Makapuku Forum

Makapuku Forum

alipogundua kuwa hali ilikuwa ni tete,na watu walikuwa wakiamishiwa kwenye maboti ili kuokoa maisha yao, bwana Charles Joughin akawashangaa watu wale kukimbia janga la meli kuzama na kusahau janga la njaa ambalo labda lingewakuta wakiwa kwenye maboti, basi mpishi yule akahakikisha kila boti lilikuwa likipata chakula.

Wakati huo Meli ya Titanic iliendelea kudidimia kwenye maji yenye ubaridi mkali zaidi ya friji, kwa nukuu za ofisa msaidizi wa meli ya Titanic aitwaye Lightoller alisema “kugusa maji ya bahari ya atlantic ilikuwa ni sawa na kuchomwa visu elfu moja mwilini”

Sauti za majonzi na vilio vya watu viliendelea kusikika, Bwana Charles Joughin aligundua kuwa hakuwa na mahali pakukaa kwenye maboti ya kuokolea , basi akarudi chumbani kwake nakuchomoa kinywaji aina ya whiskey,..mpishi huyo alikunywa na kujigalagaza.
 
Maamuzi aliyochukua yalitofautiana na watu wote lakini yalikuwa maamuzi pekee yaliyookoa maisha yake.

Baada ya muda kidogo umeme ukakatika nakusababisha watu wote kupoteza matumaini..kasoro bwana Charles ambaye hakua amepaniki kwasababu pombe ilimpa ujasiri usio wa kawada

Meli ya titanic ikakatika na kujigawa Katikati,na yote ikazama ndani ya bahari ya atlantic ,ikiwa na maelfu ya watu pamoja na bwana Charles Joughin
 
Kwa watu wengi kuingia kwenye maji hayo yenye kiwango cha baridi kali ,Wakajikuta wakipata mshtuko wa ghafla na kupoteza uhai, wanasayansi wanadai vifo vingi vilitokana na mshtuko huo uliosababishwa na baridi pamoja na hali ya hofu iliyopelekea hata mafundi wa kuogelea kuzama, na waliojitahidi kuogelea walikufa kwasababu ya baridi kali lililotafuna miili yao ndani ya dakika chache.

Lakini hali ilikuwa ya tofauti kwa bwana Charles Joughin , mtaalamu wa kuogelea aliyelewa tilalila,aliweza kukaa zaidi ya masaa matatu kwenye maji ya barafu,

katika kiza kizito cha bahari ya Atlantic, ni makelele ya vilio vya watu waliokuwa wakifa ndiyo yaliyokuwa yakisika,bwana Joughin alikaa kwenye maji hayo hadi jua lilipoanza kuchomoza,ndipo akaogelea kusogelea boti aliloliona ,watu wakamshangaa walipomuona,na japokuwa hakukuwa na nafasi lakini wakamsaidia kwa kumshika mkono huku Miguu yake ikiwa ndani ya maji hadi msaada wa meli ya Caparthia ulipofika

Bwana Charles Joughin anakumbukwa kama mlevi aliyelishinda janga kubwa zaidi katika karne ya 20.
 
WANAUME KUVAA NGUO ZA KIKE ILI KUPATA NAFASI KWENYE BOTIAjali ya meli ya Titanic haikuacha kumbukumbu za majonzi peke ake bali na vihoja vilivyoacha watu midomo wazi,huku wengine wakikumbukwa kwa ushujaa,wapo waliopigania kupona hata kama wakikumbukwa katika kashfa mbaya na kuathiri maisha yao yote.

Jua lilipochomoza na wakati meli ya Carpathia inakaribia eneo ilipozama meli ya Titanic, wanaume wengi wakaonekana katika mavazi ya kike huku wakiwa wametulia kama akili zao haziko sawa, kihoja hiki kilisababisha ndoa kuvunjika na wengine kama masabumi Hosono kupoteza ajira yake pamoja na heshima nchini kwake huku akitangazwa nchi nzima kama msaliti wa tamaduni na imani zao walizozitukuza.
 
Ni nini kilitokea katika masaa mawili hayo na dakika 40 za ajali ya kifo , na kusababisha baadhi ya wanaume kuwa katika muonekano wa kike…

Kuelewa kisa hiki inabidi turudi nyuma kidogoMeli ya Titanic ilikuwa na uwezo wa kubeba watu 3547, na kwa bahati nzuri siku hiyo ya safari kulikuwa na watu 2224

Mpango ulioandaliwa na wataalamu ni kuwa Meli hiyo kuwa na maboti ya dharura 48,lakini Idadi ikapunguzwa na Mmiliki wa meli hiyo akitaka idadi ya maboti kupungua hadi 20,kwasababu aliona maboti mengi yangeziba nafasi na kuzuia muonekano mzuri wa bahari ya Atlantic.

Baada ya ajali kutokea nafasi ya upendeleo ilikuwa kwa wanawake na watoto, hivyo wanaume wengine wakavaa mavazi ya kike nakujifanya wanawake ili wapate nafasi katika maboti.
 
Mwaka 1916 , yaani miaka minne baada ya ajali ya Titanic,abiria mashuhuri aitwaye Dickson akaachana na mke wake,baada ya mke wake kushindwa kuvumilia kashfa aliyokuwa akishutumiwa mme wake ya kujifanya mwanamke ili apone,


kashfa hiyo iliwazonga baadhi ya wanaume waliosemekana kuvaa mavazi ya kike pamoja na kuigiza kama wanawake, lakini aliyeathirika zaidi na kashfa hiyo alikuwa bwana Masabumi Hosono, raia wakijapan pekee aliyekuepo kwenye meli ya Titanic.

Kwanza baada ya ajali alipata umaarufu mkubwa nchini marekani na kuhojiwa na vyombo vya habari tofauti huku akipewa jina la “the lucky Japanese boy”, kwani alikuwa mjapani pekee katika watu 700 walioponyeka katika janga hilo la kutisha
 
Lakini habari ya wanaume waliovaa nguo za kike ilipofika japan,bwana Masabumi Hosono akajuta kupona kwenye ajali ya Titanic,

bwana Masabumi alionekana kama mtu aliyeidharirisha nchi ya Japan kwa kushindwa kufa kiume kama tamaduni zao zilivyo, Masabumi akapoteza ajira aliyokuwa nayo Mwanzoni , na kujikuta akizongwa na chuki,dharau ,kutengwa pamoja na kashfa ya aibu hadi alipokufa
 
MTU ALIYESABABISHA AJALI YA TITANIC.

Meli kubwa ilizama kwasababu ya kitu kidogo kilichosahaulika katika mifuko ya bwana David Blair.

David Blair alikuwa Afisa wa meli ya Titanic,kabla ya meli hiyo kuanza safari,bwana David blair akaondoka kwa dharura na nafasi yake ikashikiliwa na mtu mwingine, baada ya ajali ya Titanic kutokea wengi walimuona kama mtu mwenye bahati duniani lakini yeye alikuwa na huzuni kubwa kwani aliujua ukweli ,kuwa yeye ndiye aliyesababisha ajali ya Titanic,na kama angekuwepo ajali hiyo ingezuilika…

Miaka 108 iliyopita katika usafiri wa meli,wafanyakazi wa meli walitumia darubini kutazama kama kuna hatari yoyote mbele yao.

Lakini cha ajabu ,katika safari ya meli ya Titanic ,wafanyakazi wanaohusika na kazi ya kuangalia hawakuweza kuchukua darubini mahali zinapoifadhiwa kwani bwana David Blair ndiye aliyEkuwa na funguo zilizofungia Darubini hizo.
 
Kwakuwa bwana David Blair aliondoka akiwa na haraka sana,akasahau kukabidhi funguo za darubini.

Watafiti wanadai kama darubini ingekuwepo basi mwamba wa barafu ungeonekana mapema sana ,na ajali isingetokea,bila darubini,meli ya Titanic ilikuwa kama kipofu anaekimbia Katikati ya barabara yenye visiki na mashimo

Bwana Frederick fleet na Reginald lee ndio waliotegemewa kutazama kama kulikuwa na hatari yoyote mbele yao,na kwakuwa walikuwa wakitumia macho tu hawakuweza kuona mbali kwenye kiza kizito cha bahari ya Atlantic.

Inasemekana ikiwa bado kama sekunde 37 kuufikia mwamba mkubwa wa barafu ndipo bwana Frederick fleet akabwatuka kama mtu aliyekurupuka usingizini
 
iceberg,right ahead”…akimaanisha mwamba wa barafu upo mbele , na ndipo harakati za kujiokoa zilipoanza ambazo hazikuzaa matunda na meli ya Titanic ikajikuta ikibamiza vibaya mwamba huo mgumu wa barafu.


Frederick Fleet alikuwa mmoja kati ya abiria waliopona,alibeba lawama nyingi kwa kuonekana mzembe

Mwaka 1965 akajiua mwenyewe baada ya kifo cha mke wake,na katika kaburi lake zilikutwa darubini mbili pamoja na ujumbe uliosema “samahani kwa kuchelewa kuzileta darabuni“

Kuna watu wanaamini mtu huyo asiyejulikana alikuwa bwana David Blair,aliyeishi maisha yake na majuto mengi

Mwaka 2010,funguo iliyosababisha ajali ya Titanic, ikauzwa kwa dola za kimarekani laki 1 na 30 elfu ambayo ni zaidi ya milioni 300 za kitanzania;
 
UPENDO WA KWELI….

Waswahili wanasema,mapenzi upofu,mapenzi uchizi ,hili linatokana na maamuzi yasiyo ya kibinafsi wanayoyaamua watu kwasababu ya kupenda…

Katika ajali ya meli ya titanic,yapo matukio yatakayobaki kukumbukwa kama upendo wa kweli katika historia. Katika meli hiyo kulikuwa na wapendanao 26 waliokuwa wakisheherekea fungate yao , ikiwemo tajiri aliyesemekana alikuwa tajiri wa dunia katika kipindi hicho aitwae bwana John Jacob Astor, lakini matukio yaliyothibitisha upendo wa dhati hayakutokea kwa wapendanao hao, bali kwa wanandoa waliodumu kwenye ndoa kwa miaka 41. bwana Isidor na mkewe Ida Straus

Kama umetazama muvi ya Titanic,ambayo waswahili wengi tunaiita titanike ,na kama unakumbuka wakati kate Winslet alipoacha nafasi yake kwenye boti ili kufa pamoja na Leornard DiCaprio basi wazo la igizo hilo lililogharimu zaidi ya gharama zilizotumika kutengenezea meli ya Titanic limetoka kwenye kisa hiki cha wapendanao..
 
Isidor na Ida walitoka ufaransa kwenye mapumziko na kuwa moja kati ya abiria wanaoelekea marekani,ajali ya Titanic ilipotokea,wote kwa pamoja wakawaishwa kwenye maboti kutokana na hadhi walizokuwa nazo

ikumbukwe kuwa boti zilikuwa ni chache sana,kwasababu mmiliki wa meli ya Titanic aliamini kuwa meli hiyo haiwezi kuzama ila matumizi ya maboti mengi yanaeza haribu muonekano wa meli.waswahili husema kipya kinyemi.

Hakukuwa na uwezekano wakupakia kila mtu kwenye maboti,nafasi za upendeleo zilikuwa kwa bahadhi ya wanawake,watoto na watu wenye hadhi ikiwemo bwana Isidor na mkewe.
 
Hata hivo millionaire Isidor alipoona watoto wengi pamoja na wanawake wakikosa nafasi akakataa kupanda boti na kutaka nafasi yake apewe mwanamke au mtoto .

Mke wa Isidor aliyekuwa ameshajipatia nafasi katika boti akashuka baada ya mme wake kufanya maamuzi yale, japokuwa Isidor alimlazimu Ida abakie kwenye boti lakini kwa nukuu za abiria inasemekana Ida alimwambia Isidor kuwa “nafasi yangu ipo ulipo,nimeishi na wewe na kukupenda,basi nitakufa na wewe”

Wanandoa wale walishikana pamoja huku wakiwa kimya na kufutana machozi ya uchungu huku bahari ya atlantic ikimeza miili yao, kwakuwa upendo wao Ulikuwa wa dhati basi na historia haitowasahau.
 
Hata hivyo hakuwa Ida peke yake aliyetoka kwenye boti kwa ajili ya mme wake, pia kulikuwa na mwanamama anayekumbukwa kwa jina la Ann Elizabeth Isham

Kama wewe ni mpenzi wa filamu za kimarekani basi utakuwa si mgeni na tukio la mtu kurudi mahali pa hatari kwa ajili ya mbwa wake.

Mwanamama huyu alipoingia kwenye boti akakumbuka kuwa alimsahau mbwa wake aitwaye “Great Dane” basi akakimbia upesi na kurudi kwenye meli na hapo hakuonekana tena akirudi hadi baadae mwili wake ulipatikana akiwa amemkumbatia mbwa .

The end

Cooy And paste
 
Hata hivyo hakuwa Ida peke yake aliyetoka kwenye boti kwa ajili ya mme wake, pia kulikuwa na mwanamama anayekumbukwa kwa jina la Ann Elizabeth Isham

Kama wewe ni mpenzi wa filamu za kimarekani basi utakuwa si mgeni na tukio la mtu kurudi mahali pa hatari kwa ajili ya mbwa wake.

Mwanamama huyu alipoingia kwenye boti akakumbuka kuwa alimsahau mbwa wake aitwaye “Great Dane” basi akakimbia upesi na kurudi kwenye meli na hapo hakuonekana tena akirudi hadi baadae mwili wake ulipatikana akiwa amemkumbatia mbwa .

The end

Cooy And paste
Asante sana Numbi barikiwa kipenzi
 
Magazeti ya leo June 29, 2023.
Screenshot_20230629_063856_Opera%20Mini.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom