Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kutokana na hofu ya kuvamiwa na simba, Serikali ya Kijiji cha Lupembe Lwa Senga, Kata ya Lyamgungwe, wilayani Iringa imetoa rai kwa wananchi kurudi majumbani kwao ifikapo saa 11 jioni wakati jitihada za kumtafuta mnyama huyo zikiendelea.

Tangu Juni 13, mwaka huu simba hao waliingia kwenye makazi ya watu katika Kata ya Maboga na Kiponzelo, vilivyo karibu na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

Akizungumza na Mwananchi Digital, Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Ezekiel Mhhehe ameomba jitihada za kumsaka simba huyo ziongezeke ili kuondoa hofu kwa wananchi hao.

“Kijijini kwetu wamekula ng’ombe wawili, tunaomba jitihada ziongezeke kwa kweli tunaogopa sana, tunachofanya nikuwasisitiza wananchi watulie majumbani hasa kuanzia saa 11 jioni. Na kweli ikifika muda huo humkuti mtu mtaani,” amesema Mhhehe.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Veronica Kessy amesema mpaka sasa simba wanakadiriwa kuua ng’ombe 25, kujeruhi wawili, mbuzi watano, kondoo watano, nguruwe watatu na kuku mmoja.

Baadhi ya wananchi wa kijiji hao wakizungumza na Mwananchi Digital jana Jumapili Juni 26, 2023, wamesema simba hao wakipatikana maisha yao yatarudi kwenye hali ya kawaida tofauti na sasa wakati hofu imetawala.
Screenshot_20230627_052705_Instagram.jpg
 
Uvutaji shisha na matumizi ya pombe kali kwa baadhi ya vijana inaonekana kuwa ndiyo kwenda na wakati katika maisha.

Hata hivyo, mtindo huu wa maisha unaelezwa kuchangia ongezeko la maradhi ya moyo.

Wataalamu wa afya wanasema idadi ya wanaougua shinikizo la damu, kiharusi na maradhi ya moyo katika umri mdogo wa miaka 20 hadi 40 inaongezeka.

Awali, ugonjwa huo uliwapata zaidi watu wenye miaka 60 na zaidi.

“Uvutaji shisha na sigara huongeza mara tatu hatari ya mtu kufa mapema kutokana na ugonjwa wa moyo na kiharusi ikilinganishwa na kutovuta,” alisema Dk Upendra Bhalerao, mapema wiki hii alipotoa mada kwenye mdahalo uliowahusisha madaktari wa Tanzania na India, ulioandaliwa na taasisi ya Medeviva.

Dk Upendra, mbobezi wa upandikizaji moyo na mshauri wa magonjwa hayo kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India, alisema kwa wavutaji sigara na watumia tumbaku ni rahisi kupata changamoto ya mishipa ya damu inayosababisha mshtuko wa moyo na kiharusi.

Alisema uvutaji sigara huongeza kasi ya kuziba kwa mishipa ya moyo, pia huharibu mishipa mingine ya damu.

Screenshot_20230627_052834_Instagram.jpg
 
Mkali wa Afrobeat kutoka Nigeria, Burna Boy usiku wa kuamkia leo Juni 26 ameshinda tuzo ya BET Best International Act 2023 ikiwa ni mara yake ya nne.

Tuzo hiyo ambayo ni ya nne kwake inamfanya awea msanii wa kwanza kufanya hivyo Afrika akichukuwa mwaka 2019, 2020, 2021 na 2023 imetangazwa jana katika ukumbi wa Microsoft uliopo Los Angeles, Marekani.

Burna Boy amewabwaga Aya Nakamura (Ufaransa), Ayra Starr (Nigeria), Central Cee (Uingereza), Ella Mai (Uingereza), KO (Afrika Kusini), L7nnon (Brazil), Stormzy (Uingereza), Tiakola (Ufaransa), Uncle Waffles (Swaziland).
Screenshot_20230627_052932_Instagram.jpg
 
MWANASAYANSI Neil Armstrong ambaye amewahi kuufikia mwezi akitumia vyombo mbalimbali kupitia mission ya Apollo 11, alihitaji kuubeba mpira wa miguu na kwenda nao huko lakini shirika la anga la Marekani lilikataa ombi lake kwani hawakuamini kama mpira huo ni sehemu ya asili za Marekani. Soka Marekani limeanza kushika kasi miaka ya karibuni tofauti na nchi nyingine.
Screenshot_20230627_053035_Instagram.jpg
 
BAADA ya majadiliano ya muda mrefu klabu ya Coastal Union imefikia makubaliano ya kutoendelea na aliyekuwa nyota wa zamani wa Yanga, Juma Mahadhi kutokana na kutoridhishwa na kiwango chake.
.
Nyota huyo aliyejiunga na timu hiyo akitokea Geita Gold ameshindwa kuonyesha makali yake, hivyo viongozi kuamua kumpa mkono wa kwa heri ikiwa ni mwendelezo wa kuachwa kwa mastaa wengi kikosini.
.
Taarifa za ndani zinaeleza mbali na Mahadhi ila mastaa wengine pia waliopewa mkono wa kwaheri ni William Kisinga, kipa Abubakar Abbas.

Mastaa wengine ambao tayari wameachwa rasmi ni Joseph Zziwa, Emery Nimubona, Mahamoud Mroivili, Djibril Naim Olatoundji, Yema Mwamba, Yusuph Jamal na Yusuph Athuman aliyetokea Yanga kwa mkopo.
Screenshot_20230627_053130_Instagram.jpg
 
BAADA ya majadiliano ya muda mrefu klabu ya Coastal Union imefikia makubaliano ya kutoendelea na aliyekuwa nyota wa zamani wa Yanga, Juma Mahadhi kutokana na kutoridhishwa na kiwango chake.
.
Nyota huyo aliyejiunga na timu hiyo akitokea Geita Gold ameshindwa kuonyesha makali yake, hivyo viongozi kuamua kumpa mkono wa kwa heri ikiwa ni mwendelezo wa kuachwa kwa mastaa wengi kikosini.
.
Taarifa za ndani zinaeleza mbali na Mahadhi ila mastaa wengine pia waliopewa mkono wa kwaheri ni William Kisinga, kipa Abubakar Abbas.

Mastaa wengine ambao tayari wameachwa rasmi ni Joseph Zziwa, Emery Nimubona, Mahamoud Mroivili, Djibril Naim Olatoundji, Yema Mwamba, Yusuph Jamal na Yusuph Athuman aliyetokea Yanga kwa mkopo.View attachment 2670010
Hakuna maisha yenye afadhali
 
KIPA wa zamani wa Liverpool Simon Mignolet ambaye kwa sasa anaichezea Club Brugge alianza maisha yake ya soka akiwa kama mshambuliaji kwani ndiyo nafasi aliyokuwa akiipenda kuichezea. Lakini aliachwa kwenye timu na hiyo ilisababisha ajaribu upande mwingine wa kuwa kipa na huko ndiko alikofanikiwa.
Screenshot_20230627_053348_Instagram.jpg
 
SIMBA, YANGA HALI TETE U-20!
.
Hali ni tete kwa timu za vijana za Simba na Yanga baada ya juzi kufumuliwa kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vijana U-20, huku upande wa Jangwani mambo yakiwa mabaya zaidi kwani imeonyeshwa mlango wa kutokea katika ligi hiyo inayoendelea Uwanja wa Azam Complex.
.
Yanga iliyoanza michuano hiyo kwa kufungwa bao 1-0 na Dodoma Jiji, juzi ilikumbana na kibano kingine cha mabao 3-1 kutoka kwa Tanzania Prisons na leo itashuka uwanjani kukamilisha ratiba dhidi ya Polisi, huku Prisons ikijihakikisha kwenda robo fainali kutoka Kundi B.
.
Kwa upande wa mechi za Kundi D, Simba ilikumbana na kipigo cha kwanza kutoka kwa Ihefu iliyoshinda 1-0 . Simba ilianza ligi hiyo kwa kutoka suluhu na Kagera Sugar katika kundi hilo na leo itashuka uwanjani kuvaana na vinara, Azam huku ikisikilizia matokeo ya Kagera Sugar na Ihefu kama itatoboa kwenda robo kungana na Wanalambalamba.
Screenshot_20230627_053443_Instagram.jpg
 
Mido Luka Modric ameongeza kandarasi ya mwaka mmoja kusalia Madrid mpaka mwaka 2024 uamuzi huo ameufikia baada ya kuzitema ofa kubwa kutoka Saud Arabia

Mpaka sasa amehudumu kwa takribani miaka 12.
Screenshot_20230627_054017_Instagram.jpg
 
𝐎𝐅𝐅𝐈𝐂𝐈𝐀𝐋: Kalidou Koulibaly ametambulishwa kama mchezaji mpya wa Al Hilal ya Saudi Arabia kwa mkataba wa miaka mitatu

Chelsea itapokea takriban €23m kwa uhamisho huu

Screenshot_20230627_054413_Instagram.jpg
 
Washindi wa Treble wa Pep Guardiola wamejitolea kuboresha kandarasi ya winga wa Ureno Bernardo Silva katika jitihada za kumzuia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 kuondoka klabu hiyo kuelekea Saudi Arabia. (Sunday Times)

Screenshot_20230627_054502_Instagram.jpg
 
Kiungo wa kati wa Fulham na Ureno Joao Palhinha, 27, ametambuliwa kama chaguo linalowezekana kwa Barcelona. (Sport)

Screenshot_20230627_054554_Instagram.jpg
 
Arsenal wanakaribia kumsajili Jurrien Timber baada ya ofa rasmi ya 2 kuwasilishwa leo. Thamani ya ofa ya pili inakaribia €45/48m.

Mkataba uko tayari wa hadi 2028 kwani Timber amekuwa wazi: anapenda project ya Arsneal na anataka kujiunga nao.
Screenshot_20230627_054642_Instagram.jpg
 
Uongozi wa Simba SC umeonesha kuwa makini sana katika kukijenga kikosi chao kwa msimu ujao, hiyo ni baada ya kuweka wazi kwamba utashusha vyuma vya kazi kwa ajili ya kupambania malengo kwa msimu mpya wa 2023/24.

Timu hiyo chini ya Kocha Mkuu, Roberto Oliveira ‘Robertinho’, ipo kwenye mwendelezo wa maboresho ya kikosi chao ikianza kuwapitishia Panga mastaa waliofikia makubaliano ya kutoendelea nao.

Miongoni mwa nyota ambao wamepewa mkono wa asante ni Erasto Nyoni, Beno Kakolanya, Victor Akpan, Nelson Ókwa, Agustine Okrah, Mohamed Ouattara na Jonas Mkude.

Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amesema kuwa mpango mkubwa ni kusajili wachezaji wazuri ambao wataleta ushindani ndani ya kikosi hicho.

“Tutawatambulisha wachezaji wa kazi kwa ajili ya kutupa furaha Wanasimba, unajua hatukuwa na mwendo mzuri msimu ambao umeisha kwa kushindwa kufikia malego kwa asilimia kubwa.

“Msimu ujao utakuwa na ushindani mkubwa, na sisi tunalijua hilo, tunaanza na maboresho kwenye kikosi chetu, kikubwa mashabiki wawe na subira mambo mazuri yanakuja na tutafanya kazi kuwa na timu imara,” amesema Ally

Screenshot_20230627_054730_Instagram.jpg
 
Arsenal wameweka gharama ya pauni milioni 35 kwa mshambuliaji wa Marekani Folarin Balogun huku kukiwa na nia kubwa ya kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 kutoka kwa vilabu vingine (Sun)
Screenshot_20230627_054832_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom