Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
Huyu ndiye mwamba aliyemtikisa Putin.. anaitwa Yevgeny Prigozhin. Historia na makuzi yake vimejaa utata mwingi.
Aliwahi kukaa gerezani karibu miaka 10 akitumikia kifungo cha miaka 13 kutokana na unyang'anyi na wizi wa kutumia silaha.
Baada ya kutoka gerezani alianzisha kampuni ya migahawa huko Urusi, mgahawa wake maarufu sana ulikuwa unaelea majini.
Putin alipenda sana mapishi yake na akawa anawapeleka wageni wake kwenye migahawa ya huyu mwamba.
Taratibu urafiki wao ukakuwa na kuimarika, akaanza kupata tenda za kulisha Ikulu. Baadae akaibukia kumiliki jeshi binafsi linaloitwa Wagner. Wanajeshi wake wengi ni mamluki na wengi wao ni wafungwa wa Kirusi.
Jeshi la Wagner linakodiwa na mtu yeyote na wanafanya kazi yoyote ile unayotaka wewe.. ukiwapa kazi ya kumtoa ex wako kucha, wao wanafanya, au ukitaka wamgonge gonge na nyundo kwenye ugoko wao hawana hiyana..ni hela yako tu.
Huko Syria wanajeshi hawa walilaumiwa kuuwa watu kwa nyundo na kuwabanika.
Huku Afrika Wagner wamehusika kulinda baadhi ya viongozi wa Afrika na kuleta vurugu katika baadhi ya nchi za Kiafrika. Idadi kubwa ya wanajeshi hawa wako Afrika ya Kati, Mali, Sudan na Msumbiji.
Wagner wameongoza uvamizi wa Urusi nchini Ukraine na kuuteka mji wa Bakhmut. Sasa urafiki na Putin umefika mwisho kwa madai kwamba viongozi wa Jeshi la Urusi wanamhujumu.
Juzi Mwamba akaongoza vikosi vyake kwenda Moscow, kwa madai kwamba anataka viongozi wa jeshi akiwemo waziri wa Ulinzi waondolewe. Vikosi vikafika mpaka Kilomita 200 kutoka Moscow.
Putin akawasha ndege akaikimbia Moscow. Viongozi wa Magharibi na Amerika wanasema tukio la jana limefunua udhaifu wa Putin.
Putin akamtuma msela wake Rais wa Belarus. Wakakubaliana, mwamba akasitisha uasi akageuza majeshi .
Sasa mwamba anaenda kuishi Belarus na wanajeshi wake hawatashitakiwa kwa tukio la jana.Lakini kuna tetesi kwamba mwamba hatakaa muda mrefu Belarus bali ataondoka na kuja kuishi msituni huku Afrika....!!
Aliwahi kukaa gerezani karibu miaka 10 akitumikia kifungo cha miaka 13 kutokana na unyang'anyi na wizi wa kutumia silaha.
Baada ya kutoka gerezani alianzisha kampuni ya migahawa huko Urusi, mgahawa wake maarufu sana ulikuwa unaelea majini.
Putin alipenda sana mapishi yake na akawa anawapeleka wageni wake kwenye migahawa ya huyu mwamba.
Taratibu urafiki wao ukakuwa na kuimarika, akaanza kupata tenda za kulisha Ikulu. Baadae akaibukia kumiliki jeshi binafsi linaloitwa Wagner. Wanajeshi wake wengi ni mamluki na wengi wao ni wafungwa wa Kirusi.
Jeshi la Wagner linakodiwa na mtu yeyote na wanafanya kazi yoyote ile unayotaka wewe.. ukiwapa kazi ya kumtoa ex wako kucha, wao wanafanya, au ukitaka wamgonge gonge na nyundo kwenye ugoko wao hawana hiyana..ni hela yako tu.
Huko Syria wanajeshi hawa walilaumiwa kuuwa watu kwa nyundo na kuwabanika.
Huku Afrika Wagner wamehusika kulinda baadhi ya viongozi wa Afrika na kuleta vurugu katika baadhi ya nchi za Kiafrika. Idadi kubwa ya wanajeshi hawa wako Afrika ya Kati, Mali, Sudan na Msumbiji.
Wagner wameongoza uvamizi wa Urusi nchini Ukraine na kuuteka mji wa Bakhmut. Sasa urafiki na Putin umefika mwisho kwa madai kwamba viongozi wa Jeshi la Urusi wanamhujumu.
Juzi Mwamba akaongoza vikosi vyake kwenda Moscow, kwa madai kwamba anataka viongozi wa jeshi akiwemo waziri wa Ulinzi waondolewe. Vikosi vikafika mpaka Kilomita 200 kutoka Moscow.
Putin akawasha ndege akaikimbia Moscow. Viongozi wa Magharibi na Amerika wanasema tukio la jana limefunua udhaifu wa Putin.
Putin akamtuma msela wake Rais wa Belarus. Wakakubaliana, mwamba akasitisha uasi akageuza majeshi .
Sasa mwamba anaenda kuishi Belarus na wanajeshi wake hawatashitakiwa kwa tukio la jana.Lakini kuna tetesi kwamba mwamba hatakaa muda mrefu Belarus bali ataondoka na kuja kuishi msituni huku Afrika....!!
mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa mwezi huu hadi sasa bado hajafanya uamuzi wa wapi atacheza kwa msimu ujao.

#Benfica