zimeonesha uharibifu mkubwa uliotokea kwenye eneo la tukio ikiwemo mabaki ya magari madogo yaliyogongwa na lori hilo lililopinduka, Waokoaji pia wameonekana wakipambana kujaribu kuwatafuta Watu wanaoaminika wamekwama kwenye mabaki ya magari yaliyopondeka.

@dw_kiswahili imeripoti kuwa Polisi imesema ajali hiyo imetokea kwenye barabara kuu inayounganisha miji miwili ya Kericho na Nakuru, Maafisa wa Usalama wamesema mbali ya vifo vya Watu 49, wengine 30 wamejeruhiwa vibaya na kupelekewa Hospitali huku kukiwa na wasiwasi kwamba idadi inaweza kuongezeka.

Rais William Ruto wa Kenya na Viongozi wengine wa Taifa hilo wametuma salamu za rambirambi kufuatia ajali hiyo.
Screenshot_20230701_145650_Instagram.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Balozi Agnes Richard Kayola kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Malawi.

Taarifa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, imesema kuwa kabla ya uteuzi huo, Balozi Kayola alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, na kwamba uteuzi huo unaanza mara moja.

Screenshot_20230701_145814_Instagram.jpg
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewasili mkoani Tanga leo Jumamosi Julai Mosi 2023, kwa ziara ya kikazi ya siku moja.

Akiwa mkoani humo, Waziri Mkuu Majaliwa atapokea taarifa ya mradi wa upanuzi wa bandari ya Tanga na kutembelea kiwanda cha saruji cha Maweni.

Baada ya hapo, Majaliwa atafanya kikao na viongozi wa Serikali mkoani humo.
Screenshot_20230701_145909_Instagram.jpg
 
Kamati ya kitaifa ya Shoroba za Wanyamapori nchini imefanya ziara ya kuzitambua shoroba mbalimbali ambazo zinakabiliwa na changamoto kubwa inayotokana na kuongezeka kwa shughuli za kibinadamu kwenye mapitio hayo ya wanyamapori.

Kwa mujibu wa kamati hiyo, ongezeko hilo limesababisha madhara makubwa kwa wananchi wanaoishi katika maeneo hayo.

Kamati hiyo imetembelea ushoroba wa Mwanihana - Magombela unaounganisha Hifadhi ya Taifa Udzungwa, Nyerere na Pori la Akiba la Kilombero, ambapo Mwenyekiti wa kamati hiyo, Lina Kitosi amesema tembo wamekuwa wakipita kwenye maeneo hayo kwa lengo la kurejea njia zao za awali, na hivyo kusababisha uharibifu wa mazao na makazi ya watu.

"Tumetembelea ushoroba huu ambao ni miongoni mwa shoroba 61 za kitaifa, wananchi wanapaswa kuzitambua, na kuzingatia maelekezo ya Serikali na hivyo kuepuka kufanya shughuli za kibinadamu kwenye maeneo kama haya,," amesema Kitosi.
Screenshot_20230701_150015_Instagram.jpg
 
ONYANGO AZIDI KUKOMAA SIMBA
.
Mastaa wa kikosi cha Simba wameitwa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya vipimo vya afya vitakavyofanyika wiki ijayo, lakini taarifa mbaya ni kwamba beki Mkenya Joash Onyango amezidi kukomaa kwa kuandika barua nyingine tena akisisitiza aachwe asepe kwenda klabu nyingine.
.
Mbali na Onyango, inaelezwa pia beki mwingine wa kati Keneddy Juma amegoma kuongeza mkataba licha ya kuitwa mezani kwa madai kwamba anahitaji kupata timu ambayo itampa nafasi ya kucheza.
Screenshot_20230701_150131_Instagram.jpg
 
MASON MOUNT atakuwa akipokea mshahara wa Pauni 250,000 (Sh 767milioni) kwa wiki uhamisho wake utakapokamilika wiki ijayo. Kwa mujibu wa ripoti Manchester United imakubali kutoa Pauni 60 kwaajili ya kiungo huyo wa zamani wa Chelsea.
.
Mount anatajaria kusaini mkataba wa miaka mitano akipigie Man United msimu ujao. Mshahara wa Mount ni zaidi ya ule aliokuwa akipewa Chelsea Pauni 80,000.
Screenshot_20230701_150247_Instagram.jpg
 
YANGA YAKWEPA RUNGU LA FIFA
.
Mashabiki wa Yanga walikuwa na presha juu ya timu kupewa kibano cha kuzuiwa kusajili madirisha matatu kutokana na deni la kocha wa zamani, Luc Eymael, hata hivyo mabosi wamekwepa rungu la FIFA kwa kumalizana naye.
.
Eymael amethibitishwa kumaliziwa sehemu ya fedha alizokuwa akiidai Yanga kwa kumvunjia mkataba 2020 na kusababishwa klabu kuwa hatarini kufungiwa kusajili madirisha matatu kulingana na taarifa ya Fifa.

Screenshot_20230701_150535_Instagram.jpg
 
MKONGWE ASHANGAA
.
Mkongwe wa Arsenal, Ray Parlour ameshangaa sababu ya Arsenal kumsajili Kai Havertz kwa Pauni 65 milioni. Mjerumani huyo alikamilisha uhamisho wake wiki iliopita lakini mkongwe huyo hakupendezwa na usajili huo. Parlour anaamini Arsenal isingekubali kutoa kiwango hicho cha pesa kwaajili ya nyota huyo.
Screenshot_20230701_150647_Instagram.jpg
 
DE GEA ANAOA
.
Kipa wa Manchester United, David de Gea anatarajia kufunga ndoa wikiendi hii na mpenzi wake wa zamani Edurne mwenye umri wa miaka 37. Wawili hawa wamedumu kwa muda wa miaka 12 na wamebahatika kupata mtoto wa kike.
.
Kwa mujibu wa ripoti De Gea (32) amealika wachezaji wenzake na marafiki zake wa karibu, harusi hiyo itafanyika Hispania alipozaliwa.
Screenshot_20230701_150903_Instagram.jpg
 
VARDY AGOMEA WAARABU
.
Straika wa Leicester City na England, Jamie Vardy, amekataa ofa kutoka Al Khaleej ya Saudi Arabia na badala yake amepanga kuendelea kusalia kwenye kikosi chake licha ya timu hiyo kushuka daraja msimu uliomalizika.
.
Vardy mwenye umri wa miaka 36, mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika mwakani, ambapo msimu uliopita hakuwa katika ubora wake akifunga mabao sita katika mechi 42 za michuano yote.
Screenshot_20230701_150952_Instagram.jpg
 
TIMBER KUTUA LONDON KUFANYIWA VIPIMO
.
Beki wa Ajax na timu ya taifa ya Uholanzi, Jurrien Timber, 22, anatarajiwa kutua England kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya afya kabla ya kukamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Arsenal baada ya timu zote mbili kufikia makubaliano.
.
Usajili wa supastaa huyu utakwenda kuigharimu Arsenal kiasi cha Euro 42 milioni. Mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika 2025, lakini amekuwa beki aliyezivutia timu nyingi Ulaya kutokana na kiwango bora alichoonyesha.
Screenshot_20230701_151105_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom