Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Warda Obathany kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Iramba mkoani Singida leo Jumatano Juni 7, 2023.
Warda ambaye ni mjasiriamali pia amewahi kugombea nafasi ya NEC kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT).
Screenshot_20230608_053359.jpg
 
Rais samia amemteua Mtela Mwampamba kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Songea ambapo uteuzi huo ulianza jana Jumanne Juni 6, 2023.

Mwampamba aliwahi kuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe kabla ya uteuzi wake kutenguliwa na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, John Magufuli Juni 28, 2020.

Screenshot_20230608_053457.jpg
 
Taarifa za chini chini zilizotufikia Mwananchi linajua kabla ya jua kuzama leo Jumatano, Feisal Salum 'Fei Toto' atatambulishwa rasmi ndani ya Azam.

Licha ya Azam kufanya siri, lakini Mwananchii linajua klabu hiyo ilimalizana na Yanga jana jijini Dar es Salaam baada ya kikao kizito cha pande zote mbili.

Hatua hiyo imekuja baada ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kuwaomba Yanga kumaliza mgogoro na kiungo huyo ili mambo mengine yaendelea.

Fei aliingia kwenye mgogoro huo, baada ya kuvunja mkataba bila kuzingatia kanuni, hadi kesi kupelekwa kwenye Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) bado Yanga ikawa kwenye upande wa haki.

Screenshot_20230608_053627.jpg
 
WEST HAM MABINGWA CONFERENCE LEAGUE
.
FT: FIORENTINA 1-2 WEST HAM
62’—️ Said Benrahma
67’—️ Giacomo Bonaventura
89’—️ Jarrod Bowen
Screenshot_20230608_053812.jpg
 
MESSI ANUKIA MAREKANI, BECKHAM ASIMAMIA SHOO
.
Baada ya Tetesi za kuhusishwa kurudi Barcelona au kwenda Saudi Arabia, supastaa Lionel Messi amekubali kujiunga na klabu ya Inter Miami inayoshiriki Ligi Kuu ya Marekani (MLS)
.
Asilimia za Messi kujiunga na Inter Miami zinaonekana kuwa nyingi kutokana na ushawishi mkubwa uliopo wa mmiliki wa timu hiyo, David Beckham ambaye ana uhusiano mzuri na staa huyo.

Screenshot_20230608_053932.jpg
 
KAMA Mtibwa Sugar itafanikiwa kubaki Ligi Kuu msimu ujao basi huenda ikamrudisha tena kikosini hapo aliyewahi kuwa kiungo wake, Said Ndemla anayekipiga kwa sasa Singida Big Stars.
.
Taarifa zinaeleza mazungumzo ya pande hizo mbili yameanza na huenda Mtibwa ikampata Ndemla kiulaini kutokana na kile kinachodaiwa, hana furaha ndani ya Walima Alizeti hao wa kanda ya kati.
Screenshot_20230608_054050.jpg
 
SIMBA imekuwa na utaratibu mara kwa mara wa kuwatafutia baadhi ya mastaa wao sehemu za kuishi na wachezaji wengi wa timu hiyo wanaishi kwenye Apatimenti maeneo ya Mbezi jijini Dar es Salaam. Hizi ni za kishua Zaidi.
.
Kundi kubwa la wachezaji wa Simba pamoja na baadhi ya watu wa benchi la ufundi wanaishi kwenye eneo hilo ambalo inaidaiwa kuna makubaliano maalumu kati ya timu hiyo na uongozi wa Apatimenti hiyo.
.
Chanzo kinaonyesha kuwa kila mmoja analipa kitita cha dola 700 kwa mwezi mmoja. Sawa na Sh1.6Milioni. Mastaa wanaoishi hapo ni Sadio Kanoute, Peter Banda, Pape Sakho, Jean Balek, Augustine Okrah na wengine wengi wanaotoka nje ya nchi.
.
Mastaa hawa wa Simba kwenye usafiri wengi wamekuwa wakikodi kutoka kwenye makampuni mbalimbali, lakini wakati mwingine wamekuwa wakitumia ya wachezaji wenzao au marafiki. Ingawa tunajua kwamba kwenye mikataba yao kuna sehemu kuna makubaliano ya kupewa gari ila baadhi yao hutaka kupewa fedha tasilimu na kuweka mifukoni na kutumia ya kukodi.
Screenshot_20230608_054221.jpg
 
WINGA wa Yanga, Dickson Ambundo anahusishwa na kuhamia Dodoma Jiji msimu ujao. Ambundo alijiunga Yanga mwanzoni mwa msimu wa 2021/2022 akitokea Dodoma Jiji lakini ameshindwa kuwa na muendelezo wa ubora wake na mara nyingi kuishia benchi jambo ambalo uongozi wa Wanajangwani hao umepanga kuachana naye huku Dodoma ikitajwa kumhitaji.
Screenshot_20230608_062349.jpg
 
UBORA aliouonyesha Mayele msimu huu kwenye mashindano ya Kimataifa umewavutia vigogo wa Afrika na tayari kuna Ofa kubwa kutoka: Zamalek, Esperance na Kaizer Chiefs.
Screenshot_20230608_062444.jpg
 
LEICESTER YATEMA MASTAA SABA MATATA
.
Leicester City imethibitisha imewatema mastaa saba baada ya mikataba yao kufika ukomo. Leicester City imeshuka daraja kutoka kwenye Ligi Kuu England na sasa ipo kwenye mchakato wa kujijenga na kujipanga upya ili wasikae muda mrefu huko kwenye Championship.
.
Miongoni mwa wachezaji waliochwa ni kiungo wa kimataifa wa Ubelgiji, Youri Tielemans, ambaye amekuwa akihusishwa na klabu kibao za Ligi Kuu England zinazohitaji saini yake. Mastaa wengine ni Caglar Soyuncu, Daniel Amartey, Nampalys Mendy, Ryan Bertrand, Ayoze Perez na Tete ambao bila ya shaka watasababisha vita kali kutoka kwa klabu nyingine zitakazowania kunasa saini zao.

Screenshot_20230608_062555.jpg
 
SPURS YAMTAKA WATKINS AVAE BUTI ZA KANE
.
Tottenham Hotspur imeripotiwa kumweka kwenye mpango wao straika wa Aston Villa, Ollie Watkins kama mchezaji wa kwenda kuvaa buti za Harry Kane endapo kama ataondoka kwenye kikosi hicho dirisha hili la uhamisho wa majira ya kiangazi huko Ulaya.
.
Watkins, 27, alikuwa kwenye kiwango bora sana kwenye Ligi Kuu England msimu wa 2022-23 alipofunga mabao 15 na kuisaidia Aston Villa kumaliza nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi hiyo na kukamatia tiketi ya kucheza michuano ya Europa Conference League msimu ujao.
.
Watkins alitua Villa Park akitokea Brentford mwaka 2020 na tangu muda huo kiwango chake kimekuwa kikipanda.

Screenshot_20230608_062650.jpg
 
TEN HAG AMTULIZA LINDELOF, HAONDOKI
.
Kocha wa Manchester United, Erik ten Hag amefanya uamuzi wa kubaki na huduma ya beki wa kati Victor Lindelof baada ya kukoshwa na kiwango chake. Sasa beki huyo wa kati raia wa Sweden atapewa ofa ya mkataba mpya baada ya kumalizia msimu huu katika kiwango bora kabisa cha ndani ya uwanja.
.
Mkataba wake wa sasa huko Old Trafford utafika tamati mwakani na Man United imeamua kukifanyia kazi kipengele cha kumwongezea mwaka mmoja zaidi kilichokuwa kimewekwa kwenye mkataba huo.

Screenshot_20230608_062844.jpg
 
Mchezaji wa Manchester City Ilkay Gundogan, 32, huenda akarejea Borussia Dortmund msimu huu wa joto kwa sababu Barcelona hawana uwezo wa kulipa mshahara wa kiungo wa kati wa Ujerumani ambaye mkataba umemalizika. (Bild- Germany)

Barca wamejaribu kumshawishi Gundogan kwa kuongeza ofa yao ya mkataba hadi miaka mitatu na kupunguzwa mishahara, wakati Arsenal wametoa mkataba wa miaka miwili na pendekezo la faida kubwa pia linatarajiwa kutoka kwa klabu ya Saudi. (Sport-Spain)

Screenshot_20230608_063011.jpg
 
Aston Villa wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili mchezaji huru Youri Tielemans, 26, baada ya kiungo huyo wa Ubelgiji kuondoka Leicester. (Athletic)

Screenshot_20230608_063124.jpg
 
Chelsea imeungana na Barcelona na Liverpool katika mbio za kuwania saini ya kiungo wa Celta Vigo ya Uhispania Gabri Veiga. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 ana kifungu cha kuachiliwa cha pauni milioni 34.4. (Guardian)
Screenshot_20230608_063218.jpg
 
Kiungo wa Chelsea na Ufaransa N'Golo Kante, 32, anapewa mshahara ambao unaweza kufikia £86.2m kwa mwaka na klabu za Saudi Al-Ittihad na Al-Nassr. (Guardian)
Screenshot_20230608_063342.jpg
 
Tottenham Hotspur wameonyesha nia ya kumnunua mlinzi wa Manchester United na England Harry Maguire, 30, na wanatumai kuwa wanaweza kumshawishi mchezaji mwenzake wa kimataifa Harry Kane kusalia katika klabu hiyo. (Telegraph)
Screenshot_20230608_063454.jpg
 
KOMBE JIPYA LIGI KUU YA NBC

Kwa mujibu wa TFF hili kombe la msimu huu lilinunuliwa kwa dollar $60,000-$100,000. (Tsh 140,000,000-237,000,000)
Screenshot_20230608_063705.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom