Makapuku Forum

Makapuku Forum

.
MBALI ya ofa nono ya zaidi ya Pauni 40 milioni kwa mwaka kutoka Saudi Arabia, mshambuliaji wa Crystal Palace, Wilfried Zaha, 30, amepokea ofa pia kutoka Lazio.
.
Staa huyu wa kimataifa wa Ivory Coast mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa mwezi huu hadi sasa bado hajafanya uamuzi wa wapi atacheza kwa msimu ujao.
Screenshot_20230625_144840_Instagram.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
.
ARSENAL inataka kuwasilisha ofa nyingine mpya kwa Klabu ya Ajax kwa ajili staa wa timu hiyo, Jurrien Timber baada ya ofa yao ya mara ya kwanza kukataliwa. Awali Arsenal iliweka mezani Pauni 30 milioni lakini Ajax ilikataa na kusisitiza kwamba staa huyo hataondoka kwa chini kiasi chini ya Pauni 50 milioni.
.
Timber ambaye alikuwa akitakiwa na Kocha wa Manchester United, Erik ten Hag katika dirisha la majira ya joto, amedhamiria kutua uwanjani Emirates.

Screenshot_20230625_144951_Instagram.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
PSG YAMTAKA KWELI OSIMHEN
.
PSG imeripotiwa kuwa tayari kulipa Pauni 129 milioni zinazotakiwa na Napoli ili kumsajili straika Mnigeria Victor Osimhen kwenye dirisha hili la uhamisho wa majira ya kiangazi. Osimhen amekuwa gumzo kwelikweli huko Ulaya utokana na kiwango bora alichokionyesha msimu wa 2022-23, akifunga mabao 26 kwenye ligi na matano Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Screenshot_20230625_145230_Instagram.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
LIVERPOOL WAPO KWA TCHOUAMENI
.
Liverpool imeripotiwa kuweka ofa ya Pauni 47.3 milioni kumnasa kiungo wa Real Madrid, Aurelien Tchouameni. Liverpool ilihusishwa kumsajili staa huyo wa kimataifa wa Ufaransa dirisha lililopita, lakini ilishindwa kuwalipa Monaco na kuwafanya Madrid kunasa saini yake.

Screenshot_20230625_145320_Instagram.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
BAADA ya Azam FC kumtema aliyekuwa kiungo wa timu hiyo, Kenneth Muguna, nyota huyo Mkenya amegeuka lulu kwa timu za Bandari, Gor Mahia zote za Kenya na Namungo kuonyesha nia ya kuitaka saini yake.
Screenshot_20230625_145413_Instagram.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Arsenal yasonga mbele katika mazungumzo ya kumsajili Roméo Lavia. Mazungumzo yanaendelea na Southampton na kambi ya mchezaji lakini bado hakuna ofa rasmi!

Southampton wanatumai ada ya rekodi kwa mchezaji wa U21. Man Utd wanavutiwa lakini kipaumbele ni Mason Mount. Chelsea pia wakifuatilia kwa ukaribu.

Screenshot_20230625_145802_Instagram.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Meneja wa Bayern Munich Thomas Tuchel ameiomba klabu hiyo kumnunua kiungo wa kati wa Barcelona na Uholanzi Frenkie de Jong, 26, baada ya kujiondoa kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili Muingereza Declan Rice, 24, kutoka West Ham.. (Foot Mercato)

Screenshot_20230625_145859_Instagram.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Pep Guardiola amebaini mbadala wa Kyle Walker 32, ambaye anahusishwa kujiunga na FC Bayern

Sasa klabu ya Manchester City wanafikiria kuwasilisha ombi la kumnunua beki wa kulia wa Paris St-Germain Achraf Hakimi, 24, na "haitasita" kulipa ada kubwa kwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Morocco. (Marca)

Screenshot_20230625_145945_Instagram.jpg
 
Manchester United wanapania kumnunua mlinda mlango wa Cameroon na Inter Milan Andre Onana, 27, huku kukiwa na uwezekano mkubwa wa Mhispania David de Gea, 32 kuondoka Old Trafford msimu huu wa joto. (90 min)

United pia inamfuatilia kipa wa Porto na Ureno Diogo Costa, 23, na kipa wa Brentford na Uhispania David Raya, 27, kama mbadala wa David de Gea. (Sky Sports)

Screenshot_20230625_150433_Instagram.jpg
 
West Ham wanaamini kwamba ofa ya tatu ya Arsenal ya karibu £100m kwa nahodha wao Declan Rice, 24, iko karibu huku mpango wa uhamisho wa kiungo huyo wa kati wa Uingereza ikikaribia kukamilika. (Mail)
Screenshot_20230625_150530_Instagram.jpg
 
Manchester United wanafikiria kumpa winga wa Argentina Alejandro Garnacho, 18, jezi nambari saba, ambayo ilivaliwa mara ya mwisho na Cristiano Ronaldo. (Manchester Evening News)
Screenshot_20230625_150622_Instagram.jpg
 
Borussia Dortmund wanaweza kumnunua kiungo wa kati wa Chelsea na Uingereza Conor Gallagher, 23, kama mbadala wa Jude Bellingham. (Bild via Caught Offside)

Screenshot_20230625_150906_Instagram.jpg
 
Makamu Mwenyekiti mstaafu wa Chama cha Mapinduzi (CCM)-Bara, John Malecela ameshukuru miradi ya maendeleo iliyoanzishwa na Rais wa awamu ya tano, Hayati John Magufuli huku akimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyoiendeleza.

Malecela ambaye pia ni Waziri Mkuu mstaafu wa saba wa Tanzania ameyasema hayo leo Jumapili Juni 25, 2023 nyumbani kwake Kilimani, Dodoma alipokutana na waandishi wa habari kuzungumzia jitihada zinazofanywa na Rais Samia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini.

Samia aliyekuwa makamu wa Rais kuanzia Novemba 5, 2015 baada ya uchaguzi mkuu huku Rais akiwa John Magufuli, aliapishwa kuwa Rais Machi 19, 2021 baada ya Magufuli kufariki dunia Machi 17.

Malecela amewataka Watanzania kumpa nafasi Rais Samia ambaye anafanya kazi usiku na mchana katika kuliletea maendeleo Taifa hili.

“Kwa mfano, katika Tanzania baada ya miezi 12, tukifika mpaka mwaka kesho reli ya SGR au reli ya mwendokasi itakapokuwa tayari, Watanzania tutakuwa katika dunia mpya, dunia ambayo unatoka Dar es Salaam mpaka Dodoma kwa saa tatu, saa moja na nusu Morogoro, saa moja na nusu Dodoma kwa treni ya mwendokosi.

“Na nadhani tutakuwa katika nchi chache za Bara la Afrika zenye aina hiyo ya usafiri. Sasa hii italeta maana gani, italeta maana kwamba wenzetu wa Rwanda, Burundi, Congo nao watafaidika, kwa sababu mizigo yao kutoka Dar es Salaam mpaka Kigoma itachukua muda mfupi zaidi,” amesema.

Screenshot_20230625_151023_Instagram.jpg
 
Wananchi wa Kijiji cha Kisimiri Juu Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha wamemuomba, Rais Samia Suluhu kuwaboreshea miundombinu mbinu ya kilimo cha umwagiliaji sambamba na barabara ili waachane na kilimo cha bangi.

Wananchi hao wameyasema hayo leo Jumapili Juni 25, 2023 mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan katika maadhimisho ya siku ya kupinga madawa ya kulevya duniani ambayo kitaifa yamefanyika mkoani Arusha.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi hao, mwenyekiti wa Kijiji hicho, Mbayani Kuresoi alisema ili kuacha kilimo cha Bangi Kisimiri Juu ni lazima waboreshewe miundombinu ya kilimo kwa ajili ya mazao mengine.

"Tumepewa elimu na kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Arusha na kamishna wa madawa ya kulevya nchini sasa tumetambua kuwa kumbe bangi ni mbaya lakini tunahitaji tutengenezewe barabara na tuletewe maji ili tulime mazao mengine,”amesema.

Amesema kuwa katika eneo lake mazao ya mahindi, Pareto, maharage na viazi mviringo vinastawi lakini wananchi wanashindwa kujishughulisha nayo kutokana na uhaba mkubwa wa maji lakini pia barabara mbovu.

"Mheshimiwa Rais tunaomba kabla hujaondoka uje ututembelee uone jinsi tulivyo na maeneo makubwa na utoe elimu lakini uangalie namna ya kutuboresha maana watu wako tayari kuachana nacho (kilimo cha bangi)," amesema Kuresoi.

"Wananchi wa Kisimiri hawakujua madhara ya bangi kwani hawavuti bali wanauza Kama kilimo cha biashara, lakini elimu tuliyopata tumejua kumbe tunaharibu wenzetu,"ameongeza.

Screenshot_20230625_151132_Instagram.jpg
 
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema chama hicho hakina chuki wala hila katika msimamo wao wa kutokubaliana na hatua ya Serikali kuingia makubaliano na Serikali ya Dubai kuhusu uwekezaji wa bandari.

Oktoba 25, 2022, Serikali hizo mbili ziliingia makubaliano katika ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kwa ajili ya uendelezaji na uboreshaji wa utendaji kazi wa bandari uendeshaji wa miundombinu ya kimkakati ya bandari za bahari na maziwa makuu, maeneo maalumu ya kiuchumi, maegesho ya utunzaji mizigo na maeneo ya kanda za kibiashara.

Mbowe ambaye ni mbunge wa zamani wa Hai mkoani Kilimanjaro ametoa msimamo huo jana Jumamosi Juni 24, 2023 wakati akizungumza na wanadaispora wa Uingereza, nchini humo. Katika mkutano huo Mbowe aligusuia masuala ya kijamii, kiuchumi na kisiasa.

“Hatupingi jambo kwa sababu tuna chuki, hila au wivu bali tunataka Taifa letu liwe mahali salama bora zaidi kwa kuishi. Chadema tulishauri kabla ya kupitishwa Serikali ya Tanzania na Zanzibar kuketi ili kuondoa sintofahamu na kasoro zilizopo, sambammba na kuwapa muda wananchi kuujadili,”amesema Mbowe.

Mbowe ambaye ni kiongozi wa zamani wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni (KUB), amesema sakata hilo linagusa maslahi ya Watanzania wote bara na visiwani, akisisitiza suala hilo sio dogo na halitaishia katika mipaka ya Tanzania.
Screenshot_20230625_151334_Instagram.jpg
 
Waziri Mkuu mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, John Malecela ametoa kauli kuhusu sakata la makubaliano ya uwekezaji wa bandari nchini na Serikali ya Dubai kupitia Kampuni ya Dubai Port World (DPW).

Malecela ametoa kauli hiyo leo Jumapili Juni 25, 2023 baada ya kuulizwa swali kuhusiana na uwekezaji huo unaohusisha Serikali hizo mbili.

Malecela amesema haoni shida ya uwekezaji huo na amewashangaa wanaopinga akisema ndio demokrasia inavyowaruhusu.

“Kwanza wako wachache wanaopinga na sioni hoja yao,” amesema Malecela ambaye ni Waziri Mkuu wa saba wa Tanzania akipokea nafasi hiyo kutoka kwa Jaji Joseph Warioba.

Leo, Malecela amekutana na waandishi wa habari nyumbani kwake eneo la Kilimani jijini Dodoma akielezea kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Screenshot_20230625_151435_Instagram.jpg
 
Kama moja ya njia ya kuzuia machafuko na umwagaji damu mjini Moscow nchini Russia, Mkuu wa jeshi binafsi la Wagner, Yevgeny Prigozhin ameghailisha mpango wa jeshi hilo kuuvamia mji huo; na kukubali kwenda kuishi uhamishoni katika nchi ya Belarus ambayo kimsingi ilikuwa moja ya majimbo ya Umoja wa Kisoviet tangu 1919 hadi 1991.

Hatua hii inakuja baada Rais wa Belarus Alexander Lukashenko kufanya mazungumzo na kiongozi wa kundi hilo la Wegner ili kusitisha maasi.

Bosi huyo wa Wagner aliagiza vikosi vyake kutokwenda Moscow kwa kile alichokiita kuzuia umwagaji damu na kukubali kwenda kuishi uhamishoni nchini Belarus na hivyo kuhitimisha moja ya changamoto kubwa kuwahi kutokea katika utawala Rais Vladimir Putin.

Prigozhin amesema, wakati majeshi yake yakiwa kama kilometa 200 kuufikia mji mkuu wa Moscow aliamua kuwarejesha askari wake ili kuzua mauaji.
Screenshot_20230625_151541_Instagram.jpg
 
Siku 11 tangu simba walipovamia baadhi ya vijiji vya Kata za Kiponzelo, Maboga na maeneo ya Tanangozi, Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Veronica Kessy ametoa tahadhari kwa wananchi kutotembea usiku na kuwa kwenye makundi nyakati za mchana.

Mbali ya kuagiza muda wa mwisho wa matembezi kuwa saa 11 jioni, pia amewataka wananchi kutowafukuza simba wanapovamia mazizi ya mifugo yao ili washibe na kutoleta madhara kwa binadamu.

Wakati Kessy akieleza njia za kufanya ili kujihadhari na simba, Hifadhi ya Taifa Ruaha jana ilianza kutumia helikopta kuwasaka wanyama hao ambao mpaka sasa wameua ng’ombe 11, nguruwe mmoja na kuku.

Tangu simba wavamie kwenye vijiji mbalimbali, hofu imetanda miongoni mwa jamii na kuwafanya wananchi washindwe kutembea kwa uhuru, hasa usiku.

Akizungumza na Mwananchi, Kessy alisema simba huanza kutembea usiku kutafuta chakula, hivyo ni vizuri muda huo wananchi wasitembee ikiwa ni mojawapo ya mbinu ya kujihami.

Screenshot_20230625_151649_Instagram.jpg
 
Huyu ndiye Cleopatra.. yule Malkia na Firauni wa mwisho wa Misri ya kale.. inadaiwa Cleopatra alikuwa mwanamke mzuri... sasa bana tangu nianze kuandika hakuna historia ambayo imekuwa ikinichanganya na kunipa ugumu kuandika kama ya Cleopatra..

Maribu miaka 3 naandika Story ya Cleopatra... naandika mpaka mwisho nikimaliza kuandika nikisoma mwenyewe nashindwa kuelewa.. Maisha ya Cleopatra yalijaa utata mwingi...Cleopatra alikuwa mwanamke ambaye anaweza kutumia chochote alinacho hata mwili wake kufanikisha malengo yake..

Ukigeuka huku Cleopatra kaolewa na mdogo wake.. Cleopatra aliwahi kuolewa na mdogo wake toka nitoke, tena mdogo wake akiwa na umri wa miaka 10 Cleopatra yeye akiwa na umri wa miaka 18..

Ukigeuka huku Cleopatra kaolewa na Julius Caesar..huku Cleopatra kazaa na Mark Anthony... yaani ni full mkanganyiko... mimi nimeshindwa bana....!
Screenshot_20230625_151805_Instagram.jpg
 
Baraza la Tiba Asili na Tiba mbadala limepiga marufuku uingizaji, usambazaji, uuzaji na utumiaji wa kinywaji cha kuongeza nguvu kiitwacho AKAYABAGU baada ya kufanya uchunguzi na kugundua kuwa kinywaji hicho hakijawahi kusajiliwa na Baraza hilo Nchini.

Taarifa ya Baraza hilo imesema pia limegundua kuwa kimechanganywa na dawa ya kisasa aina ya sildenafil (Viagra majina mengine Erecto ama Vega) jambo ambalo ni kinyume cha sheria hivyo Watumiaji wamedanganywa na Wahusika ambapo kwa kitendo cha kuchanganywa na Sildenafil (Viagra) kinywaji hiko sio tena cha tiba asili bali ni kinywaji chenye viagra.

“Kuanzia tarehe 23/06/2023 Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala linapiga marufuku uingizaji, usambazaji, uuzaji na utumiaji wa kinywaji hiki kote nchini, yeyote atakayekiuka agizo hilo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake na vilevile atakayepatikana akiwa na kinywaji cha AKAYABAGU atakuwa ametenda kosa na ataweza kushitakiwa kwa mujibu wa Sheria” View attachment 2667331
saa itajuaje
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom